Diwani wa kata ya Kingori kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema Ndg. Peter Kesi Pamoja na Mwenyekiti wa Kijiji cha  Mboreni Ndg. Enock Mbise wametangaza kujiuzulu nyadhifa zao zote na kujiunga na Chama cha Mapinduzi Ccm mapema hii leo.



Ndg.Kesi ameeleza kuwa amechukua maamuzi hayo baada ya Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mh.Jerry Muro  kufanya ziara katika kata ya kingori  kwa ajili ya kutatua kero mbalimbali za wananchi katika kata hiyo baada ya kutatua kero hizo Diwani huyo na mwenyekiti wa Kijiji waliamua kuchukua uamuzi huo baada ya kufurahishwa na kazi nzuri anazofanya Rais wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na serikali ya awamu ya tano.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: