Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro amefanya mabadiliko ya baadhi ya Makamanda wa Polisi nchini ambapo aliekuwa Kamanda wa Polisi Viwanja vya ndege, Naibu Kamishna (DCP) Matanga Mbushi anakwenda kuwa Mkuu wa vikosi vya Polisi, Kamisheni ya Operesheni na Mafunzo Makao Makuu.

Nafasi ya DCP Mbushi inachukuliwa na aliyekuwa Afisa Mnadhimu Mkoa wa Mara, Kamishna Msaidizi(ACP) Jeremiah Shilla.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: