Wahitamu wa vyuo na vyuo vikuu nchini wametakiwa kuanza
kufikiria kujiajiri kwa kuishi na kutumia fursa ya mkopo wa asilimia 4
unaotolewa katika halmashauri kwa vijana ili wawe chachu ya mabadiliko
katika jamii kuweza kutoa ajira kwa vijana wenzao.
Akiongea
kwenye Mahafali ya Idara ya vijana wa CCM vyuo na vyuo vikuu mkoa wa
Arusha Mjumbe wa Halmashauri kuu ya CCM taifa MNEC UVCCM Mussa
Mwakitinya aliemuwakilisha Mwenyekiti wa UVCCM taifa khery James
amewataka vijana wasomi hao kuwa sehemu ya mabadiliko na chachu ya
maendeleo katika taifa.
Aliwaeleza
kuwa mtaani wanahitajika kujipambanua kwa kuanza kutengeneza fursa za
ajira na hili wasisubiri watakuwa wameonyesha taswira ya kumsaidia
Mh.Rais Dkt.John Magufuli katika Shamira yake kuelekea serikali ya
uchumi wa kati wa Viwanda.
"Vijana
nendeni mkachangamkie Fursa ya mikopo kuzalisha ajira kwani mnahitaji
kulifikiria hili kwa kuanza kujiajiri kwani chama pekee chenye imani ni
CCM mkaziishi imani za chama chetu katika jamii kukijenga na
kukiimarisha chama kupata ushindi katika chaguzi zilizopo mbele yetu"
Aliwataka
vijana hao kucha kujilweza kwa usomi wao bali wakakijenge chama katika
jamii kwa misingi ya uwajibikaji na mshikamano utakaosaidia chama hicho
kupata ushindi kwa kuwa wakalimani wa shughuli inayofanywa na serikali
ya chama chetu.
"Chama
chetu kinataka ushindi na Arusha iwe ya kijani vijana jitokezeni
kugombea ila nyie mkajipambanue ili tuweze kupata ushindi kwa kuziishi
na kutafsiri kanuni na utaratibu wa chama chetu"
Akawaambia
vijana hao kufuata Maadili mema wakati watakapopata fursa za ajira kwa
kuacha fikra za kupiga na badala yake wawe wazalendo kwa kutanguliza
taifa Lao mbele.
Awali
Mwenyekiti wa Idara ya vyuo na vyuo vikuu mkoa wa Arusha Baraka Solomon
amesema kuwa wasomi wana nafasi kubwa ya kuleta mabadiliko ndani ya
chama hicho na nchi kwa ujumla kama watatumia vyema taaluma zao
kuikomboa jamii kutoka hapo ilipo kuweza kujiletea maendeleo.
Amesema
kuwa mshikamano na ushirikiano uliopo kati yao na viongozi wa chama
mkoani hapa ndio umewafikisha hapo katika kukijenga chama ambapo
akawataka viongozi kuona umuhimu wa Idara hiyo kuwa na Mali kama ilivyo
chama hicho ikiwemo ofisi.
Alisema
kuwa vijana wanatakiwa kufanya mambo yao kwa teknolojia na mtandao ndio
maana wao kama viongozi walinunua kompyuta na printer kwa ajili ya
ofisi na wanampango wa kujenga ofisi ili ziendane na hadhi ya chama
hicho.
Kwa upande wake
katibu wa mkoa wa Arusha wa chama hicho Mussa Matoroka aliemuwakilisha
Mlezi wa chama hicho Humphrey Polepole aliwapongeza Idara hiyo kwa
kuhakikisha Arusha inakuwa ya kijani sanjari na kuwataka kuwa mabalozi
wazuri wa kukitangaza chama hicho na kugombea nafasi za uongozi kwenye
chaguzi.
Akawataka
kutumia nafasi ya ushirikiano popote watakapoenda kwa kuhubiri amani
kwani walifanya uamuzi sahihi kuwa sehemu ya chama hicho nasi tutawapa
ushirikiano wakati wowote kukijenga chama chetu ili Arusha iwe ya
kijani.
"Serikali inataka
kumuweka mtu ambayo habari zake zipo wazi tumieni nafasi hii kuweza
kutoa taarifa zenu kwenye kanzidata kwani sasa hamna kushikana mkono
bali ujuzi na taarifa zako ndio zitawapata viongozi wenye weledi"
Akaendelea
kuwataka kutoa data zao kwa faida ya kujenga mtandao mpana wa uongozi
na wasomi hao vijana ndio ambao wataijenga nchi bila kujali uwezo wao
akibainisha wa tafakari katika muktadha wa kujiajiri ili kupata suluhu
ya tatizo la ajira.
Nae
Mjumbe wa Halmashauri kuu ya CCM taifa MNEC Annagatha Msuya alisema kuwa
mshikamano miongoni mwa vijana hao na kuisemea serikali utasaidia
kukijenga chama hicho na kuwataka kuwa mabalozi wazuri na wazalendo huko
mitaani kukisemea mazuri yanayofanywa na serikali.
Post A Comment: