Raisa said,Korogwe


MBUNGE wa Korogwe Vijijini Mkoani Tanga Timotheo Mzava amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Samia  Suluhu Hasan  Kwa kuwapatia shilingi bilion 3.8 Kwa  akili ya Ujenzi wa daraja llinalounganisha kata mbili za Halmashauri ya Wilaya

ya Korogwe.


Ujenzi wa daraja hilo unatimiza ahadi yake  ambayo aliyoitoa siku mbili kabla ya kuteuliwa kuwa Rais.


Akielezea kuhusu daraja hilo wakati wa ziara yake katika eneo hilo linapojengwa daraja hilo,

 amesema kuwa

 daraja hilo ni ukombozi.


Amesema kuwa mradi huo utachukua miezi  18 kukamilika na akamtaka

mkadarasi huyo aliyemtambulisha kwa jina la Nyanzi kuhakikisha mradi

huo unakwisha kwa wakati na ikiwezekana hata kabla ya miezi hiyo

iliyopangwa.


Mnzava alimsifia Rais Samia kwa kusikiliza kilio cha wananchi wa eneo

hilo ambao walikuwa wanapata tabu a kuvuka na kuhatarisha maisha yao

kutokana na mto uo kuwa na mamba wengi wakilazimika kuvuka kwa kutumia

boti.


Amesema akiwa pale alimwomba Mama Samia wakati huo akiwa Makamu wa

Raisi ambaye aliagiza kiwekwe kivuko cha muda kuwasidia wananchi

kuvuka katika eneo hilo.


Amesema kuwa ujenzi wa daraja hilo ni pamoja ujenzi wa barabara kuweka

changarawe kutoka eneo la Kwasunga hadi katika daraja hilo.


Mkazi wa Majengo, Mswaha, Zuberi Mbwana amesema wamepoteza watu

wanofikia wanne kwa kuliwa na mamba. “Hata mimi nimeshadondoka na

pikipiki hapa.kuna pikipiki  kama mbili zipo ndani ya hapo hivyo

ujenzi wa daraja hili ni nafuui kubwa kwetu,” alisema Mbwana.


Mkazi mwingine wa Mswaha Darajani, Miraji Athumani Msanga amesema kuwa

wananchi walikuwa wanapata tatizo na hata wanawake walikuwa

wanajifungulia hapo kutokana na changamoto ya daraja.


 “hapa ni kama makao makuu ya mamba. Watu walikuwa wanaliwa na mamba hapa.  Ukivuka tu ni kama wanakutamani wanakuja. 

Watu walikuwa wanatozwa Sh 1,000 kuvushwa hapo katika kivuko lakini tangu ujenzi uanze naona hali inaanza kupungua,” alisema.

Naye Msimamizi wa mradi huo Joel Mkinga alisema walichelewa kuanza ujenzi kutokana mchakato wa kupata vibari .

“Tu memaliza kukusanya vifaa na ujenzi utakamilika Septemba, mwakakesho,” amesema.

Share To:

Post A Comment: