Mabingwa wa tetezi wa ligi kuu soka Tanzania Bara klabu ya Yanga hii leo wamefanya mazoezi ya mwisho kabla ya kuivaa timu ya Township Rollers FC michuano ya klabu bingwa Barani Afrika.
Yanga SC itashuka katika uwanja wa Taifa wa Botswana hapo kesho majira ya saa 10:45 jioni kucheza na wenyeji wao Township.
Yanga SC itashuka dimbani huku ikiwa na kumbukumbu ya kupoteza mchezo uliyooita uliyopigwa jijini Dar es Salaam kwa jumla ya mabao 2 – 1 kutoka kwa Township Rollers FC na hivyo italazimika kuchomoza na ushindi ili kujihakikishia inasonga mbele.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: