Wafanyakazi wa Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI)  wa Kituo cha Maruku mkoani Kagera wakiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi wa Utafiti na Ubunifu wa TARI Dkt Joseph Ndunguru (wa nne kutoka kushoto) baada ya kikao kilichofanyika leo katika ziara yake ya kikazi ya vituo vya ukanda wa ziwa. 

Na Junior Mwemezi, TARI

TAASISI ya Utafiti wa Kilimo   Tanzania -TARI imesema itaendelea na utaratibu wa kuwajengea uwezo watumishi wake wa idara tofauti juu uandikaji wa maandiko ya miradi  itakayoweza kuongeza ufanisi katika maswala ya kiutafiti.

Kauli hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa Utafiti na Ubunifu wa TARI Dkt Joseph Ndunguru katika kikao chake na watumishi wa kituo cha Utafiti wa Kilimo cha Maruku mkoani Kagera  ikiwa ni mwendelezo wa ziara yake ya kikazi katika vituo vya ukanda wa ziwa.

Dkt Ndunguru amesema wafadhili wengi wamekuwa wakishindwa kutoa pesa katika miradi mbali mbali kutokana na waandaaji wa maandiko ya miradi hiyo kutoainisha mambo muhimu ,ambayo yanaweza kuwashawishi wafadili .

Aidha Dkt Ndunguru amewaeleza wafanyakazi wa TARI Maruku  kuwa njia pekee ya kufikia mafanikio ni kuepukabhana makundi,ubinafsi na kujenga umoja na kutambua wote wanajenga nyumba moja ambayo ni Tanzania.

Mkurugenzi wa Utafiti na Ubunifu wa TARI Dkt Joseph Ndunguru akizungumza na watumishi wa TARI wa kituo cha Utafiti wa Kilimo cha Maruku mkoani Kagera.

Watumishi wa TARI Kituo cha Maruku Kagera wakiwa kwenye kikao hicho.
Kikao kikiendelea.
Kikao kikiendelea.
Watumishi wa TARI  Kiruo cha Maruku wakiwa kwenye kikao hicho.

Kikao kikiendelea.


Kikao kikiendelea.
 

Share To:

dotto mwaibale

Post A Comment: