Polisi mkoani Katavi wamefanikiwa kuwaua watu wawili wasiofahamika wanaodhaniwa kuwa ni majambazi katika majibizano ya risasi.
 
Kamanda wa Polisi mkoani hapa, Damasi Nyanda, alisema  tukio hilo lilitokea Januari 26 saa 4 za usiku katika Kijiji cha Kapalamsenga Wilaya ya Tanganyika. 

Alisema kabla ya tukio hilo, polisi walipata taarifa kutoka kwa raia wema kuwa kijijini hapo kuna watu ambao ni wageni na hawaeleweki mienendo yao, ambapo walihofia huenda wakawa wamefika kufanya ujambazi. Alisema baada ya taarifa hizo polisi walianza kufanya msako wa kuwatafuta watu hao, ambao wapo watano kisha walianza kuandaa mtego wa kuwakamata. 

Alisema kabla ya kuwakamata walishtukia mtego huo na kuanza kuwarushia polisi risasi   ambapo  polisi nao walijibu mapigo na kuwaua wawili na kuwakamata watatu  na waliwakuta wakiwa na bunduki tatu aina ya SMG na risasi 16  pamoja na magazini tano. Kamanda Nyanda alisema watu hao walikutwa na vipande vya  meno ya tembo vyenye uzito wa kilo 6.6 yakiwa na thamani ya zaidi ya Sh. milioni 34  pamoja na nyama ya pofu kilo 20 yenye thamani ya Sh. milioni nne.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: