Mfanyabiashara maarufu na mzazi mwenza wa staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz, Zarinah Hassan amethibitisha kuwa yeye ni Bosslady kweli baada ya kuweka wazi kuwa amenunua gari aina ya Range Rover lenye thamani ya shilingi milioni 171,337,500.

Zari alitangaza mpango wake wa kununua gari hilo wiki chache zilizopita na hatimaye wikiendi hii alilianika gari hilo jipya na kuliweka Kwenye mitandao ya kijamii.

Mara baada ya kuweka gari hilo kuna habari zilizuka kuwa amenunuliwa gari hilo na mpenzi wake taarifa alizozikana na kuweka wazi kuwa amenunua gari lile kwa hela zake mwenyewe.

Lakini pia Zari ameweka wazi mipango yake ya kuanzisha Food franchise kama vile KFC au McDonalds.

Share To:

msumbanews

Post A Comment: