Mkuu wa Wilaya ya Ikungi, Jerry Muro.


NIMEONA niandike machache kwa leo yanayowahusu watumishi wa umma ambao ni walimu, watu wa sekta ya afya na kada mbalimbali katika utumishi wa umma.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan alitangaza kupunguza Kodi ya mishahara (PAYE) kwa 1% kwa watumishi wa umma, akaenda mbali akafuta tozo ya 6% kwa Watumishi wa umma wenye Mikopo ya Elimu ya Juu na kuondoa adhabu ya 10% kwa kuchelewa kulipa Mkopo huo.

Katika kuimarisha utawala bora na kutoa huduma bora kwa wananchi Rais Samia amewapandisha Vyeo na madaraja Watumishi 198,215 hili sio jambo dogo ni jambo linalohitaji ujasiri na haswa ukizingatia kuwa kila anaepandishwa daraja ana stahiki zake katika daraja husika.

Katika kipindi cha mwaka mmoja Rais Samia ameridhia kuajiriwa zaidi ya watumishi wapya 40,000 katika kada mbalimbali zikiwemo afya na elimu.

Katika eneo la utumishi wa umma, Mhe Rais Samia ameridhia pia kulipa malimbikizo ya mishahara kwa Wafanyakazi 75,000 ambayo ni zaidi ya  Bilioni 124.3 fedha ambazo sasa zimeingia katika mzunguko wa maisha ya watumishi hatua inayoongeza mzunguko wa fedha mitaani.

Share To:

dottomwaibale

Post A Comment: