Na Mwandishi Wetu
Abuja, Nigeria
Ubalozi
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Nigeria na Uwakilishi wa nchi
nyingine 14 za Afrika Magharibi, ulifanya maadhimisho ya siku ya
Kiswahili Duniani nchini hapa.
Maadhimisho
hayo yaliyofanyika sambamba na maonesho ya Filamu ya Tanzania the Royal
Tour, ni kutokana na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sayansi na
Utamaduni, (United Nations Education, Scientific and Cultural
Organization -UNESCO), Novemba 23, 2021 wakati wa Mkutano wa 41 wa nchi
Wanachama walipitisha Julai 7, kila mwaka kuwa siku ya Kiswahili
Duniani.
Uamuzi huo ulifikiwa kutokana na Kiswahili kuwa miongoni mwa lugha 10 zinazozungumzwa zaidi ulimwenguni.
Maadhimisho
hayo yaliyofanyika Jijini Abuja, yalihudhulia na Jumuiya ya
Wanadiplomasia (kutoka Balozi za Afrika Kusini, Rwanda, Uganda, Burundi,
Kenya, Kongo-DRC, Bulgaria, Palestine, Burkina Faso, Cuba, Mali,
Guinea, Poland, Senegal), ambapo Mwakilishi wa UNESCO nchini Nigeria,
Asasi za kiraia (kama vile women in Business and Tourism, Women Arise,
wafanyabiashara, maofisa kutoka taasisi za Serikali ya Nigeria kama vile
Voice of Nigeria, Nigerian Export Promotion Council, taasisi za elimu
(kama vile Chuo Kikuu cha Ghana, Legon, Chuo Kikuu cha Port Harcourt,
Chuo Kikuu cha Ibadan, Taasisi ya SOS ya Ghana): Diaspora Afrika
Mashariki na vyombo vya habari (kama vile Voice of Nigeria, Nigeria
Television Authority, na wadau wengine wa karibu wa Ubalozi.
Katika maadhimisho hayo mgeni rasmi alikuwa Balozi wa Botswana nchini Nigeria, Pule Mphothwe.
Pamoja
na mambo mengine, maadhimisho yamliambatana na mdahalo wa wazi kuhusu
ambao ulijadili kuhusu mchango wa Kiswahili katika ukombozi wa Bara la
Afrika; Umuhimu wa Lugha katika ujenzi wa taifa; nafasi ya kimkakati ya
Lugha ya Kiswahili katika kufikia malengo ya Eneo Huru la Biashara
Barani Africa, AfCFTA; changamoto na uzoefu wa kufundisha Lugha ya
Kiswahili katika taasisi za elimu Afrika Magharibi na changamoto
zinazovikabili vyombo ya habari katika kutangaza idhaa za Kiswahili
Afika Magharabi.
Wakati
wa maadhimisho hayo, Ubalozi wa Tanzania nchini Nigeria, uliwapatia
vyeti vya kushiriki mafunzo ya awali wafanyakazi 10 wa Nigerian Export
Promotion Council, NEPC.
Wanafunzi hao waliweza kushiriki mafunzo hayo kikamilifu, mbali na changamoto na wingi wa majukumu mengine ya kikazi.
Mafunzo
hayo yaliyodumu kwa takribani miezi sita, yaliendeshwa na Ubalozi kwa
Kushirkiana na NEPC kuanzia Novemba 2021, ambapo darasa hilo
linakusudia kuendelea na mafunzo ngazi ya juu.
Sambamba
na maadhimisho hayo, ubalozi ulitumia fursa hiyo kuwaonesha washiriki
Filamu ya Tanzania the Royal Tour, ikiwa ni moja ya mikakati wa
kutangaza vivutio vya Utalii vya Tanzania Bara na Zanzibar.
Post A Comment: