Chama Cha Mapinduzi wilayani Nyamagana Cha tembea kifua mbele kwa utekelezaji wa miradi 260 katika kipindi Cha miaka mitano kuanzia Mwaka 2015 Hadi Mwaka 2020 katika uongozi wa serikali ya awamu ya tano ukiongozwa na Jemedari Dkt. John Pombe Magufuli kwa kushirikiana na Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo la Nyamagana.

Hayo yamebainika katika ziara ya siku nne ya Kamati ya siasa ya Chama Cha Mapinduzi wilaya ya Nyamagana ikiongozwa na Mwenyekiti wake Comrade Zebedayo Athuman Wakati wa kukagua miradi 260 ya Maendeleo inayotekelezwa chini ya halmashauri ya Jiji la Mwanza. Ziara hiyo inahusisha ukaguzi wa miradi inayotekelezwa kupitia fedha za Serikali Kuu,  Mapato ya Ndani ya Halmashauri ya Jiji la Mwanza, Miradi chini ya Mfuko wa Jimbo pamoja na Miradi kupitia hisani ya Wadau wa Maendeleo katika sekta za elimu, Afya, Miundombinu, Biashara na Uchumi, Maji, Nishati pamoja na Jamii.

Ziara ya siku nne imeanza mnamo Tarehe 03.06.2020 inatarajia kuisha tarehe 07.06.2020. Katika ziara hii Mhe. Zebedayo ameambatana na Kamati ya ulinzi na usalama Wilaya ya Nyamagana chini ya Mwenyekiti wake DC Dkt. Philis Nyimbi, Ofisi ya Mbunge Jimbo la Nyamagana, Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Jiji la Mwanza likiongozwa na Mstahiki Mayor James Bwire pamoja na Mkurugenzi wa Halmashauri Kiamoni Kibamba akiwa na watendaji.

Imetolewa na
Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Nyamagana🇹🇿
Share To:

msumbanews

Post A Comment: