Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akivuta pazia kuashiria uwekaji wa jiwe la msingi la ujenzi wa Ofisi ya Utawala ya Halmashauri ya Wilaya ya Singida katika hafla iliyofanyika jana. Kutoka kushoto ni Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Singida, Martha Gwau na Mbunge wa Jimbo la Singida Kaskazini, Ramadhani Ighondo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Singida, Ester Chaula (kulia) akitoa taarifa ya ujenzi wa ofisi hiyo kwa Waziri Mkuu Kassim Majaliwa.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akifafanuliwa jambo na Mganga Mfawidhi Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Singida, Dk. Deogratias Banuba (kulia) wakati alipokagua ujenzi wa Hospitali hiyo ya Rufaa, akiwa kwenye ziara ya siku mbili mkoani Singida. 

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na wananchi baada ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa jengo la Utawala la Halmashauri ya Wilaya ya Singida, ambalo ujenzi wake unategemea kukamilika ifikapo Novemba, 2022, akiwa kwenye ziara ya siku mbili mkoani Singida. 


Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tawala za Mkoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) David Silinde akizungumza kwenye ziara.
Wananchi wa Ilongero wakiwa kwenye hafla ya uzinduzi wa ofisi hiyo.
Wananchi wa Ilongero wakiserebuka wakatiwakimsubiri Waziri Mkuu kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa ofisi hiyo.
Muonekano wa Ofisi ya Utawala ya Halmashauri ya Wilaya ya Singida.
Viongozi wakimsubiri Waziri Mkuu Kassim Majaliwa kuja kuja kuweka jiwe la msingi la ofisi hiyo.

Viongozi wakimsubiri Waziri Mkuu kuja kuweka jiwe la msingi la ofisi hiyo. Kutoka kulia ni Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Singida, Martha Gwau, Mbunge wa Singida Mjini, Mussa Sima, Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Singida, William Nyalandu, Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM (NEC) Taifa Mkoa wa Singida, Yohana Msita na Mbunge wa Singida Kaskazini, Ramadhani Ighondo.
Viongozi mbalimbali wakiwa kwenye hafla hiyo. Kushoto ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Singida, Eliya Digha.
Taswira ya hafla hiyo.
Hafla hiyo ikiendelea.
Mbunge wa Singida Kaskazini, Ramadhani Ighondo akizungumza kwenye hafla hiyo.
Wazee wa Ilongero wakiwa kwenye hafla hiyo.
Watoto wakiwa kwenye hafla hiyo.
Wanafunzi wa Shule ya Msingi Ilongero wakiwa kwenye hafla hiyo.
Mbunge wa Singida Mjini, Mussa Sima akizungumza.
Wakina mama wa CCM wa Ilongero wakiwa kwenye hafla hiyo.
Mbunge wa Viti Maalum  Mkoa wa Singida, Nusrat Hanje akizungumza.
Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Singida, Martha Gwau akichangia jambo kwenye hafla hiyo.

Mwenyekiti wa CCM  Mkoa wa Singida, Alhajj Juma Killimbah akizungumza.

Mbunge wa Singida Mashariki, Miraji Mtaturu, akizungumza wakati wa mkutano wa majumuisho wa ziara hiyoya Waziri Mkuu.


Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akimuhoji Meneja wa Wakala wa Barabara za Mijini na Vijijini (TARURA) Wilaya ya Singida Mhandisi Lambati Bayona (kushoto) kuhusu malalamiko yaliyotolewa na wananchi ambao walikuwa wajengewe daraja au kupatiwa kivuko cha kutoka eneo la Mwahango kwenda Kinyeto.
Wananchi wakimsubiri Waziri Mkuu nje ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Singida ili kumsikiliza baada ya kukagua ujenzi wa wa majengo ya hospitali hiyo
Wananchi wakimsubiri Waziri Mkuu nje ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Singida ili kumsikiliza baada ya kukagua ujenzi wa wa majengo ya hospitali hiyo.
Madiwani wa Manispaa ya Singida wakimsubiri Waziri Mkuu.
Mwandishi wa Habari wa Gazeti la Nipashe na Guardian Mkoa wa Singida, Thobias Mwanakatwe (kushoto) akiwajibika wakati wa ziara hiyo ya Waziri Mkuu. Kulia ni Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Stellah Mutahibirwa.

Wananchi wakimsikiliza Waziri Mkuu nje ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Singida Mandewa.

Sheikh wa Mkoa wa Singida, Issa Nassoro akiomba dua kabla ya kuanza kwa mkutano wa majumuisho wa ziara ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa uliofanyika Ukumbi wa Mikutano wa Taasisi ya Uhasibu (TIA) Kampasi ya Singida.
Mkutano wa ndani ukiendelea.
Wabunge wakiwa kwenye mkutano huo.
Wajumbe wa kamati ya siasa Mkoa wa Singida wakiwa kwenye mkutano huo. Kulia ni Katibu Mwenezi wa CCM Mkoa wa Singida, Ahmed Kaburu.
Mkutano ukiendelea. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Singida, Ester Chaula.
Mkutano ukiendelea.
Mkutano ukiendelea.

Mshereheshaji maarufu Mkoa wa Singida Chrispin Nyaulingo akiongoza mkutano huo.

 


Na Dotto Mwaibale, Singida

 

WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa, amemaliza ziara yakeya kikazi ya siku mbili mkoani Singida ambapo ametoa maagizo mazito kwa Wakuu wa Wilaya ya kuhakikisha wanasimamia watumishi wote wa Halmashauri za Mkoa wa Singida ambao walikusanya fedha za mapato lakini hawakuzipeleka benki kuzirudisha haraka.

Majaliwa alitoa agizo hilo jana katika kikao cha majumuisho ya ziara yake  hiyo wakati akizungumza na watumishi wa Halmashauri za Wilaya ya Singida, Ikungi na Halmashauri ya Manispaa ya Singida.

Alisema kumekuwa na tatizo kubwa kwenye halmashauri nyingi nchini katika ukusanyaji wa mapato ya ndani ambapo baadhi ya watumishi wanapokusanya fedha haziingizi kwenye mfumo  wa serikali jambo ambalo imekuwa kero kubwa.

"Wakuu wa Wilaya hakikisheni watumishi wanaodaiwa fedha wazirudishe haraka, Iramba, Manyoni na hata Ilongero (Halmashauri ya Wilaya ya Singida) nimepewa orodha ya watumishi ambao wanadaiwa fedha za makusanyo," alisema.

Majaliwa alisema Rais Samia Suluhu Hassan amekuwa akisisitiza suala la ukusanyaji wa mapato na hata majuzi wakati anawaapisha wakuu wa mikoa lakini cha kushangaza baadhi ya watumishi wa umma wamegeuka kuwa wabadhirifu.

Alisema ujanja unaofanywa na baadhi ya watumishi kufuja fedha za makusanyo ni kwamba wanapokusanya fedha hasa wanapobaini ni nyingi wanazima mashine ili zisiingie kwenye mfumo wa serikali.

Aidha, Waziri Mkuu amewataka watumishi kuacha urasimu katika utendaji wa kazi kwani mambo hayo ndio yanakaribisha vitendo vya rushwa chini.

Kuhusu idara za manunuzi, alisema limekuwa ni tatizo kubwa ambapo idara hizo zimekuwa zikiweka makadirio makubwa ya bei za manunuzi ya vifaa vya ujenzi kwenye miradi hususani inayotumia 'force account'.

Aliongeza kuwa kwenye halmashauri kumekuwa na tatizo kubwa la usimamizi wa miradi inayotekelezwa na kwamba kuna umuhimu kwa watumishi kuhakikisha suala hili linapewa umuhimu wa juu.

Alisisitiza suala la mahusiano kwa watumishi wa umma mahali pa kazi kwani kufanya hivyo kutaboresha utendaji kazi na kuleta ufanisi mkubwa katika kuwatumikia wananchi.

Aidha, alizitaka halmashauri kuratibu vizuri suala la wafanyabiashara wadogo maarufu wamachinga ili wapewe maeneo ya kufanyia biashara zao bila usumbufu.

Awali Waziri Mkuu aliweka jiwe la msingi la ujenzi wa jengo la Utawala la Halmashauri ya Wilaya ya Singida linalojengwa Ilongero katika Kijiji cha Mwahango kwa thamani ya Sh.2.7 bilioni.

Akizungumza na wananchi wa eneo hilo,alimwagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Singida, Ester Chaula, kuisimamia idara ya manunuzi ili ujenzi wa jengo hilo uweze kukamilika na kuanza kutumika.

"Nimeridhishwa na ujenzi unavyoendelea, DED (Mkurugenzi wa Halmashauri) isimamie idara ya manunuzi, wasikuvuruge, mkandarasi alipwe fedha zake, " alisema.

Akiwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Singida inayojengwa kwa Sh.bilioni 19.5 Waziri Mkuu, alisema ujenzi wa hospitali hiyo itakuwa mkombozi mkubwa kwa wananchi wa mkoa huu na mikoa jirani.

 

Share To:

dotto mwaibale

Post A Comment: