Na Denis Chambi, Tanga


JUMLA ya walimu 2000 wa shule za Sekondari za kata  katika Mikoa ya Dodoma, Mbeya visiwani Zanzibar   wameunganishwa na huduma ya Smart wasomi  iliyopo chini ya Kampuni ya Airtel Tanzania wenye lengo la  kuwasaidia kupata maudhui ya elimu kwa njia ya mtandao.

Mradi huo ambao umewashirikisha wadau kutoka Shiriki la Umoja wa mataifa  la kumhudumia watoto 'UNICEF' utahusisha shule  3000 za Sekondari na kuwawezesha   kupata maudhui ya kujifunza  bila gharama yeyote  maktaba zilizopo hapa nchini.

Majaribio ya mradi huo ambayo yamefanyika katika shule za Sekondari za kata zilizopo Zanzibar , Dodoma na Mbeya  utawezeaha kuwafikia wanafunzi 5500 .

Aidha Mradi huo wa Smartwasomi umefanya upembuzi yakinifu  juu ya Hali ya mtandao  wa Internet yenye kasi ya 4G ambapo takribani  shule 4,200 zilizopo Tanzania bara na 500 za Zanzibar zitapata  huduma ya maktaba mtandao bure bila ya kulipiza gharama yeyote hatua ambayo itakwenda kuongeza kasi ya ufundishaji kwa walimu pamoja na kukuza  uelewa kwa wanafunzi.

Mkurugenzi mtendaji wa Kampuni ya Airtel Tanzania Dinesh Balinh ameeleza kuwa  "Dhamira yetu kupitia mradi huo wa Smartwasomi  ni kuweka shule 3000 kidigitali  kwa muda wa miaka mitano ambapo kwa mwaka huu wa 2024  tutaanza na  shule 1000kisha Kila shule ya Sekondari iliyounganishwa  itakuwa ukipata GB 1200 kwa mwaka ili kuwawezesha walimu na wanafunzi kwenye kujisomea kwenye maktaba kimtandao"

Akizindua mradi huo katika  kilele cha maonyesho ya wiki ya elimu, ujuzi na ubunifu yaliyofanyika kitaifa mkoani Tanga Mei 31 ,2023 Waziri  Mkuu wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kassim Majaliwa amebainisha kuwa uwiano uliopota mashuleni  kwa wanafunzi na vitabu katika shule mbalimbali zilizopo hapa nchini  haukudhi mahitaji kulingana na viwango vilivyowekwa na Serikali.

Aidha Waziri Majaliwa ameipongeza  Airtel kwa kushirikiana na  Shirika la Umoja wa mataifa 'UNICEF' kupitia mpango huo ambapo  itasaidia juhudi za  Serikali katika kuongeza upatikanaji wa elimu kiendana na maendeleo ya Teknolojia yaliyopo kwa sasa,

"Serikali tunaipongeza Kampuni ya Airtel kwa kushirikiana na UNICEF katika mpango huu kwani utaleta matokeo chanya ya kidumi  katika nyanja ya elimu, ushirikiano huu hauongezei tu ubora wa elimu  bali pia unahakikish watoto wetu Wana zana zinazohitajika ili kuwawezesha kufaulu katika enzi hizi za maendeleo ya kidigitali" amesema Waziri Majaliwa.

Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia  Prof. Adolf Mkenda  ameishukuru na kuipongeza Kampuni ya Airtel Tanzania kwa kuiunga mkono Serikali kupitia mradi huo ambao unakwenda  kuboresha hali ya ufaulu masomo ya kidigital watakayoyapata kwenye maktaba mbalimbali sambamba  na kuongeza motisha ya ufundishaji kwa walimu.

"Mpango huu utaweka kiwango kipya katika ubora wa elimu na kuwawezesha vijana wetu kustawi katika ulimwengu wa kidigitali , tunawapongeza kwa kuingia mkono jitihada hii  tunatazamiakushuhudia matokeo chanya katika sekta ya elimu hapa nchini"
Share To:

JOEL MADUKA

Post A Comment: