Wafanyakazi wa Bohari ya Dawa (MSD) wakiendelea na zoezi la kuhesabu malikatika maghara yao. 

Na Dotto Mwaibale,  

BOHARI ya Dawa (MSD) imeanza rasmi zoezi la kuhesabu mali kwa mujibu wa sheria. Zoezi hilo la kuhesabu mali  linategemewa kukamilika  mwishoni  mwa mwezi Juni 2023 ili kuanza mwaka mpya wa fedha. 

Katika kipindi hiki maghala yote ya MSD Makao Makuu pamoja na Kanda zote  yatakuwa yamefungwa kupisha zoezi hilo. 

Awali kabla ya kuanza kwa zoezi hilo Bohari ya Dawa (MSD) iliwaarifu wateja wake wote wa Hospitali, Vituo vya Afya na Zahanati kuwa  kuanzia Juni 15, 2023 mpaka Juni 30, 2023 litafanyika zoezi la kuhesabu mali kwa mujibu wa sheria na kuwa kutokana na zoezi hilo la kuhesabu mali, maghala yote ya MSD yatafungwa kwa kipindi cha wiki mbili kuanzia Juni, 15, 2023.

Maombi yote ya dawa, vifaa tiba na vitendanishi vya maabara yawasilishwe MSD kabla ya Juni 7, 2023, ili kukidhi mahitaji wakati wote maghala hayo yatakapokuwa yamefungwa na kuwa  huduma ya dharura ya kupata mahitaji itatolewa, pale tu itakapothibitika uhitaji.

Zoezi la kuhesabu mali likiendelea.
Mali za MSD zikihesabiwa.
Umakini ukifanyika wakati wa kuhesabu mali hizo
 

Share To:

dotto mwaibale

Post A Comment: