Wananchi wanaoishi Kata ya Nduruma katika halmashauri ya Arusha DC wameondokana na kero ya ubovu wa barabra ambapo  Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini(TARURA) wameanza kutekeleza ujenzi wa barabara hiyo ya Malalua -Nduruma yenye urefu wa kilomita 28 ikiwa na thamani ya sh, bilioni 30.8 itakayowaondolea kero ya usafiri ikiwemo usafirishaji wa mazao yao. 

Shukrani hizo zilitolewa na wananchi hao mara baada ya Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Asmil Ali Ussi wakati mwenge huo ulipoweka  jiwe la msingi na kukaguliwa barabara hiyo. 

Elizabeth Kaaya alisema awali barabara hiyo ya ilikuwa na changamoto sababu ya mashimo na vumbi linaloleta kero kwa wasafiri hali iliyopelekea daladala kupandisha nauli kutoka sh,2500-3000 badala ya sh, 1500.

Alisema kujengwa kwa barabara hiyo kutasaidia maendeleo kupatikalisema ambio za mwenge ameagua mradi wa uboreshaji wa barabara kwa ni awali

 Ilikuwa na changamoto kubwa kwa wananchi hao huku  dereva wa bodaboda Lazaro Marko mkazi wa kitongoji cha bwawani akiishukuru serikali kwa ujenzi wa barabara hiyo ambayo awali ilikuwa na changamoto

"Sisi wananchi tunaishukuru serikali kwa kutengeneza barabara hii ya Nduruma awali ilikuwa ni kero lakini pia kwa bodaboda napo bei juu kuliko mahali unapoenda, tunaomba barabara hii ikamilike kwa wakati kwani leo wamezindua ujenzi wa mita 600

Ambapo Mkimbiza mwenge,Usi alisisitiza barabara hiyo kukamilika kwa wakati ili wananchi waweze kuitumia kusafirisha bidhaa zao na kusisitiza kuwa serikali itaendelea kutatua changamoto za wananchi hususan katika sekta ya miundombinu ili kurahisisha usafiri na usafirishaji wa bidhaa

Awali Meneja wa Tarura Wilaya ya Arumeru, Injinia Julius Kaaya alisema barabara hiyo ilianza kujengwa Septemba 13,2024 na inatarajia kumalizika Agosti 8,2025



Mashabiki   wa Timu za Simba na Yanga ambao ni watumishi wa Chuo cha Maendeleo ya Jamii Tengeru(TICD), wamecheza mechi ya kirafiki katika juhudi za kuendelea kudumisha mahusiano na ushirikiano katika maeneo ya kazi.

Akizungumza katika bonanza hilo Mgeni rasmi Kaimu Naibu Mkuu wa chuo cha Maendeleo ya Jamii Tengeru (TICD),anayeshughulikia Mipango na Utawala bi.Janeth Zemba  alisema kuwa lengo hasa la bonanza hilo ni kuendelea kutangaza taasisi hiyo kupitia michezo.

"Bonanza hili ni la tatu kufanyika na leo hakuna aliyepatikana mshindi kwa kuwa sio mashabiki ya Simba wala Yanga aliyemfunga  mwenzake hivyo tutaendelea kushirikiana katika  michezo kwa kuwa inajenga mahusiano mema,ni furaha amani na pia inatuweka vizuri kiafya kupitia mazoezi tunayoyafanya mwaka mzima hivyo  tutaendelea kuboresha na kushirikiana  pia na wadau mbali mbali ".Alisema bi.Zemba

Aidha alitumia fursa hiyo kuwaasa wadau mbali mbali kuendelea kudumisha mshikamo na ushirikiano,na kuendelea kuitangaza taasisi hiyo kupitia sekta hiyo ya burudani ambayo inaleta makada mbali mbali.

Kwa upande wake Mkuu wa chuo hicho Daktari Bakari George alisema kuwa bonanza hilo  linaleta watumishi na jamii ya maendeleo ya tengeru pamoja na ni mfulululizo wa bonanza ambalo linawakutuanisha pia na watu maarufu ambao wamewahi kutumikia vilabu vikubwa nchini vya Simba na Yanga.

"Mwaka Jana katika bonanza kama hili tuliwashirikisha wasemaji wa timu hizi mbili na Leo pia Mwaka huu tuna wachezaji ambao ni Mrisho Khalifan Ngassa ambaye amewahi kucheza katika klabu ya Yanga na Daniel Mrwanda ambaye aliwahi kucheza katika timu ya Wekendu wa Msimbazi Simba na timu ya Taifa pia "Alisema dkt.Bakari 

Dkt.Bakari alisema kuwa nia kubwa ni hamasa ya michezo na vilevile kuitangaza taaisisi hiyo ya TICD,kupitia sekta ya michezo ambayo huleta watu wengi pamoja.

Hata hivyo alisema kuwa bonanza hilo ni kichocheo kikubwa kwa watumishi kuendelea kufanya mazoezi mwaka mzima na kulete tija katika maeneo ya kazi.

Bonanza hilo limekutanisha mashabiki wa timu ya Simba na Yanga kutoka katika viunga wa mkoa wa Arusha,ambapo limekuwa likijipatia umaarufu mwaka hadi mwaka ambapo lengo ni kulipeleka katika maeneo mengine nchini.

Mechi ya utangulizi ilikutanisha timu ya Wanafunzi wa chuo Cha Maendeleo ya Jamii Tengeru (TICD) ambao ni mashabiki wa Simba na Yanga,ambapo matokeo yalikuwa ni 1-1 mchezo uliofanyika katika uwanja wa chuo Cha Mifugo Tengeru.













Mwenge wa UhuruWanafunzi wa zaidi 80  wanaosoma shule ya sekondari Malula kata ya Malula Wilayani Arumeru wameondokana na adha  ya mabweni baada ya Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF)kujenga bweni lenye thamani ya milioni 168.4

Uzunduzi wa bweni hilo ulifanywa na  Kiongozi wa  mbio za mwenge Kitaifa, Ismail AliUssi mara baada ya kukagua bweni hilo lenye vyumba 20 vitanda 40 na kupongeza juhudi za serikali katika kuinua sekta ya elimu

Alisema mradi huo ni wa kimkakati unaopelekea wanafunzi kupata elimu bora , ndio maana serikali imeboresha sekta ya miundombinu ya elimu ili kuhakikisha ufaulu wa wanafunzi unaongezeka zaidi. 

"Mradi huu umetekelezwa kwa ufasaha chini ya Uongozi wa Rais Samia Hassan Suluhu hivyo alimpongeza Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Mwinyi Ahmed Mwinyi na viongozi wengine kwa ujenzi wa shule hiyo katika kuhakikisha kiwango cha elimu kinaongezeka"

Alisisitiza wananchi kujitokeza kushiriki uchaguzi mkuu kwa amani na utulivu hivyo na kuwapongeza wanafunzi kupitia klabu ya Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa(Takukuru) kuhakikisha wanatekeleza uadilifu na kushika yale yote wanayoelekezwa ili kupinga rushwa ikiwemo walimu kusimamia wanafunzi hao kupata elimu na kuendelea na mapambano dhidi ya rushwa 

Akisoma taarifa ya mradi huo Mwenyekiti wa Kamati inayosimamia miradi ya Tasaf, Onesmo Nanyaro alisema mradi huo utasaidia wanafunzi kusoma kwa bidii ikiwemo kuondokana na adha ya ukosefu wa malazi 

Awali akipokea mwenge wa uhuru kutoka Mkoani Kilimanjaro , Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Kenan Kihongosi alisema mwenge huo utazindua miradi 54 yenye thamani ya sh, bilioni 30.3 katika halmashauri saba 

Mwenge huo uliwasili jana mkoani Arusha na kukabithiwa eneo la King'ori Kibaoni  Wilayani Arumeru ukitokea Mkoani Kilimanjaro ambapo utapitia  miradi 54 kisekta yenye thamani ya sh, bilioni 30.3 mkoani hapa.












Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Ismail Ali Ussu ameipongeza Serikali ya awamu ya sita chini ya Mhe.Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan Serikali, kupitia Wakala wa Barabara za  Mijini na Vijijini (TARURA), kwa kutoa fedha nyingi za utekelezaji wa miradi ya  miundo ya barabara nchini, licha ya kurahisisha usafiri imechochea kasi ya maendeleo na kukuza uchumi katika maeneo mengi.

Akizungumza wakati akiweka Jiwe la Msingi mradi wa ujenzi wa Daraja la zege na chuma barabara ya Usa River - Maji ya Chai halmashauri ya Meru, daraja lililojengwa na  kwa gharama ya shilingi milioni 499.8,ameipongeza TARURA Arumeru kwa kazi nzuri waliyoifanya inayoakisi dhamira njema ya Mhe.Rais.

Kupitia mradi huo, Kiongozi huyo amesema kuwa, Serikali ya awamu ya sita chini ya uongozi mahiri wa Dkt.Samia Suluhu Hassan, imefanya kazi nzuri katika sekta zote ikiwemo miundo mbinu ya barabara na wilaya ya Arumeru ni moja ya eneo lililonufaika sana kwa kuzingatia miradi mingi iliyotekelezwa kwa kipindi cha awamu ya sita

"Nimeishuhudia kazi nzuri ya ujenzi wa daraja hili la mawe na chuma, daraja ambalo limejengwa kwa kuzingatia viwango vya ubora vinavyoenda na thamani ya fedha zilizotolewa na tayari limeanza kuwahudumia wananchi wa maeneo haya, ninaipongeza sana TARURA kwa kazi hii nzuri". Amesema

Ameongeza kuwa, kupitia mradi huu,  Mwenge wa Uhuru umeleta matumaini mapya kwa wananchi wa halmasahuri ya Meru, wananchi wamepata furaha na amani, kwa kuwa timu imejiridhisha daraja hilo limejengwa kwa ubora wa hali ya juu.











Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), Bw. Moremi Marwa, Julai 4, 2025, amefanya ziara maalum katika Banda la TTCL kwenye Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa (SabaSaba), yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam.

Katika ziara hiyo, Bw. Marwa alipokelewa na wataalamu waandamizi wa TTCL, ambao walimtembeza katika maeneo mbalimbali ya banda hilo na kumweleza kwa kina kuhusu huduma na teknolojia zinazotolewa na Shirika hilo.

Miongoni mwa huduma zilizowasilishwa ni pamoja na Faiba Mlangoni, inayowezesha upatikanaji wa intaneti ya kasi moja kwa moja majumbani na maofisini, ikiwa ni sehemu ya dhamira ya TTCL kuhakikisha kila Mtanzania anapata huduma bora za mawasiliano kwa gharama nafuu.

Pia alielezwa kuhusu Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano (NICTBB), ambao tayari umesambazwa katika mikoa yote 26 na wilaya 112 kati ya 139 nchini. Mkongo huo umeunganisha Tanzania na nchi jirani na kuchochea matumizi ya TEHAMA katika utoaji wa huduma kwa wananchi.

Huduma nyingine alizotembelea ni pamoja na Kituo cha Taifa cha Kuhifadhi Taarifa Kimtandao (NIDC), chenye uwezo wa kisasa wa kuhifadhi na kulinda taarifa muhimu za taasisi na kampuni mbalimbali, na hivyo kuchangia ukuaji wa uchumi wa kidijitali nchini.

Aidha, Mkurugenzi Mkuu alifahamishwa kuhusu huduma ya Call Center ya TTCL inayosaidia mashirika kuwasiliana kitaalamu na wateja wao, pamoja na WiFi ya Umma (Public WiFi) inayowawezesha wananchi kupata huduma ya intaneti kwa urahisi katika maeneo ya wazi.

Katika kuendeleza ushirikiano wa kimkakati, Bw. Marwa pia alitembelea mabanda ya taasisi mbalimbali rafiki, ikiwemo Shirika la Posta Tanzania (TPC), Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF), Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo (SIDO), Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA), pamoja na Banda la Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari.

Katika kila banda, alielezwa kuhusu majukumu na huduma zinazotolewa, huku akisisitiza umuhimu wa kuimarisha ushirikiano ili kufanikisha malengo ya pamoja ya kidijitali na kiuchumi kwa maendeleo ya Taifa.