Aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai Lengai Ole Sabaya ambaye juzi ijumaa alihukumiwa miaka 30 gerezani, kesho Jumatatu tarehe 18 Oktoba 2021, atarejea tena Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha kuendelea kusikiliza kesi nyingine inayomkabili ya Uhujumu Uchumi.

Sabaya mwenye miaka 34 na wenzake sita, wanakabiliwa na kesi hiyo ya uhujumu uchumi katika Mahakama hiyo ambayo Ijumaa iliyopita ya tarehe 15 Oktoba 2021, ilimhukumu kifungo hicho jela yeye pamoja na wenzake watatu.


Wakati akiendelea kutumikia adhabu hiyo, kesho Jumatatu, atarejea tena mahakama hapo kuanza kusikilizwa mfululizo kwa kesi nyingine ya uhujumu uchumi inayosikilizwa na Hakimu Mkazi Patricia Kisinda.

Kesi hiyo ya uhujumu uchumi inamashtaka mbalimbali ikiwemo kuongoza genge la uhalifu pamoja na utakatishaji fedha inayomkabili Sabaya na wenzake sita ambao ni, John Aweyo, Watson Mwahomange, Enock Mnkeni, Sylvester Nyegu, Nathan Msuya na Jackson Macha.

Katika kesi hiyo, washtakiwa wote wanatuhumiwa kujipatia Sh.90 milioni kutoka kwa
mfanyabiashara Fransis Mrosso kinyume na sheria.

Share To:

Teddy Kilanga

Post A Comment: