Wakazi wa Mbezi Beach, Dar es Salaam walishtuka baada ya mwanamke mmoja kugundua kuwa mume wake alikuwa amemwandikisha mwanamke mwingine kwenye bima ya afya ya kampuni alikofanya kazi akimwita “mke wake wa ndoa.” Tukio hilo lilizua taharuki kwa familia hiyo, huku likizua mjadala mkubwa kwenye makundi ya wanawake mtandaoni.

Kwa miaka sita ya ndoa yetu, nilidhani nina mume mwaminifu. Tulikuwa tumepitia mengi pamoja kushiriki ndoto, kupambana na madeni, na hata kupata mtoto mmoja wa kiume.

Sikuwahi hata mara moja kuwa na mashaka juu ya uaminifu wake. Lakini kama wanavyosema, mchana wa ndoa ni mrefu, na ndani yake kuna mawingu yasiyotabirika.

Kisa chote kilianza siku moja nilipoambatana na mume wangu hospitalini baada ya kuumwa ghafla. Alikuwa na bima ya afya ya kazini, hivyo aliwasilisha kadi yake mapokezi. Muda mfupi baadaye, mhasibu wa hospitali alituita pembeni na kuuliza iwapo “mke wa pili” naye angepata huduma. Nilidhani ni makosa ya kawaida ya kiutawala. Soma zaidi hapa 

 

Hospitali moja kubwa jijini Dar es Salaam iliwahi kuandaa wasifu wa kifo kwa mgonjwa ambaye madaktari walithibitisha hakuwa na matumaini ya kupona tena. Wauguzi waliambiwa kuwa muda wowote wangehitajika kutoa taarifa rasmi ya kifo. 

Familia yake ilishaandaa jeneza na michango ya mazishi ilianza kutumwa. Lakini kwa mshangao wa kila mtu, mgonjwa huyo aliamka, akapata nafuu ya ghafla, na leo hii anaendesha biashara yake mwenyewe akiwa na afya tele.

Kwa wiki kadhaa, habari hii ilisambaa sana kwenye mitandao ya kijamii huku wengi wakijiuliza, “Huyu jamaa alifufuka?” Au “Ilikuwa bahati tu?” Hii ni hadithi isiyo ya kawaida, lakini kwa Hassan Mussa mwenyewe, aliyepitia masaibu hayo, anasema hiyo si bahati bali ni nguvu ya tiba ya mitishamba ya kweli. Soma zaidi hapa 

NA EMMANUEL MBATILO, BAGAMOYO

WAKALA wa Maendeleo ya Uongozi wa Elimu (ADEM) umesaini Hati ya Makubaliano ya Ushirikiano (MoU) na Shirika la Elimu lisilo la Kiserikali kutoka Ubelgiji, VVOB, kwa lengo la kuimarisha maendeleo ya kitaaluma ya viongozi wa shule za sekondari nchini Tanzania.

  

Mashuhuda wanasema ilikuwa siku ya kawaida ya jioni, watu wakifanya shughuli zao za kila siku, hadi ghafla utulivu ukavunjwa na sauti ya kijana mmoja aliyekuwa akipaza sauti kueleza tukio la ajabu.

Kijana huyo, aliyekuwa amevaa fulana nyepesi na suruali ya zamani, alisimama katikati ya barabara ndogo na kuanza kueleza hadharani jinsi alivyoingia kwenye nyumba ya mtu usiku bila ruhusa, akitaja hata baadhi ya vitu alivyoviona mle ndani.

Watu waliokuwa karibu walianza kukusanyika, wengine kwa mshangao, wengine kwa udadisi, na wachache wakirekodi kwa simu zao. Soma zaidi hapa 

 









Na Mwandishi Wetu – Dodoma

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ametoa wito kwa mashirika yasiyo ya kiserikali, sekta binafsi na taasisi za dini kuimairisha ushirikiano na Serikali na kujiunga katika mtandao wa kitaifa wa usimamizi wa huduma za kibinadamu.

Wito huo umetolewa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu Mhe. Willium Lukuvi wakati akimwakilisha Waziri Mkuu katika Maadhimisho ya Siku ya Watoa Huduma za Misaada ya Kibinadamu Duniani tarehe 19 Agosti, 2025 Jijini Dodoma.


“Ninatoa wito kwa mashirika yasiyo ya kiserikali, sekta binafsi na taasisi za dini kuimairisha ushirikiano na Serikali na kujiunga katika mtandao wa kitaifa wa usimamizi wa huduma za kibinadamu, kwa kufanya hivyo kutaongeza uratibu, uwajibikaji na ufanisi katika kushughulikia majanga” ameeleza

Aidha, amesisitiza watoa huduma za kibinadamu kutia mkazo katika suala la kuelimisha umma ili wananchi waweze kuzingatia maelekezo yanayotolewa na wataalamu ili kuweza kupunguza athari za majanga pindi yanapotokea.


“Kwa kuwa yapo majanga ambayo hayakwepeki, ninawasihi sana watoa huduma za kibinadamu, kutilia mkazo suala la kuelimisha umma. Wananchi waelimishwe kuzingatia maelekezo yanayotolewa na watalaamu ili kupunguza athari za majanga yanapotokea” amefafanua.

Mbali na hayo amewataka wananchi kushiriki kikamilifu katika utekelezaji wa mikakati na kampeni zote za uhifadhi na utunzaji wa mazingira kwani kwa kufanya hivyo kutawezesha katika kukabiliana na majanga hususan yale ya asilia.

“Suala na utunzaji wa mazingira ni muhimu sana katika kukabiliana na majanga hususan yale ya asilia, nitoe wito kwa wananchi wote kushiriki kikamilifu katika utekelezaji wa mikakati na kampeni zote za uhifadhi na utunzaji wa mazingira. Hatua mojawapo muhimu ni kuhamia kwenye matumizi ya nishati safi hivyo niwakumbushe Watanzania wote kushiriki kikamilifu katika kampeni hizo muhimu za Kitaifa” amesisitiza.

 Akizungumza kuhusu Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge unaotarajiwa kufanyika 29 Oktoba, 2025 amewataka Watanzania kushiriki kikamilifu katika kuwachagua Viongozi wao akiwemo Rais, Wabunge na Madiwani. 

“Tujitokeze kwa wingi kutumia haki yetu ya kikatiba, kila Mtanzania atambue kuwa kupiga kura ni haki na wajibu wake ili kuwapata viongozi bora watakaoharakisha maendeleo ya taifa letu” amesisitiza Waziri Lukuvi.

Maadhimisho ya Siku ya Watoa Misaada ya Kibinadamu Duniani huadhimishwa kila mwaka tarehe 19 Agosti, Kaulimbiu ya Maadhimisho hayo kwa mwaka 2025 inasema 

“Kuimarisha Utoaji wa Huduma za Kibinadamu na Ustahimilivu Dhidi ya Majanga.” 




Na Oscar Assenga,TANGA

JUMUIYA wa Wafanyabiashara Tanzania (JWT) Mkoa wa Tanga imemshukuru Rais Dkt Samia Sukuhu kwa kutatua kero za wafanyabiashara na hivyo kuwawezesha kufanya shughuli zao kwa ufanisi kutokana kuondolewa kwa vikwazo ambavyo walikwa walikabiliana navyo awali.

Hayo yalisemwa leo na Katibu wa JWT mkoa wa Tanga Ismail Masoud wakati akizungumza na waandishi wa habari Jijini Tanga kutoa shukrani kwa Rais Samia Suluhu na Serikali kwa mambo aliyoyafanyia wafanyabiashara Tanzania hatua ambayo imepeleka kupandisha mapato kupitia Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA)

Masoud ambaye pia ni Mjumbe Bodi ya Jumuiya ya Wafnyabiashara Tanzania (JWT) alizitaja changamoto ambazo awali zilikuwa zinawakili na sasa zimepatiwa ufumbuzi ni pamoja na umeme ambapo alisema ulipelekea kutokuzalisha kisawasawa kutokana na matatizo ya umeme .

Alisema kufuatia uwepo wa changamoto hiyo,Serikali ya awamu ya sita ilitatua tatizo hilo kupitia Bwawa la Mwalimu Nyerere ambalo limekwisha na hivyo kupelekea kuondoa mgao wa umeme hivyo wanaishukuru awamu ya sita na mamlaka ya mapato Tanzania (TRA) kwa makusanyo.

 


Hadi sasa kati ya mambo ambayo siwezi kuja kuyasahau katika maisha yangu ni matukio ya kukabwa nikiwa ndotoni na watu ambao nakuwa nawafahamu hasa rafiki zangu lakini nikishaamka siwakumbuki tena.

Naitwa Meshaki, mwaka mmoja na nusu uliyopita nilikumbwa na changamoto moja kubwa sana katika maisha yangu, hasa pale ambapo nilianza kuota ndoto za kutisha kiasi kwamba nilikuwa hadi napata mawazo ukifika wakati wa kulala.

Nilijaribu kwenda kwa waganga wa jadi na kuwasilimulia ndoto ambazo nazikumbuka waweze kuniambia nini maana yake lakini wengi hao walisema wanashindwa kutambua changamoto yangu, huku wengine wakitaka kiasi kikubwa cha fedha.

Hali ile iliendelea kwa miazi kadhaa na kubadilika na kuwa mbaya zaidi kwani safari hii nilikuwa nanyongwa kabisa ndoto na kikundi cha watu ninaowafahamu na wengine ni rafiki zangu kabisa lakini nikishtuka nakuwa sikumbuki chochote huku mwili ukitokwa jasho lingi. Soma zaidi hapa 


Majirani wa Kimara, Dar es Salaam walishuhudia furaha isiyoelezeka pale ambapo mama mkwe ambaye awali alikuwa akiendesha chuki na matusi dhidi ya mkwe wake kwa kutopata mtoto, alionekana akimpa zawadi za kila aina mama huyo baada ya kujifungua mapacha wa kiume. Kisa hiki kimezua mjadala mitaani kuhusu jinsi mitishamba inavyochangia kutatua matatizo ya uzazi.

Kwa miaka saba ya ndoa yangu na mume wangu Raymond, kila siku ilikuwa ni vita visivyoisha. Tatizo halikuwa ndoa yetu kama msingi mume wangu alikuwa mpole, mcha Mungu na mwenye huruma bali lilikuwa ni presha ya mama yake ambaye alionekana kuwa na hasira ya kudumu juu ya kutopata mjukuu.

Nilipoolewa, nilikuwa msichana wa miaka 26, nikiwa bado nina ndoto nyingi maishani. Tulipanga kupata mtoto ndani ya mwaka mmoja, lakini mambo hayakwenda kama tulivyotarajia.

Miezi iligeuka kuwa miaka, vipimo vya hospitali havikuonyesha tatizo lolote kwetu wawili. Hata hivyo, kila mwaka ulivyozidi kwenda, ndivyo mama mkwe alivyozidi kuamini kuwa mimi ndiye tatizo. Soma zaidi hapa 

 


Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Mha. Felchesmi Mramba amesema kuwa katika miradi ya kimkakati inayotekelezwa nchini Wizara ya Nishati inatekeleza takribani miradi saba.

Mhandisi Mramba ameyasema hayo Agosti 17, 2025 wakati wa uzinduzi wa Mpango wa Uwezeshaji wa Kiuchumi kwa Vijana (YEE) ambao unagusa maeneo yanayopitiwa na mradi wa Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP).

“Miradi hiyo ni mradi wa Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP), Bwawa la Julius Nyerere (JNHPP), Mradi wa kugeuza gesi kuwa kimiminika (LNG), Mradi wa utafutaji mafuta, Miradi ya umeme ya Rumakali na Ruhudji na utafiti wa mafuta eneo la Mnazi Bay North”, amesema Mha. Mramba.

Ameeleza kuwa katika miradi hiyo saba, mradi wa bwawa la kufua umeme kwa maji wa Julius Nyerere unaozalisha megawati 2,115 umekamilika na unaingiza umeme kwenye gridi ya Taifa.

Ameongeza kuwa mradi wa bomba la mafuta ghafi (EACOP) umefikia asilimia 65 na upo mbioni kukamilika, mradi wa LNG  upo katika hatua za mwisho na miradi ya umeme ya  Ruhudji na Rumakali tafiti zimekamilika.

Aidha, amesema Serikali ya Tanzania imeshachangia takribani shilingi trilioni 1.12 kwenye mradi wa EACOP kama hisa ya Tanzania katika mradi huo na kuna kampuni za kitanzania 200 ambazo zinatekeleza kazi mbalimbali katika mradi wa EACOP ambazo zitalipwa i jumla ya shilingi trilioni 1.325.

Mhandisi Mramba ametanabaisha kuwa mbali ya fursa za kiuchumi zinazopatikana pia wananchi wa maeneo ambayo  mradi ya umeme inayopeleka umeme EACOP itapita watanufaika kwa kuunganishwa na huduma ya umeme.



Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Viongozi Wanawake duniani (WPL), Neema Lugangira ameshauri wahariri kuhakikisha wanatumia kwa usahihi teknolojia ya Akili Unde (AI) wakati wa Uchaguzi Mkuu kuepusha madhara katika vyombo vya habari.

Akitoa mada ya 'Uchaguzi Mkuu na Matumizi ya AI'  kwenye mkutano wa kawaida wa TEF, jijini Dar es Salaam ameeleza katika uchaguzi kuwa kuna taarifa nyingi potofu hivyo AI inaweza kutumika vizuri kuhakiki usahihi wa taarifa.

"Kuna faida nyingi za kutumia AI ikiwemo kusaidia kuhakiki taarifa kwa haraka, kufuatilia kauli za uchochezi hata uchambuzi wa data," amesema.

Lugangira ameendelea kueleza kuwa licha ya AI kuwa na matumizi makubwa kwenye dunia ya sasa, pia hutumika kupotosha jamii sambamba na kuharibu heshima ya mtu ama mgombea katika jamii.

Hata hivyo amesisitiza kwamba, vyombo vya habari vina jukumu kubwa la kulinda maadili katika Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika tarehe 29 Oktoba 2025.

Sambamba na hayo Lugangira alikabidhi nakala 40 kwa Jukwaa la Wahariri na 20 kwa Chama cha Wanahabari Wanawake (TAMWA) za mwongozo wa Jumuiya ya Tume za Uchaguzi Afrika (AAEA) kuhusu matumizi ya mitandao ya kijamii na Teknolojia kwenye chaguzi barani Afrika ambapo miongozo hiyo alishiriki kuiandaa wakati akiwa mjumbe wa timu ya wataalamu mwaka wa 2022/2023.






  

Matukio ya wizi katika maeneo mengi ya Kenya yamekuwa kero kubwa kwa wananchi ambao mara nyingi huachwa na majonzi na hasara baada ya kupokonywa mali zao, na hali hii imekuwa ikiongeza hofu kila siku kwani watu hufanya biashara au safari zao bila uhakika wa usalama wa mali zao.

Mara nyingi wahanga wa wizi hupoteza matumaini ya kurudishiwa mali zao kwa sababu wezi mara nyingi huenda mafichoni au huuza vitu hivyo kwa haraka, jambo linalosababisha wengi kuamini kuwa haki haiwezi kupatikana kupitia njia yoyote zaidi ya kuvumilia hasara.

Lakini simulizi ya kijana mmoja kutoka mtaa wa Kayole, Nairobi, ni ya aina yake kwa sababu wezi waliompora simu yake walijikuta wamelazimika kuirudisha baada ya muda mfupi, na sio tu kuirudisha bali walifanya hivyo wakiwa wanalia kwa sauti kubwa mbele ya watu waliokusanyika kushuhudia tukio hilo la ajabu. Soma zaidi hapa 

Walikuwa wananiita “mshenzi wa mapenzi.” Marafiki zangu wa karibu walinicheka kwa siri, wengine wakisema sijui kuchagua wanaume, wengine wakinihurumia kwa kimya. Katika familia, nilikuwa mfano wa “usiotakiwa kufuatwa”ndugu walinitumia kama somo kwa wadogo zangu, “msije kuwa kama dada yenu.”

Kwa miaka nane, nilihangaika kwenye mahusiano yaliyokuwa na maumivu tu. Nilivumilia udhalilishaji, nililipa kodi ya nyumba kwa wanaume wasiokuwa na kazi, nilishuhudia wanaume wakinipenda mchana na kunisaliti usiku. Kuna wakati mmoja nilimkuta mchumba wangu wa wakati huo amelala na mpango wake wa kando kitandani kwangu. Nilihisi dunia imenimeza.

Nilikuwa nimefikia mahali ambapo nilijiona sifai kupendwa. Nilijiambia pengine mimi siyo mrembo, au kuna kitu kibaya ndani yangu kinachowafanya wanaume kunitumia kisha kunitupa. Nilijaribu kubadilika kubadilisha mtindo wa nywele, mavazi, tabia… lakini bado nilikuwa naishia kuumizwa. Soma zaidi hapa 

 


Wakazi wa mkoa wa Shinyanga na mikoa ya jirani wametakiwa kujitokeza kwa wingi kupima afya za mioyo yao pamoja na saratani ya shingo ya kizazi huduma zinazotolewa kwenye kambi maalumu ya matibabu inayofanyika katika Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Shinyanga (SRRH).

Wito huo umetolewa leo na Mkuu wa Mkoa huo Mhe. Mboni Mhita wakati akifungua kambi maalumu ya siku tano ya upimaji na matibabu ya moyo na saratani ya shingo ya kizazi inayofanyika katika Hospitali hiyo.

Mhe. Mboni alisema mkoa wa Shinyanga ni moja ya mikoa ambayo iko mbali na Hospitali zinazotoa huduma za kibingwa za matibabu ya magonjwa mbalimbali ikiwemo moyo kuwepo kwa kambi hiyo ya matibabu kutawasaidia wananchi kupata huduma ya uchunguzi na matibabu kwa urahisi tofauti na ambavyo wangezifuata Dar es Salaam.

“Tunaishukuru Serikali kwa uwekezaji mkubwa ulioufanya katika sekta ya afya hii ikiwa ni pamoja na kujenga majengo ya kisasa, kusomesha wataalamu na kununua vifaa tiba vya kisasa, huduma za matibabu ya ubingwa bobezi zimesogezwa karibu zaidi na wananchi hii ndiyo maana mnaona leo wataalamu wetu wako hapa Shinyanga kutoa huduma kwa wananchi”, alisema Mhe. Mboni.

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga (RMO) Dkt. Yudas Ndungile alisema katika kambi hiyo kutakuwa na madaktari bingwa wa moyo kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) ambao watatoa huduma za kibingwa za uchunguzi wa magonjwa ya moyo, elimu ya magonjwa ya moyo na kuwajengea uwezo wataalamu wa afya kutoka hospitali zote za wilaya za mkoa huu.

“Pia tuko na wataalamu kutoka Hospitali ya Aga Khan ya jijini Dar es Salaam ambao wanatoa huduma za uchunguzi wa saratani ya shingo ya kizazi, elimu ya magonjwa ya saratani, pamoja na matibabu ya awali ya ugonjwa huu ambao watakuwepo katika hospitali hii kwa muda wa wiki moja baada ya hapo watakwenda wilaya za Shinyanga na Kahama”, alisema Dkt. Yudas Ndungile.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Peter Kisenge alisema kutokana na tatizo la magonjwa ya moyo ambayo yanaweza kuzuilika kwa kufuata ushauri wa kitaalamu kuwa kubwa na kusababisha vifo vya watu wengi, JKCI ilianzisha program ya Tiba Mkoba ya Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Outreach Services kwa kusogeza huduma za ubingwa bobezi kwa wananchi kwa kuwafuata mahali walipo.

“Katika program hii tunashirikiana na wataalamu wa Hospitali za Kanda, Mikoa, Wilaya na Vituo vya Afya kutoa huduma za uchunguzi na matibabu ya moyo, elimu ya lishe bora na matumizi sahihi ya dawa za moyo kwa wananchi. Tunawajengea uwezo wataalamu wa Afya wa kutambua na kutibu magonjwa ya moyo ili watakapowapata wagonjwa waweze kuwapa matibabu sahihi na kwa wakati”, alisema Dkt. Kisenge.

Dkt. Kisenge alisema tangu program hiyo imeanza mwaka 2022 wameshatoa huduma katika mikoa 21 na maeneo ya kazi 17 na kuwafikia watu 35,456 watu wazima wakiwa 32,345 na watoto 3,111 kati ya hao 12,685 watu wazima wakiwa 12,164 na watoto 521 walikutwa na matatizo mbalimbali ya moyo na kuanzishiwa matibabu.

“Katika ya watu tuliowaona wagonjwa 3,199 watu wazima 2,857 na watoto 342 walikutwa na matatizo yaliyohitaji matibabu ya kibingwa na kupewa rufaa ya kwenda kutibiwa JKCI” alisema Dkt.Kisenge

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mhe. Dkt. Doto Biteko leo amezindua  Mpango wa Uwezeshaji wa Kiuchumi kwa Vijana (YEE) ambao unagusa maeneo yanayopitiwa na mradi wa Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP) ikiwa ni jitihada zinazoendelea kufanywa na Serikali katika kuhakikisha kuwa jamii zilizo karibu na miradi zinanufaika na miradi hiyo.

Akizindua mradi huo katika  Kijiji cha Bukombe, wilayani Bukombe, Mkoa wa Geita tarehe 18 Agosti 2025, Dkt. Biteko amesema mradi huo wa Uwezeshaji Vijana Kiuchumi ni moja ya miradi iliyopangwa kuwezeshwa na Kampuni ya EACOP kwa kipindi cha ujenzi na baada ya ujenzi ikiwa ni sehemu ya Uwajibikaji wa Kampuni hiyo kwa jamii. 

Amesema mradi huo umepangwa  kuwafikia zaidi ya vijana 12,261 ambapo miongoni mwao wanawake ni 6,130; wanaume 4,905 na makundi maalumu ni 1,226 katika awamu ya kwanza inayohusisha Mikoa ya Geita, Kagera, Tabora na Tanga. 

"Tunapozindua mradi huu hatuna budi kuwashukuru Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na Mheshimiwa Yoweri Kaguta Museveni, Rais wa Jamhuri ya Uganda.

Viongozi wetu hawa kwa nia yao  ya dhati na moyo wa uzalendo wameuendeleza na  kuusimamia kikamilifu mradi huu wa EACOP ambao umefikia asilimia 65, tumefikia hapa sababu ya msukumo wao wa kutekeleza mradi huu " Amesema Dkt. Biteko

Ameeleza kuwa  tangu kuanza kwa mradi wa EACOP  mwaka 2022 hadi sasa,  jumla ya Watanzania 9,194 wamepata nafasi za kufanya kazi ndani ya mradi na hivyo kuwa fursa kwao ya kujipatia kipato, mwaka 2024 kampuni ilitoa mafunzo maalumu kwa Vijana 170 na kuwapatia kazi kwenye mradi, Vijana wengine 110 wapo katika masomo na wanatarajiwa kujumlishwa  pia katika Mradi huo pamoja na kutoa ufadhili wa Vijana 238 katika vyuo mbalimbali nchini. 

Amesema wananchi wanaopitiwa na miradi wanayo haki ya kunufaika na miradi lakini wana wajibu wa kulinda miundombinu ya mradi na kuufanya kuwa ni sehemu yao kwani unachangia pia kubadilisha maisha ya wananchi.

 Pia, Dkt. Biteko ameipongeza kampuni ya EACOP  na Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania ( TPDC) kwa kusimamia kwa ufanisi mradi huo huku akisisitiza kuwa, ili wananchi waone mradi huo ni sehemu yao lazima waone faida zake  hivyo miradi kama ya YEE inawapa chachu wananchi kulinda miundombinu ya EACOP kwa  wivu mkubwa.

Katika hatua nyingine, Dkt. Biteko amesisitiza kuwa, kampuni mbalimbali zinazotekeleza miradi kuhakikisha kuwa hawaweki mkazo  kwenye kuongeza ujuzi tu kwa wananchi bali wanawapatia mitaji ili waweze kufanya vizuri zaidi.

Aidha, amewaasa vijana kuchangamkia fursa zinazotokea kwenye miradi, wajitume, wawe waaminifu pale wanapopata fursa na kueleza kuwa Serikali itaendelea kuwatengenezea fursa  ili wajikwamue kiuchumi na kuleta maendeleo nchini.

Kwa upande wake, Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana na Ajira), Mhe. Patrobas Katambi amesema Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan ametengeneza mipango mikakati ya kuhakikisha vijana wanapewa fursa za ajira na mitaji kwenye maeneo mbalimbali ambapo mpango wa YEE ni kielelezo cha matokeo ya mipango hiyo.

Ameeleza kuwa, kumekuwa na programu mbalimbali ikiwemo ya uwezeshaji wananchi kiuchumi ambapo kupitia programu hiyo zaidi ya shilingi trilioni tatu zilitolewa kwa Watanzania  takriban milioni 24 ikiwemo Wanawake,  Vijana na Makundi maalum kwa lengo la kuwawezesha kujikwamua kiuchumi

Mkuu wa Mkoa Geita, Martine Shigella akizungumza kwa niaba ya Wakuu wa Mikoa inayopitiwa na mradi wa EACOP amesema kuwa mradi wa EACOP ni miongoni mwa miradi mikubwa ambayo wananchi wa Geita wamenufaika nayo kwa namna mbalimbali ikiwemo ajira za moja kwa moja na muda na mfupi pamoja na  mnyororo wa thamani kupitia biashara ya vyakula, mbogamboga, matunda.

Amesema Mpango wa  uwezeshaji wa vijana kiuchumi ni matunda ya Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan ambaye ameendelea kuhakikisha vijana wanapata elimu na ujuzi hivyo mpango wa YEE unaongeza chachu hiyo ya utoaji elimu na ujuzi kwa wananchi wakiwemo vijana.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Mhandisi Felchesmi Mramba amesema utekelezaji wa mradi wa EACOP wenye urefu wa km 1443 ni moja ya miradi 17 inayotekelezwa na Wizara ya Nishati ikiwemo mradi wa Julius Nyerere ( MW 2,115) ambao umekamilika, miradi ya umeme ya Ruhudji,  Rumakali na Malagarasi pamoja miradi mingine ya utafutaji na uzalishaji wa mafuta na gesi asilia ukiwemo wa Eyasi Wembere.

Katika mradi wa EACOP amesema Serikali imechangia shilingi trilioni 1.12  ambazo ni hisa za Tanzania na kuna kampuni za kitanzania 200 ambazo zinafanya kazi mbalimbali katika mradi ambazo zitalipwa jumla ya shilingi trilioni 1.325 ikiwa ni moja ya matunda ya uwepo wa mradi huo nchini.

Akieleza sababu za kufanyika.kwa uzinduzi wa mradi wa YEE wiiayani Bukombe amesema kuwa Bukombe  kuna  kituo kikubwa zaidi cha kusukuma mafuta yatakayotoka nchini Uganda hadi Chongoleani Tanga,   kuna kambi kubwa ya mradi wa EACOP na pia kilometa 20 za bomba hilo la mafuta zinapita katika eneo la Bukombe.

Aidha, Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania ( TPDC), Mussa Makame  ameeleza kuwa, TPDC imeendelea kushirikiana na kampuni ya EACOP kuhakikisha kuwa mahitaji ya wananchi yanabainishwa na kuzingatiwa katika utekelezaji wa mpango wa Uwajibikaji kwa Jamii (CSR).

Ameeleza kuwa mahitaji yaliyoainishwa katika mradi wa YEE yaliandaliwa kwa kushirikiana na Serikali za Mitaa kwa ngazi ya vijiji, Kata na Halmashauri zilizopo maeneo linapopita bomba la mafuta. 

Awali  Clare Haule - Meneja wa Uwekezaji na Uwajibikaji kwa Jamii katika kampuni ya EACOP alisema mradi wa YEE umeanzishwa kwa kutambua kwamba zaidi ya asilimia 65 ya idadi ya watu wa Tanzania ni vijana chini ya umri wa miaka 35. Hata hivyo, vijana wengi hasa katika maeneo ya vijijini wanakumbana na vikwazo vingi kama vile ukosefu wa ajira, ukosefu wa mafunzo ya ufundi stadi , na ugumu wa kupata mitaji ya kuanzisha au kukuza biashara.

Alisema awamu ya kwanza ya Mradi wa YEE  utawawezesha kiuchumi vijana katika mikoa ya Geita, Kgera,Tabora, na Tanga na  mikoa inayobaki itanufaika katika awamu ya pili ambayo ni Singida, Shinyanga, Dodoma na Manyara ambapo vijana watapewa ujuzi  unaolingana na mahitaji ya soko, kuboresha upatikanaji wa huduma za kifedha, na kuondoa vikwazo vya ujasiriamali na ajira binafsi.

Aliongeza kuwa, Mradi wa YEE ni sehemu ya Sera ya Uendelevu ya EACOP, chini ya nguzo ya Vizazi Vijavyo, inayolenga kujenga uwezo wa vijana na kuongeza upatikanaji wa fursa za kiuchumi katika jamii zinazoguswa na mradi.

 


📌RC Kunenge aipongeza REA kwa kuhamasisha matumizi nishati safi

📌Mifumo ya umeme jua kuchochea upatikanaji wa umeme kwa asilimia 100 ifikapo mwaka 2030


Wakala wa Nishati Vijijini (REA), imetoa jumla ya Majiko Banifu 10,650 Mkoani Pwani ikiwa ni mwendelezo wa jitihada za Serikali za kuhakikisha  kila mwananchi anatumia Nishati Safi ya kupikia nchini. 

Akizungumza leo tarehe 18 Agosti, 2025 ofisini kwa Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Meneja wa Teknolojia za Nishati kutoka REA, Mha. Michael Kyessi amesema mradi huo unalenga kuuza na kusambaza Majiko Banifu kwa bei ya ruzuku ambapo mwananchi atachangia asilimia ishirini (20%) za gharama ya jiko huku asilimia themanini (80%) zikitolewa na Serikali. 

“Mwananchi wa kawaida atachangia 20% tu za gharama za jiko ambapo bei ya jiko ni 56,000 na mwananchi atagharamika kuchangia shilingi 11,200 tu baada ya ruzuku kutolewa na Serikali” amesema Mha. Kyessi. 

Sambamba na hilo Mha. Kyessi amebainisha thamani ya mradi huo kwa ujumla ni milioni 596,400,00 ambapo Serikali kupitia REA imetoa ruzuku ya shilingi milioni 477,120,00 ambayo ni sawa na asilimia themanini. 

Katika hatua nyingine, REA inatekeleza lengo la Serikali ya Tanzania kufikia mpango wa Umoja wa Mataifa wa "Nishati Endelevu kwa Wote" (SE4ALL) wa upatikanaji wa nishati 

kwa asilimia 100 ifikapo mwaka 2030. Mradi huu utatumia nishati Jadidifu ili kuweza kufikia wananchi wa maeneo ya visiwani na utekelezaji wake ni kwa kupitia mradi wa Ufadhili unaotegemea Matokeo (RBF) kupitia Benki ya Dunia. 

"Serikali ya Tanzania kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umetenga fedha kwa ajili ya utekelezaji wa mradi wa kufunga mifumo ya umeme jua maeneo ya visiwani kwa 

kutoa ruzuku kwa bei ya mwisho ya mtumiaji wa mfumo wa Umeme Jua ili kufanikisha upatikanaji wa umeme katika maeneo hayo yaliyo mbali na Gridi ya Taifa, " Amesema Mha. Kyessi. 

Mha. Kyessi amesema katika Mkoa wa Pwani mradi wa umeme jua unategemea kuhudumia visiwa 13 na jumla ya watoa huduma wawili (2) wanategemea kuhudumia visiwa hivyo kupeleka jumla ya mifumo 2,243 ndani ya kipindi cha miaka miwili (2) na gharama za mradi kwa mkoa wa Pwani ni shilingi  bilioni 1.372 ambapo ruzuku ni shilingi milioni 935.7 sawa na asilimia 69 ya gharama zote ya mradi na shilingi milioni 436.6 ni fedha toka kwa wanufaika. 

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhe. Abubakar Kunenge ameipongeza REA kwa mkakati wa kuendelea kuongeza matumizi ya Nishati safi na kuondoa kero kwa wananchi kuhusu matumizi ya kuni na mkaa ambayo ni hatarishi kwa afya zao. 

Mradi huo utatekelezwa kwa muda wa miezi 15 katika mkoa wa Pwani na jumla ya Majiko Banifu 10,650 yatasambazwa kwa wananchi.

 



Wataalam wa wanaoandaa na kusimamia Bajeti ya Serikali wameagizwa kutumia mafunzo ya Mfumo ulioboreshwa wa Uandaaji na Usimamizi wa Bajeti (CBMS), kuboresha utendaji kazi katika usimamizi wa uandaaji na utekelezaji wa Bajeti ya Serikali.

Agizo hilo limetolewa jijini Dodoma na Kamshina wa Bajeti, Wizara ya Fedha, Bw. Meshack Anyingisye wakati akifungua mafunzo ya Mfumo wa CBMS ulioboreshwa na baadae kufanya Tathmini ya Utekelezaji wa Bajeti ya Serikali ya Mwaka 2024/25, Maandalizi ya Bajeti ya Serikali ya Mwaka 2025/26 na kupata maoni ya kuboresha mchakato wa maandalizi ya Mwongozo wa Maandalizi ya Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2026/27.

Bw. Anyingisye alisema wataalam hao ni watu muhimu sana katika uandaaji na utekelezaji wa bajeti ya Serikali hivyo watumie mafunzo hayo kusimamia bajeti na kushauri Idara tumizi namna bora ya kutekeleza bajeti zao pamoja na kuboresha usimamzi wa bajeti ya Serikali.

“Usimamizi wa bajeti sio jukumu la Wizara ya Fedha tu, ni jukumu la kila mmoja wetu hivyo ni vema tukatekeleza majukumu yetu kikamilifu katika kushauri na kuchakata takwimu mbalimbali kutoka katika bajeti zetu”, alisisitiza Bw. Anyingisye.

Aidha, alisisitiza kuwa ushiriki wa watumishi hao katika kikao hicho unaashiria kujitolea kwa pamoja katika kuboresha utekelezaji na usimamizi wa bajeti ya Serikali, kuongeza ufanisi katika mchakato wa bajeti na kuhakikisha vipaumbele vya Serikali vinatekelezwa ipasavyo.

Awali akizungumzia mafunzo hayo, Kamishna Msaidizi wa Bajeti anayeshughulikia uchambuzi na mbinu za kibajeti Wizara ya Fedha, Bw. Fundi Makama, alisema mafunzo hayo yamehusisha wadau kutoka Wizara, Idara zinazojitegemea, Wakala za Serikali, Ofisi za Wakuu wa Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa.

Alisema mafunzo hayo ya siku tano (5) yatatolewa kwa awamu mbili ambapo awamu ya kwanza itahusu mafunzo ya Mfumo wa Uandaaji na Usimamizi wa Bajeti (CBMS) ulioboreshwa na awamu ya pili itajikita kwenye Tathmini ya Uandaaji wa Bajeti ya 2025/26 na tathmini ya utekelezaji wa Bajeti ya 2024/25. 

Bw. Makama alibainisha kuwa mafunzo hayo yatawezesha kupata maoni ya mchakato wa maandalizi ya Mwongozo wa uandaaji wa Mpango na Bajeti ambao unatarajiwa kuanza hivi karibuni.

Kwa upande wake Bw. Deodatus Kayango, Katibu Tawala Msaidizi wa Mipango na Uratibu kutoka Mkoa wa Geita, ambaye ni mshiriki wa mafunzo hayo alisema mafunzo hayo yatawezesha kufanya mipango yao kwa kutumia mifumo hali ambayo inatarahisisha upangaji, utekelezaji na tathmini ya mipango hiyo.

Kikao kazi cha wataalam wa Wizara, Idara zinazojitegemea, Wakala za Serikali na Sekretarieti za Mikoa ni jukwaa muhimu la kutafakari na kujadili kuhusu mafanikio na changamoto zilizojitokeza wakati wa utekelezaji wa bajeti ya mwaka 2024/25, uandaaji wa bajeti ya 2025/26 na kupata maoni ya maandalizi ya  Mwongozo wa uandaaji wa  Mpango na Bajeti ya Serikali wa mwaka 2026/27 ili kubaini maeneo ya kuboresha na kuweka mikakati itakayosaidia kuboresha uandaaji wa mipango na bajeti kwa mwaka 2026/27




KADA ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Hamadi Shamisi Hamadi leo amechukua fomu ya kuwania Udiwani Kata ya Msambweni Jijini Tanga huku akihaidi kufanya kazi kwa uadilifu.

Hamadi aliyasema hayo leo mara baada ya kuchukua fomu katika Ofisi ya Mtendaji Kata ya Msambweni huku akiwa amesindikizwa na wanachama wa chama hicho wakiwemo wananchi.

Alisema kwamba lengo lake ni kuhakikisha anawatumikia wananchi wa kata hiyo na kuwa kiungo cha maendeleo ya wananchi na hivyo kuchochea ukuaji wa maendeleo.

“Nawaambia tutafanya kazi kwa dhati na kutanguliza uaminifu na uadilifu kuhakikisha wananchi wanapata maendeleo na shahidi ni Baba yangu mzazi ambaye ananisindikiza hapa”Alisema

Awali akizungumza Mwenyekiti wa CCM kata ya Msambweni alisema kwamba hicho ni kishindo cha kwanza ila Agosti 28 wanaanza kampeni zao na wanafungua kwenye tawi la Msambweni B eneo la Komesho watakuwa na Mbunge wa Tanga Jijini kampeni za wilaya zitafunguliwa hapo.

Alisema Agosti 29 utakuwa uzinduzi wa kampeni wa Diwani wa Kata ya Msambweni na zitazinduliwa Mtaa wa Madina eneo la Mabanda ya Papa huku akiwataka wananchi kujitokeza kwa wingi katika uzinduzi huo.

Naye kwa upande wake Mwenyekiti wa zamani wa Mtaa wa Madina Godfrey Mazimu alisema kwamba amefurahi kuona wanachama wenzake na wananchi wa Msambweni huku akiwataka kuendelea kuunganisha nguvu za pamoja mpaka mwisho na wasiachane.