![]() |
Na John Mapepele
Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo. Mhe, Mohamed Mchengerwa amesema Serikali itaendelea kuwekeza kwenye timu zinazofanya vizuri huku akiwataka Watendaji wa michezo kufanya tathmini kwa zisizofanya vizuri ili Serikali ichukue maamuzi magumu.
Mhe. Mchengerwa ameyasema haya usiku wa leo hafla ya utoaji wa tuzo kwa washindi wa mashindano ya Afrika ya Gofu ya Wanawake -All Africa Competition Trophy (AACT) yaliyofanyika kuanzia Septemba, 6-8, 2022 kwenye viwanja vya Gymkhana jijini Dar es Salaam na kushirisha nchi 20.
Katika mashindano hayo Tanzania imeshika nafasi ya tatu wakati Morocco imeshika nafasi ya pili na nchi ya Afrika Kusini kuwa mshindi wa kwanza.
Ameipongeza timu ya Tanzania kwa kushika nafasi ya tatu huku akifafanua kuwa hayo ni matunda ya uwekezaji mkubwa wa Rais Samia Suluhu Hassan kwenye michezo katika kipindi kifupi cha uongozi wake.
Aidha, ameipongeza timu ya taifa ya soka ya wanawake ya Twiga Stars kwa kuingia nusu fainali katika mashindano ya COSAFA.
Ametoa rai kwa timu nyingine kufanya vizuri ili kuendelea kuitangaza Tanzania Kimataifa ambapo pia ametoa wito kwa wadau wengine nchini kuendelea kudhamini ili kukuza vipaji vya michezo.
Hafla hiyo ilihudhuriwa na wageni mbalimbali na wadau wa michezo ikiwa ni pamoja na Balozi wa Morocco nchini Zakaria El Goumiri na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo, S
Post A Comment: