Denis Chambi ,  Tanga.

JESHI la Polisi Mkoa wa Tanga  limefanikiwa kuwakamata watu tisa wakidaiwa kuwa ni waganga wa kienyeji  ambao walikuwa wanajihusisha na ramli chonganishi katika kijiji cha Kivindani kata ya Tongoni Tarafa ya Pongwe wilaya ya Tanga ambapo walikiwa wakifanya ukaguzi katika nyumba zilizokuwa zikisadikiwa kuwa na  uchawi.


Akitoa taarifa kwa vyombo vya habari leo November 28 ,  2023 kamanda wa jeshi la Polisi mkoa wa Tanga Almachius Mchunguzi amesema  kuwa  wananchi wa kijiji cha Kivindani,  kata ya Tongoni  Tarafa ya Pongwe wilaya ya Tanga  waliwaita waganga hao kwaajili ya kufanya ukaguzi katika nyumba ambazo zilisadikiwa kuwa na  uchawi ambao  wanakijiji wamekuwa wakilalamika kuwa  wakitendewa vitendo vya udhalilishaji kuvuliwa nguo usiku na  kuachwa wakiwa watupu.

"Tumefanikiwa kumkamata Hamisi Kombo(46) mkazi wa Kwediboma wilaya ya Kilindi akiwa na wenzake 8  wote ni waganga wa kienyeji ambao wanajihusiaha na ramli Chonganishi wakiwa katika kijiji cha Kivindani kata ya Tongoni Tarafa ya Pongwe  wilaya ya Tanga ambao wananchi wa enwo hilo waliwaita waganga  hao kwaajili kufanya ukaguzi katika nyumba za kijiji hicho ambazo zinasadikiwa kuwa na uchawi  ambao wanakijiji hao walilalamika kuwa wakitendewa vitendo vya uzalilishaji kwa kuvuliwa nguo na kuachwa wakiwa watupu kimazingira wakati wakiwa wamelala  usiku ,  watuhumiwa hao wote wapo nje kwaajili ya dhamana wakati upelelezi wa shauti lao ukiendelea" alisema kamada Almachius.

Aidha katika taarifa nyingine  kamanda Mchunguzi amesema kuwa wamefanikiwa kuwakamta  watuhumiwa 107  kwa makosa mbalimbali ikiwemo mauaji , wizi wa mifugo  unyang'anyi wa kitumia Silaha ,  kuingia nchini bila kibali  pamoja na kupatikana na dawa za kulevya.

"Kati ya watuhumiwa hao  watuhumiwa 21 wamekamatwa na Bhangi kilogram 43,  Mirungi 124.3 na Heroin 242,  watuhumiwa  wanne   wamekamatwa kwa kosa la kusafirisha raia 7 wa Ethiopia  kuingia nchini bila kibali mtuhumiwa mmoja unyang'anyi wa  kutumia silaha  aina ya Panga  na watuhumiwa wengine 74 wamekamatwa na upelelezi  unaendelea" alisema Kamanda  Mchunguzi.

Alisema  watu wa tatu wamehukumiwa  kunyongwa hadi kufa  kwa kosa la mauaji ya mtoto wa kike  mwenye umri wa miaka 9 huku  watu nane katika maeneo mbalimbali mkoani hapa  wakifariki dunia kutokana na mvua kubwa  inayoendelwa kunyesha.

" Kulitokea tukio la  mauaji ambapo watuhumiwa ni  Rashidi Mwalimu (32)  , Siwajui Kigaa (27) na Zuberi Hassan  wote wakazi wa  kijiji cha Kwandungwa  wilaya ya Handeni  ambao walihukumiwa  kunyongwa hafi kufa  kwa kosa la mauaji ya mtoto wa kike  mwenye umri wa miaka tisa" alisema

Aidha  jumla ya watuhumiwa 41  wamefikishwa mahakamani wakati kesi27 zikitolewa  hukumu mbalimbali  huku 11 zikiwa zinaendelea ambapo  watumiwa watatu ambao ni  Justine Kunael (41) ,  Said Adam (32) na  Maliki (38) wakazi wa  Handeni wakihukumiwa  kifungo cha maisha  jela kwa kosa la kubaka.


Share To:

Post A Comment: