WhatsApp%2BImage%2B2019-03-08%2Bat%2B10.53.19%2BAM
WhatsApp%2BImage%2B2019-03-08%2Bat%2B10.53.22%2BAM
WhatsApp%2BImage%2B2019-03-08%2Bat%2B10.53.25%2BAM
 Mwili wa Daimon Munishi ukitolewa kwenye Korongo la maji Makando lililopo katika kijiji cha Isawerwa kata ya Romu wilayani Hai.
WhatsApp%2BImage%2B2019-03-08%2Bat%2B10.53.16%2BAM
 Mkuu wa wilaya ya Hai,Lengai Ole Sabaya (mwenye kofia) alitizama mwili uliokutwa katika Korongo la maji Makando lililopo katika kijiji cha Isawerwa kata ya Romu wilayani Hai.
WhatsApp%2BImage%2B2019-03-08%2Bat%2B10.53.28%2BAM
 Mwili wa Daimon Munishi ukipandishwa kwenye gari la polisi mara baada ya kutolewa kwenye Korongo la maji Makando lililopo katika kijiji cha Isawerwa kata ya Romu wilayani Hai.
WhatsApp%2BImage%2B2019-03-08%2Bat%2B10.53.31%2BAM
 WhatsApp%2BImage%2B2019-03-08%2Bat%2B10.53.37%2BAM
Mkuu wa wilaya ya Hai,Lengai Ole Sabaya ( mwenye kofia) akitoa pole kwa wananchi waliofika eneo la tukio wakati wa kutoa mwili wa marehemu kwenye Korongo la maji Makando lililopo katika kijiji cha Isawerwa kata ya Romu wilayani Hai.
WhatsApp%2BImage%2B2019-03-08%2Bat%2B10.53.34%2BAM
 Katibu tawala wilaya ya Hai,Upendo Wera akitoa pole kwa wananchi wa eneo hilo

MTU mmoja aliyefahamika kwa jina la Diamon Munishi (87) amekutwa amefariki dunia katika Korongo la maji Makando lililopo katika kijiji cha Isawerwa kata ya Romu wilayani Hai.

Kwa mujibu wa mashuhuda wameeleza kuwa marehemu alikua na tatizo la uoni hafifu na kwamba alianguka kwenye korongo wakati mvua kubwa iliyoambatana na upepo mkali ikinyesha.

Mkuu wa Polisi wilaya ya Hai Lwelwe Luhaga Mpina alithibitisha kufariki dunia na kwamba kifo chake ni cha kawaida kutokana na  matatizo aliyokuwa nayo marehemu.


Mkuu wa wilaya ya Hai,Lengai Ole Sabaya alifika eneo la tukio na kutoa pole kwa familia iliyofikwa na msiba wa mzee wa huyo.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: