Mapema Leo, Tarehe 25.1.2023 Mbunge wa Jimbo la Msalala Mhe.Iddi Kassim Iddi  amekabidhi  Pikipiki kumi na Tatu (13)  Kwa Kikundi Cha Vijana Boda Boda Segese kutoka Kata  Segese.


Atua hiyo ya Mbunge inatokana na  maombi kutoka kwa vijana hao,suala ambalo lilimlazimu Mbunge Iddi  kuomba Halmashauri ya ya Msalala ikubali kutenga fedha kiasi Cha Tsh. 38,090,000 (milioni thelathini na nane  na Elfu tisini) Kwa ajili ya kununua pikipiki 13 ambazo zitachochea shughuli zao za uzalishaji na kusaidia  kufanyika Kwa ufanisi zaidi ili vijana hao waweze kujiinua kiuchumi.


Aidha, Mhe.Iddi Kassim Iddi amesisitiza vijana kuchangamkia fursa za mikopo inayotolewa Halmashauri Ili waweze Kujenga uchumi imara Kwani vijana ndio Nguvu Kazi ya Taifa. 

"Tunatambua vijana ndio nguzo ya Taifa niwaombe vijana wenzangu undeni vikundi mje mchukue mikopo kama kuna changamoto inayokwamisha niambieni mimi Mbunge wenu nitawasaidia"Iddi Kassim Iddi Mbunge Jimbo la Msalala.


Aidha, amepongeza na Kutoa wito Kwa  Mkurugenzi wa Halmashauri ya Msalala Ndg. Charles E.Fussi  kuendelea Kutoa Pikipiki kwa vikundi vyote vya  Bodaboda vya Msalala.


Pia  Mbunge Iddi  ameongeza adhima yake kubwa ni kuona vijana wanaimarika kiuchumu ndani ya Jimbo la Msalala .




Share To:

mwangaza wa hbari

Post A Comment: