Wananchi wa Kijiji cha Mdughuyu Kata ya Kaugeri wilayani Ikungi mkoani Singida wakisukuma gari la Mbunge wao Elibariki Kingu wakati alipokuwa amewasili kijijini hapo jana kufanya mkutano wa hadhara.
Mbunge wa Jimbo la Singida Magharibi, Elibariki Kingu akizungumza na Wanafunzi wa Shule ya Msingi Mdughuyu iliyopo Kata ya Kaugeri wilayani Ikungi mkoani Singida wakati alipokuwa amewasili shuleni hapo jana kukagua ujenzi wa madarasa na vyoo.Awali shule hiyo ilikuwa na madarasa mawili tu lakini sasa ina madarasa manne yaliyo jengwa kwa msaada wa mbunge huyo na Diwani.

Mbunge wa Jimbo la Singida Magharibi, Elibariki Kingu akikagua ujenzi wa vyoo vya Shule ya Msingi Mdughuyu.
Mbunge wa Jimbo la Singida Magharibi, Elibariki Kingu akicheza pamoja na waimba kwaya wa Kijiji cha Mdughuyu.
Mbunge wa Jimbo la Singida Magharibi, Elibariki Kingu akiwahutubia Wananchi wa Kijiji cha Mdughuyu.
Wananchi wa Kijiji cha Mdughuyu wakiwa kwenye mkutano huo.
Wasanii wakitoa burudani
Mbunge wa Jimbo la Singida Magharibi, Elibariki Kingu, akimkabidhi fedha mmoja wa kiongozi wa Chadema aliyehamia CCM ili akanunue sare za chama.
Mbunge wa Jimbo la Singida Magharibi, Elibariki Kingu, akimtwisha ndoo ya maji Mwanafunzi wa Kidato cha tatu wa Shule ya Sekondary ya Mwaru, Faidha Jumanne kutoka katika bomba lililo jengwa shuleni hapo kwa msaada wa mbunge huyo.
Watoto wa Kata ya Mwaru wakiwa wamepanda kwenye miti wakimsikiliza mbunge wao.
Diwani wa Kata ya Mwaru Iddi Makangale akihutubia.



Na Dotto Mwaibale, Singida

WANANCHI wa Jimbo la Uchaguzi la Singida Magharibi wamesema wakati ukifika wa uchaguzi wa viongozi wa Serikali za mitaa na uchaguzi mkuu utakaofanyika mwakani wagombea wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Rais, Mbunge na Madiwani wabaki nyumbani wasiende kufanya kampeni kwani wao watawachagua tu.

Wananchi hao waliyasema hayo kwa nyakati tofauti jana katika mikutano ya hadhara iliyoandaliwa na Mbunge wa Jimbo hilo Elibariki Kingu yenye lengo la kuelezea kazi za miradi ya maendeleo zilizofanywa na Serikali ya awamu ya tano inayoongonzwa na Rais Dkt.John Magufuli na kusimamiwa na mbunge pamoja na madiwani.

"Mheshimiwa Mbunge wakati ukifika wa kampeni katika uchaguzi wa viongozi wa Serikali za mitaa na uchaguzi mkuu mwakani mbaki nyumbani msije kufanya kampeni tutawachagua tu kwa kura nyingi kwani maendeleo mliyotuletea kwa miaka minne mliyokuwa madarakani ni makubwa mno" alisema mkazi mmoja wa Kijiji cha Mdughuyu Kata ya Kaugeri wilayani Ikungi mkoani Singida aliyejitambulisha kwa jina moja la Manyama.

Manyama alimwambia Kingu kwamba Serikali ya CCM imefanya kazi kubwa ya kuwajengea barabara, shule na zahanati hivyo wanakila sababu ya kuwachagua wagombea watakao simamishwa kugombea nafasi za Wenyekiti wa Serikali za Mitaa, Urais, Ubunge na Udiwani kupitia chama hicho.

Mkazi mwingine wa Kata ya Mwaru aliyejitambulisha kwa jina la Shija alisema wagombea wa CCM waondoe mashaka kabisa kwani watachaguliwa wote tena bila ya kuharibika kwa kura hata moja. Shija alisema Serikali inayoongonzwa na Rais Dkt.Johnn Magufuli imejibu maswali yao kwani imewapelekea maji, shule na zahanati vitu walivyokuwa wamevikosa kwa zaidi ya miaka 50.

Akihutubia katika mikutano iliyofanyika Mdughuyu na Kata ya Mwaru Kingu alisema miradi hiyo yote inafanyika baada ya Rais kuzuia matumizi mabaya ya fedha za Serikali na kuzielekeza kwenye miradi ya maendeleo ya wananchi."Kwa kweli ninyi Wasukuma mnajua kuzaa mmetuletea huyu mwanaume Magufuli anafanya makubwa sana hapa nchini tuzidi kumuombea" alisema Kingu.

Kingu aliwaambia wananchi hao kuwa sasa wasubiri kupata umeme wa REA ambao tayari Serikali imetenga fedha za kuwawekea katika vijiji vyao kwa gharama ya sh.27,000 tu.Diwani wa Kata ya Mwaru Iddi Makangale alisema kazi inayofanywa na Rais Magufuli na Kingu ni ya kutukuka kwani inaonekana na wananchi wa kata hiyo wameiona kupitia miradi ya maendeleo iliyofanyika ndio maana wanasema wataichagua CCM kwa kura nyingi.

Katika mikutano hiyo baadhi ya wananchi waliokuwa ni wanachama wa Chadema pamoja na viongozi wao walijiunga CCM.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: