Klabu ya soka ya Real Madrid imezidi kujiweka katika nafasi mbaya ya kushinda taji la ligi kuu ya Hispania (La Liga) baada ya usiku wa jana kukubali kichapo cha goli 1-0 kutoka kwa Espanyol.

Madrid ambao walikuwa katika uwanja wa ugenini wa RCD Espanyol, walifungwa goli hilo na Gerard Moreno katika dakika ya 90 ya mchezo.

Hata hivyo Cristiano Ronaldo wa Madrid hakuwepo katika mcheo huo.

Kutokana na matokeo hayo, Real inabakia katika nafasi yake ya tatu kwenye msimamo wa ligi akiwa na alama zao 51 huku akiwa mbele kwa mchezo mmoja, wakati huo huo Barcelona ndio anaongoza msimamo huo akiwa katika nafasi yake ya kwanza na alama 65.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: