Mwanamuziki wa Bongo fleva Nandy anayetokea nyumba ya vipaji THT na mpenzi wake rapa Billnas hatimaye wameanika penzi lao hadharani baada ya kulificha kwa muda mrefu.

Kwa kipindi kirefu Kumekuwa na tetesi kuwa Nandy na Billnas wana mahusiano ya kimapenzi na hata picha zao wakiwa maeneno sawa kwa wakati mmoja zilisambaa lakini kila mmoja alikana mahusiano hayo na kusisitiza kuwa ni marafiki.

Lakini waswahili wanasema mapenzi kikohozi kwani baada ya kuficha kwa muda mrefu hatimaye wawili hao wameonekana wakiwa pamoja kwenye picha ambazo wameposti Kwenye mtandao wa Instagram.

Leo ni siku ya kusheherekea siku ya kuzaliwa ya Billnas kama ilivyo desturi Nandy kamtakia heri ya siku yake ya kuzaliwa Kupitia ukurasa wake wa Instagram Nandy kamuandikia ujumbe wa heri na kusindikiza na picha yao:

Share To:

msumbanews

Post A Comment: