Mashabiki   wa Timu za Simba na Yanga ambao ni watumishi wa Chuo cha Maendeleo ya Jamii Tengeru(TICD), wamecheza mechi ya kirafiki katika juhudi za kuendelea kudumisha mahusiano na ushirikiano katika maeneo ya kazi.

Akizungumza katika bonanza hilo Mgeni rasmi Kaimu Naibu Mkuu wa chuo cha Maendeleo ya Jamii Tengeru (TICD),anayeshughulikia Mipango na Utawala bi.Janeth Zemba  alisema kuwa lengo hasa la bonanza hilo ni kuendelea kutangaza taasisi hiyo kupitia michezo.

"Bonanza hili ni la tatu kufanyika na leo hakuna aliyepatikana mshindi kwa kuwa sio mashabiki ya Simba wala Yanga aliyemfunga  mwenzake hivyo tutaendelea kushirikiana katika  michezo kwa kuwa inajenga mahusiano mema,ni furaha amani na pia inatuweka vizuri kiafya kupitia mazoezi tunayoyafanya mwaka mzima hivyo  tutaendelea kuboresha na kushirikiana  pia na wadau mbali mbali ".Alisema bi.Zemba

Aidha alitumia fursa hiyo kuwaasa wadau mbali mbali kuendelea kudumisha mshikamo na ushirikiano,na kuendelea kuitangaza taasisi hiyo kupitia sekta hiyo ya burudani ambayo inaleta makada mbali mbali.

Kwa upande wake Mkuu wa chuo hicho Daktari Bakari George alisema kuwa bonanza hilo  linaleta watumishi na jamii ya maendeleo ya tengeru pamoja na ni mfulululizo wa bonanza ambalo linawakutuanisha pia na watu maarufu ambao wamewahi kutumikia vilabu vikubwa nchini vya Simba na Yanga.

"Mwaka Jana katika bonanza kama hili tuliwashirikisha wasemaji wa timu hizi mbili na Leo pia Mwaka huu tuna wachezaji ambao ni Mrisho Khalifan Ngassa ambaye amewahi kucheza katika klabu ya Yanga na Daniel Mrwanda ambaye aliwahi kucheza katika timu ya Wekendu wa Msimbazi Simba na timu ya Taifa pia "Alisema dkt.Bakari 

Dkt.Bakari alisema kuwa nia kubwa ni hamasa ya michezo na vilevile kuitangaza taaisisi hiyo ya TICD,kupitia sekta ya michezo ambayo huleta watu wengi pamoja.

Hata hivyo alisema kuwa bonanza hilo ni kichocheo kikubwa kwa watumishi kuendelea kufanya mazoezi mwaka mzima na kulete tija katika maeneo ya kazi.

Bonanza hilo limekutanisha mashabiki wa timu ya Simba na Yanga kutoka katika viunga wa mkoa wa Arusha,ambapo limekuwa likijipatia umaarufu mwaka hadi mwaka ambapo lengo ni kulipeleka katika maeneo mengine nchini.

Mechi ya utangulizi ilikutanisha timu ya Wanafunzi wa chuo Cha Maendeleo ya Jamii Tengeru (TICD) ambao ni mashabiki wa Simba na Yanga,ambapo matokeo yalikuwa ni 1-1 mchezo uliofanyika katika uwanja wa chuo Cha Mifugo Tengeru.













Mwenge wa UhuruWanafunzi wa zaidi 80  wanaosoma shule ya sekondari Malula kata ya Malula Wilayani Arumeru wameondokana na adha  ya mabweni baada ya Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF)kujenga bweni lenye thamani ya milioni 168.4

Uzunduzi wa bweni hilo ulifanywa na  Kiongozi wa  mbio za mwenge Kitaifa, Ismail AliUssi mara baada ya kukagua bweni hilo lenye vyumba 20 vitanda 40 na kupongeza juhudi za serikali katika kuinua sekta ya elimu

Alisema mradi huo ni wa kimkakati unaopelekea wanafunzi kupata elimu bora , ndio maana serikali imeboresha sekta ya miundombinu ya elimu ili kuhakikisha ufaulu wa wanafunzi unaongezeka zaidi. 

"Mradi huu umetekelezwa kwa ufasaha chini ya Uongozi wa Rais Samia Hassan Suluhu hivyo alimpongeza Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Mwinyi Ahmed Mwinyi na viongozi wengine kwa ujenzi wa shule hiyo katika kuhakikisha kiwango cha elimu kinaongezeka"

Alisisitiza wananchi kujitokeza kushiriki uchaguzi mkuu kwa amani na utulivu hivyo na kuwapongeza wanafunzi kupitia klabu ya Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa(Takukuru) kuhakikisha wanatekeleza uadilifu na kushika yale yote wanayoelekezwa ili kupinga rushwa ikiwemo walimu kusimamia wanafunzi hao kupata elimu na kuendelea na mapambano dhidi ya rushwa 

Akisoma taarifa ya mradi huo Mwenyekiti wa Kamati inayosimamia miradi ya Tasaf, Onesmo Nanyaro alisema mradi huo utasaidia wanafunzi kusoma kwa bidii ikiwemo kuondokana na adha ya ukosefu wa malazi 

Awali akipokea mwenge wa uhuru kutoka Mkoani Kilimanjaro , Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Kenan Kihongosi alisema mwenge huo utazindua miradi 54 yenye thamani ya sh, bilioni 30.3 katika halmashauri saba 

Mwenge huo uliwasili jana mkoani Arusha na kukabithiwa eneo la King'ori Kibaoni  Wilayani Arumeru ukitokea Mkoani Kilimanjaro ambapo utapitia  miradi 54 kisekta yenye thamani ya sh, bilioni 30.3 mkoani hapa.












Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Ismail Ali Ussu ameipongeza Serikali ya awamu ya sita chini ya Mhe.Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan Serikali, kupitia Wakala wa Barabara za  Mijini na Vijijini (TARURA), kwa kutoa fedha nyingi za utekelezaji wa miradi ya  miundo ya barabara nchini, licha ya kurahisisha usafiri imechochea kasi ya maendeleo na kukuza uchumi katika maeneo mengi.

Akizungumza wakati akiweka Jiwe la Msingi mradi wa ujenzi wa Daraja la zege na chuma barabara ya Usa River - Maji ya Chai halmashauri ya Meru, daraja lililojengwa na  kwa gharama ya shilingi milioni 499.8,ameipongeza TARURA Arumeru kwa kazi nzuri waliyoifanya inayoakisi dhamira njema ya Mhe.Rais.

Kupitia mradi huo, Kiongozi huyo amesema kuwa, Serikali ya awamu ya sita chini ya uongozi mahiri wa Dkt.Samia Suluhu Hassan, imefanya kazi nzuri katika sekta zote ikiwemo miundo mbinu ya barabara na wilaya ya Arumeru ni moja ya eneo lililonufaika sana kwa kuzingatia miradi mingi iliyotekelezwa kwa kipindi cha awamu ya sita

"Nimeishuhudia kazi nzuri ya ujenzi wa daraja hili la mawe na chuma, daraja ambalo limejengwa kwa kuzingatia viwango vya ubora vinavyoenda na thamani ya fedha zilizotolewa na tayari limeanza kuwahudumia wananchi wa maeneo haya, ninaipongeza sana TARURA kwa kazi hii nzuri". Amesema

Ameongeza kuwa, kupitia mradi huu,  Mwenge wa Uhuru umeleta matumaini mapya kwa wananchi wa halmasahuri ya Meru, wananchi wamepata furaha na amani, kwa kuwa timu imejiridhisha daraja hilo limejengwa kwa ubora wa hali ya juu.











Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL), Bw. Moremi Marwa, Julai 4, 2025, amefanya ziara maalum katika Banda la TTCL kwenye Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa (SabaSaba), yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam.

Katika ziara hiyo, Bw. Marwa alipokelewa na wataalamu waandamizi wa TTCL, ambao walimtembeza katika maeneo mbalimbali ya banda hilo na kumweleza kwa kina kuhusu huduma na teknolojia zinazotolewa na Shirika hilo.

Miongoni mwa huduma zilizowasilishwa ni pamoja na Faiba Mlangoni, inayowezesha upatikanaji wa intaneti ya kasi moja kwa moja majumbani na maofisini, ikiwa ni sehemu ya dhamira ya TTCL kuhakikisha kila Mtanzania anapata huduma bora za mawasiliano kwa gharama nafuu.

Pia alielezwa kuhusu Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano (NICTBB), ambao tayari umesambazwa katika mikoa yote 26 na wilaya 112 kati ya 139 nchini. Mkongo huo umeunganisha Tanzania na nchi jirani na kuchochea matumizi ya TEHAMA katika utoaji wa huduma kwa wananchi.

Huduma nyingine alizotembelea ni pamoja na Kituo cha Taifa cha Kuhifadhi Taarifa Kimtandao (NIDC), chenye uwezo wa kisasa wa kuhifadhi na kulinda taarifa muhimu za taasisi na kampuni mbalimbali, na hivyo kuchangia ukuaji wa uchumi wa kidijitali nchini.

Aidha, Mkurugenzi Mkuu alifahamishwa kuhusu huduma ya Call Center ya TTCL inayosaidia mashirika kuwasiliana kitaalamu na wateja wao, pamoja na WiFi ya Umma (Public WiFi) inayowawezesha wananchi kupata huduma ya intaneti kwa urahisi katika maeneo ya wazi.

Katika kuendeleza ushirikiano wa kimkakati, Bw. Marwa pia alitembelea mabanda ya taasisi mbalimbali rafiki, ikiwemo Shirika la Posta Tanzania (TPC), Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF), Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo (SIDO), Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA), pamoja na Banda la Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari.

Katika kila banda, alielezwa kuhusu majukumu na huduma zinazotolewa, huku akisisitiza umuhimu wa kuimarisha ushirikiano ili kufanikisha malengo ya pamoja ya kidijitali na kiuchumi kwa maendeleo ya Taifa. 


















NA EMMANUEL MBATILO, PWANI

HIFADHI ya Mazingira Asilia ya Uluguru kutoka mkoani Morogoro imefanya ziara ya mafunzo katika Hifadhi ya Mazingira Asilia ya Pugu Kazimzumbwi, kwa lengo la kuwajengea uwezo wadau wa utalii kutoka mkoa huo, sambamba na kuimarisha ushirikiano katika uhifadhi wa mazingira na kukuza utalii wa ikolojia.
Na Mwandishi Wetu - Dar es Salaam.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Ridhiwani Kikwete ametoa wito kwa vijana kuchangamkia fursa mbalimbali zilizopo ikiwemo mikopo na mifuko mbalimbali ya uwezeshaji Wananchi kiuchumi.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Ushindani (FCC) Tanzania bi.Hadija Juma Ngasongwa amesema wawekezaji wa ndani ya nchi wanasimamiwa na sheria madhubuti zinazosimamia uwekezaji nchini, kusaidia kuimarisha biashara nchini, kulinda

 


Wananchi wametakiwa kuwa na uelewa kuhusu Sera za Kodi  zinazoandaliwa na Wizara ya Fedha kwa lengo la kumfanya mwananchi kulipa kodi kwa hiari ili kuisaidia Serikali kutoa huduma bora na endelevu katika sekta mbalimbali ikiwemo ya afya, maji, barabara, nishati na kilimo.

Hayo yamesemwa na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Bi. Jenifa Christian Omolo alipotembelea Banda la Wizara ya Fedha na mabanda mengine kwenye Maonesho ya 49 ya Kimataifa ya Biashara Dar es Salaam (Sabasaba) ambayo yameanza  tarehe 28 Juni na kutarajiwa kuhitimishwa Julai 13 mwaka huu.

Alisema kuwa Bunge limepitisha Bajeti Kuu ya Serikali ya Kiasi cha shilingi trilioni 56.49 ambayo inalenga pamoja na mambo mengine kutekeleza miradi yenye faida ya moja kwa moja kwa mwananchi kama barabara, nishati, maji na kilimo.

Bi. Omolo alisema kuwa jukumu la mwananchi katika kufanikisha hilo ni pamoja na kulipa kodi kwa hiari kwa mazingira rafiki ambayo yanatokana na Sera nzuri za kodi ambazo zimeandaliwa  na Wizara ya Fedha. 

Ametoa rai kwa wananchi wanaotembelea katika Maonesho hayo kufika Banda la Wizara ya Fedha ili kukutana na wataalamu ambao watawapa elimu ya Sera ya Kodi na faida zake kwa jamii.

Bi. Omolo amewahakikishia wananchi kupata huduma bora kutoka Serikalini kupitia Bajeti iliyopitishwa na Bunge hivi karibuni kwa kuwa lengo la Serikali ni kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora na kwa gharama nafuu.

Aidha, alisema kuwa ndani ya Banda la Wizara ya Fedha inatolewa elimu ya huduma ndogo za fedha kwa lengo la kuhakikisha wananchi wanakuwa na uelewa wa masuala ya fedha ili kuondokana na kuchukua mikopo isiyo na tija. 

Alisema pia kuwa Banda la Wizara ya Fedha linashirikisha Vyuo vikuu vilivyo chini ya Wizara ambavyo vinatoa elimu kuhusu kozi mbalimbali ambapo alivitaja vyuo hivyo kuwa ni pamoja na, Chuo cha Mipango ya Maendeleo Vijijini (IRDP), Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) na Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA). 

Aidha alisema kuwa wataalamu wengine ni kutoka Idara na Vitengo vya Wizara hiyo na Taasisi zake ikiwa ni pamoja na Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu (NBAA), Mfuko wa Dhamana na Uwekezaji Tanzania (UTT AMIS), Mfuko wa Self Microfinance, Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana (CMSA) na Soko la Bidhaa Tanzania (TMX).

Taasisi nyingine ni pamoja na Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE), Baraza la Masoko ya Mitaji (CMT), Benki ya Maendeleo TIB na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), Hazina SACCOS, Mamlaka ya Udhibiti wa Manunuzi ya Umma (PPRA), Mamlaka ya Rufaa za Zabuni za Umma (PPAA) na Wakala wa Huduma ya Ununuzi Serikalini (GPSA).