Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa amesema wanamshikilia Fatuma Chikawe kwa tuhuma za kudanganya kuwa ni mtoto wa Waziri Mkuu mstaafu, Edward Lowassa.

Hii ni wiki moja baada ya Fatuma kujitokeza kwenye vyombo vya habari na kudai ametelekezwa na Lowassa kwenye zoezi la kusikiliza malalamiko ya wanawake waliotelekezewa watoto linaloendeshwa chini ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda, ambaye alisisitiza wahusika watoe taarifa za ukweli.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: