MKUU wa mkoa wa Arusha, John Mongella, amezitaka halmashauri zote za wilayani katika Mkoa huo kuhakikisha zinakuwa na Waratibu wa Tasaf,waadilifu ambao watahakikisha wananchi wenye hali duniza maishaI wanaboresha maisha yao vinginevyo hatasita kuwaondoa kwenye nafasi hizo kwa kuwa watakuwa wanakwamisha lengo zima la kuwezesha wananchi kupata maisha.

Rc Mongela,ameyasema hayo leo alipokuwa akifungua mafunzo ya awamu ya pili sehemu ya tatu ya mpango wa TASAF,yanayowashirikisha mdiiwani,wabunge ,Waratibu wa Tasaf jiji,pamoja na. watendaji wa halmashauri  ya Jiji la Arusha,yanayofanyika ukumbi wa Katibu tawala wa mkoa.

Rc Mongella,amesema mkoa utasimamia Tasaf,ili iweze kutekeleza  lengo lake la.kuwawezesha  wananchi wenye hali duni ya maisha na kiuchumi ili waweze kuboresha maisha yao hivyo lazima wawepo waratibu wenye sifa ,ubunifu na uwezo wa kufanya kazi zitakazosaidia kaya masikini kuinuka kiuchumi.

Amesema Tasaf inafanya kazi kubwa ya kuboresha maisha ya wananchi wenye hali duni ili nao wawe na maisha bora, kupitia Tasaf wapo wananchi walookuwa na hali duni tangia ianzishwe miaka 7,leo wanaboresha maisha ambapi wameweza kuanzisha shughuli za kiuchumi na sasa wana maisha  mazuri

Ameonya mapungufu yaliyojitokeza kwenye utekelezaji wa Tasaf awamu ya kwanza na. ya Pili ya Kiungiza kaya ziisizokuwa na. sifa yasijirudie na akawataka madiwani wahakikishe wanasimamia zoezi hilo la utambuzi wa kaya duni kuhakikisha kaya zitakazoingjzwa kwenye mpango huo wawe ni walengwa ambao ndio wenye uhifaji na si vinginevyo.

Akitoa nasaha zake mkuu wa wilaya ya Arusha Sophia Mjema,amesema mafunzo hayo yanawajengea uelewa madiwani na Waratibu ili waweze kushiriki kaikamilifu katika utekelezaji na usimamizi wa mpango huo wa Tasaf,ili kuepuka Wasio na.sifa wasiingizwe kwenye mpango huo Bali  wananchi wenye hali duni 
ndiio waweze kuingizwa kwenye mpango huo hatimae waboresha maisha yao.

Amewaambia madiwani hao kuhakikisha kuwa wanazitambua kaya zote zenye hali duni ili kuwezesha wahitaji kupata ruzuku ya fedha inayotolewa na Tasaf, waweze kunufaika kwa kuwa wanazifahamu kaya duni zenye uhitaji ziweze kunufaika n.a. hatimae ziboreshe maisha.

 Amesema yeye atashiriki zoezi hilo ili kuondoa udanganyifu wa kwa kuingiza wasiokuwa na sifa,na hataki wilaya yake kuwepo na wahitaji hewa bali kuwepo na idadi halisi ya wahitaji halisi na akaonya kwamba yeyote akaefanya udanganyifu  kwa kuweka kaya hewa huyo atadhughulikuwa kwa majibu wa sheria.

Mbunge wa jambo la Arusha, Mrisho Gambo,amesema wapo wasiokuw na. sifa wanafanya kazi Tasaf na. matokeo yake ni kukosekana kwa,ufanisi

Ameitaka Tasaf kuwakumbuka wazee kwa kutambua kuwa wazee wameifanyia mambo mengi nchi hii lakini wamekuwa wakisahaulika kwenye miradi mbalimbali ya kuboresha maisha wakati changamoyo ya umasikini haina umri.

Tasaf,umekuwa ni msaada mkubwa kwa wananchi hivyo akamuomba mkuu wa mkoa kuweka jicho la zida kwenye miradi na ushauri serikali iipitie na. kuratibu ipasavyo ili kuonfoa udanganyifu unaweza kujitokeza na kuingizwa kaya hewa.

Kwa upande wake Mstahiki meya wa Jiji la Arusha, Maxilian Illanghe,amesema katika salamu zake kwamba madiwani wanasimamia  Programu hiyo ya Tasaf,ipasavyo,kwa kuhakikusha vigezo vilivyo wekwa vya walengwa kuingizwa kwenye programu hiyo ni wale wenye uhitaji na hakuna endeleo.

Amesema mafunzo hayo yatawawesha madiwani kusimamia ukusanyaji mapato ambayo yatasaidia wajasriamali katika kipindi cho na hivyo kupunguza maskini katika jamii.

Awali mwakilushi wa mkurugenzi miuu wa Tasaf, Janeth Madulu, alisema kuwa mara baada ya mafunzo hayo wataenda mitaani kwa ajilivya utekelezaji wa zoezi hilo la kutambua kaya duni ili ziingixwe kwenye mpango huo.

Ameongeza kwamba asilimia 12% ya Kaya umaskini umepungua  ambapo kupitia Tasaf,walengwa wameweza kufanya shughuli za ujasiria mali


Share To:

Post A Comment: