Hatimaye mrembo Agnes Gerald maarufu kwa jina la Masogange ameachiwa huru katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu baada ya kulipa faini ya kei iliyokuwa inamkabili.
Masogange ambaye leo (Jumanne) alipatikana na hatia ya makosa mwawili ya kutumia dawa za kulevya.
Kosa la kwanza ni kutumia dawa za kulevya aina ya heroine, na la pili kutumia dawa za kulevya aina ya 0xazepam.
Mahakama hiyo ilimuhukumu mrembo huyo kwenda jela miaka mitatu au kulipa faini ya shilingi milioni 1.5 za kitanzania ambapo Masogange amefanikisha kulipa faini hiyo.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: