Naibu  waziri  wa  habari,mawasiliano  na  teknolojia  ya  habari Mhandisi  MaryPrisca Mahundi amewataka  wanawake wenye  malengo  ya  kujiendeleza  kiuchumi   kutokuwa  wabinafsi  katika  kupeana  ujuzi  na maarifa  ya mafanikio  waliopata na kutembea pamoja bila kuwekeana chuki  na husuda kwa mafanikio ya mtu  mwingine .

Mhandisi Mahundi  amezungumza  hayo  jijini mbeya  wakati  akizungumza  na umoja wa  wanawake wenye malengo  katika  mkutano  mkuu wa kundi  hilo  ambalo  sasa  lina mtaji  na dhamana ya zaidi  ya milioni mia  sita  walizojiwekea

Naibu waziri  wa  habari,mawasiliano  na  teknolojia  ya  habari  Mhandisi Marry Prisca akifungua  mkutano huo wenye lengo la kufahamiana na  wadau ametoa  rai  kwa  wanawake  kuendelea  kupendana bila  kuwa  na  choyo  ya  ujuzi  na uwezo  walionao  katika  kuhakikisha  kila moja  anakuwa  kibiashara.

Beno  malisa   ni  mkuu wa  wilaya  ya  Mbeya   akitoa  salamu  mbele  ya uimoja  huo amewataka  wanawake  kuungana  mkono  katika  nafasi  za uongozi  na kusaidiana  kibiashara pasipo  kuingia  katika  mikopo umiza.

Mwenyekiti wa  umoja  wa  wanawake  waliojiwekea malengo (women with Taget)Doris  Luvanda  pamoja  na mhasisi  wa kundi  hilo Nasra   Haonga wakazungumzia  malengo  yao.








Share To:

Post A Comment: