Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Leo imekabidhi Pikipiki zaidi ya 2500 kwa  Waratibu Elimu Kata ili ziwasidie katika kutekeleza majukumu yao kwa lengo la kuimarisha Elimu hapa nchini.

Pikipiki hizo zinakabidhiwa Leo Jijini Dar es Salaam na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa  Joyce Ndalichako ambapo amesema Wizara ya Elimu kupitia Mradi wa Kukuza Stadi za Kusoma, Kuandika na Kuhesabu (LANES)  umenunua Pikipiki hizo 2894 kwa zaidi ya shilingi bilioni  Nane.

Waziri Ndalichako amesema pikipiki hizo zitasambazwa nchi nzima kupitia Ofisi ya Rais TAMISEMI.

"Rais alipoingia madarakani alihaidi kuimarisha ubora wa Elimu, sasa moja ya mikakati ya kutekelez hilo ndiyo maana hii Leo tunashuhudia vitendea Kazi hivi ambavyo vitasambazwa nchi nzima, lengo hapa ni kuhakikisha Elimu  inayotolewa inakuwa bora na kuhakikisha  nchi inakuwa na matokeo chanya kiuchumi” amesema Ndalichako.

Waziri Ndalichako pia amewataka waratibu elimu Kata hao kuhakikisha pikipiki hizo zinatumika kwa ajili yakusimamia elimu katika maeneo yao na kupandisha ufaulu na si vinginevyo.

Kwa upande wake Waziri wa nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI Selemani Jafo amewataka waratibu elimu kata kuhakikisha wanasimamia taaluma katika maeneo yao.

Aidha, Jafo amewaagiza Wakurugenzi wa Mikoa, Halmashauri, Manispaa na Majiji kuweka utaratibu wa kuzihudumia pikipiki hizo katika maeneo yao.

Imetolewa na:
Kitengo Cha mawasiliano Setikalini
WIZARA YA ELIMU, SAYSNSI NA TEKNOLOJIA
3/7/2017
Share To:

msumbanews

Post A Comment: