Na John Walter-Babati
Halmashauri ya wilaya ya Babati  mkoa wa Manyara, imeomba kupatiwa msaasa wa  gari la wagonjwa ili kuweza kukabiliana na changamoto inayowakabili ya kusafirisha wagonjwa.
Ombi hilo limetolewa na Mganga mkuu wa Halmashauri ya wilaya ya Babati  Dr.Hosea Madama  akitoa taarifa ya idara ya afya kwa Naibu waziri wa TAMISEMI Josephat Kandege wakati wa uzinduzi wa Zahanati ya Kijiji cha Gajal kata ya Ayalagaya.
Dr. Madama amesema kuwa wapo katika njia kuu na ajali nyingi hutokea hivyo serikali na wadau mbalimbali wajitokeze kusaidia kupatikana kwa  magari hayo kwa vituo vya afya saba vilivyopo ndani ya Halmashauri ya wilaya ya Babati.
Aidha Dr.Madama ameomba serikali  kutoa fedha za kujenga miundo mbinu inayohitajika katika zahanati mbili za Dareda Kati na Bashnet zilizopo katika tarafa ya Bashnet ili kusaidia kutoa huduma za dharura na upasuaji kwa wananchi.
Amesema licha ya Halmashauri hiyo kuwa na hospitali mbili,  Zahanati 40 nyingi zikiwa ni za serikali pamoja na vituo vya afya saba, lakini wanakabiliwa na changamoto mbalimbali za upungufu wa nyumba za watumishi pamoja na watumishi wa kada hiyo.
Ameeleza kuwa Idara ya watumishi wa afya ina jumla ya watumishi 324 ambapo  wanaohitajika ni 747 sawa na asilimia 43, huku nyumba za watumishi zikiwa 14 wakati hitaji ni nyumba 84  sawa na asilimia 16 ya hitaji.

Kuboreshwa kwa huduma za afya katika Halmashauri ya wilaya ya Babati,  itawasaidia wananchi wa wilaya hiyo wanaokadiriwa kuwa zaidi ya laki tatu (300,000)  ikiwa na Tarafa nne (4) , kata 25, na vijiji mia moja na mbili (102)
Mbunge wa Jimbo la Babati Vijijini Mheshimiwa Jituson Vrajilal ameiomba serikali pindi inaposambaza vifaa katika vituo mbalimbali, ikumbuke kituo cha Dareda kati.
Mkuu wa wilaya ya Babati Elizabeth Kitundu  amesema wamepokea fedha za kutosha katika kusaidia miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwepo za ujenzi wa hospitali ya wilaya ya Babati vijijini ambayo haikuwepo.
Naye  Naibu waziri ofisi ya Rais tawala za mikoa na serikali za mitaa (TAMISEMI) Josephat Kandege  akizindua zahanati hiyo iliyogaharimu jumla ya shilingi Milioni 245,595,000, amewapongeza wananchi wa kijiiji cha Gajal na uongozi wa kijiji  hicho kwa kujitolea na kuanzisha ujenzi wa jengo la Zahanati  hiyo.
Share To:

Post A Comment: