Mkuu wa Wilaya ya Rufiji Mkoani Pwani Meja Edward Gowele  amesema hayo alipokuwa akitembelea  maonyesho ya nanenane kanda ya mashariki yaliyofanyika mkoani morogoro ambapo amesema  sekta za kilimo, ufugaji na uvuvi vinatakiwa kufuata ushauri wa wataalamu vita weza kupunguza  migogoro katika ya wakulima na wafugaji. 

Meja Gowele amesema kuwa kupitia maonyesho ya nanenane wataweza kujifunza  Teknolojia  mpya zinavyo badilishwa kutoka kwenye kilimo cha mkono na kwenda kwenye kilimo cha kisasa ambacho ndio kilimo chenye tija na kumnufaisha mkulima . 

Pia amesema kuwa katika maonyesho hayo wameona namna wafugaji wanavyofuga mifugo kwa njia ya kisasa na kwanjia nzuri za kunenepesha  wanyama kwa kutumia malisho bora kwa kupanda majiani  ambayo yatasaidia kuepusha migogoro katika ya wakulima na wafugaji iliyopo sasa katik maeneo mengi.

Aidha Mkuu wa Wilaya Meja Edward Gowele amesema kama elimu hii ya kilimo ,ufugaji na uvuvi itafika vizuri Kwa watanzania kutakuwa na mabadiliko makubwa kwani sekta hizo  muhimu  ambapo zitakuwa na tija  kwa wakulima wavuvi na wafugaji wataweza kufanya shughuli zao kibiashara  na kuweza kupata   mafanikio yao na taifa litaweza kunufaika.

Share To:

Post A Comment: