Mkuu wa wilaya ya Ngorongoro Rashid Mfaume Taka akimkabidhi Mwenge wa uhuru mkuu wa wilaya ya Karatu Bi Theresia Mahongo kwa ajili ya kuendelea na majukumu ya mwenge wilayani humo.
Katikati ni kiongozi wa mbio za mwenge wa uhuru Taifa 2018 Ndg:Charles Kabeho akizundua mradi wa shamba la kilimo cha vitunguu katika kijiji Cha Dofa wilayani karatu.
Nyumba mpya ya waalimu 6 by one shule ya sekondari Baray iliyopo wilayani karatu iliyo zinduliwa na Kiongozi wa mbio za mwenge wa uhuru Ndg: Charles F. Kabeho wilayani humo.
Wakwanza kulia ni Mkuu wa wilaya ya Karatu Bi Theresia Mahongo akishuhudia uzinduzi wa nyumba za walimu 6/1 katika shule ya sekondari Baray ujenzi wa nyumba hizo zinakadiriwa kuwa zaidi ya milion 141 kwa ushirikiano na wananchi.



Na Imma Msumba, Karatu

Baada ya kiongozi wa mbio za Mwenge wa uhuru kitaifa Ndg:Charles Francis Kabeho kukamilisha ziara ya mwenge wilaya ya ngorongoro ambapo katika wilaya hiyo miradi 6 imezinduliwa na kiongozi huyo.

Miongoni mwa miradi iliyozinduliwa ni pamoja na mradi wa vyoo chenye matundu 10,bweni la wanafunzi wa sekondari,maabara ya kisasa ya kemia na fizikia katika shule ya nainokanoka,barabara ya kiwango cha changarawe kutoka Eneo la Errikepus mpaka nainokanoka,mradi wa maji safi na salama pamoja josho la kisasa kwa ajili ya mifugo katiaka hiyo na vijiji jirani.

Septemba 13 kiongozi wa mbio za mwenge wa uhuru kitaifa ndg Charles Kabeho anatarajiwa kuzindua na kukagua maendeleo ya miradi zaidi ya 6 kwa kushirikiana na mkuu wa wilaya ya Karatu Theresia Mahongo.

Katika wilaya ya karatu kijiji cha Dofa amezindua mradi wa Kilimo cha vitunguu katika shamba la bonde la Eyasi na kutembelea shamba la muekezaji mzalendo ndg Gilole katika kijiji cha Qang'ded baray.

Shamba hilo lenye zaidi ya hekari zaidi ya 70 limekuwa chachu ya kujiingizia kipato kwa wananchi ambapo kwa mujibu wa taarifa ya mradi huo zaidi ya wananchi 200 wamekuwa wakifanya kazi ndogondogo na kujipatia fedha kwa ajili ya kujikimu katika maisha yao ya kila siku.

Miradi mingine inayo tarajiwa kuzinduliwa na kukaguliwa  ni pamoja na uzinduzi wa nyumba za walimu 6 kwa moja shule ya sekondari Baray,kuzindua kikundi cha vijana katika kampeni ya Tuwalinde vijana wetu,kufungua ofisi ya kijiji kwa ajili ya utoaji huduma.

Share To:

msumbanews

Post A Comment: