Fatuma Juma, mkazi wa Mombasa, alikuwa amezoea maisha ya upweke kwa karibu miaka mitatu baada ya mume wake kumwacha bila maelezo. Kila siku alijikuta akijiuliza ni wapi alikosea katika ndoa yao iliyodumu kwa miaka saba kabla ya matatizo kuanza.

Kwa mujibu wa Fatuma, mume wake alianza kubadilika ghafla. Alianza kuchelewa kurudi nyumbani, mawasiliano yakapungua na hatimaye akaondoka kabisa bila kuaga. Jaribio la kuwasiliana naye lilikuwa gumu kwani mara nyingi hakuwa akipokea simu zake.

“Nilibaki na watoto wawili na maswali mengi kichwani. Nilijaribu kuomba msamaha hata bila kujua kosa langu lakini hakutaka kunisikiliza,” alisema Fatuma. SOMA ZAIDI.
Share To:

Post A Comment: