Angela Msimbira TAMISEMI


Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Majaliwa Majaliwa ameiagiza Ofisi ya Rais- TAMISEMI kupitia Wakurugenzi wa Halmashauri kuhakikisha  wanatekeleza Mpango wa Maendeleo ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi katika Halmashauri zao.


Pia Mhe. Majaliwa ameelekeza Wakurugenzi hao kutenga maeneo ya uwekezaji ili kuwawezesha wananchi kufanya kazi zao za kilimo, ufugaji na ujenzi wa viwanda katika mazingira bora na yanayotambulika.


Akizundua Mipango ya kuendeleza sekta ya Kilimo ya Wilaya uliofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Chuo cha Mipango Jijini Dodoma leo tarehe 3 Machi, 2022 Mhe. Majaliwa amesema utengaji wa maeneo ni kuhimu ili kila mwekezaji anapohitaji eneo ka kuwekeza apate kwa haraka bila urasimu.


Amesema  yapo maeneo ambayo ni makubwa lakini bado yanamilikiwa na watu, Serikali imeshafanya mapitio ya kuyatambua maeneo hayo, hivyo ameziagiza Halmashauri zote nchini kuhakikisha wanasimamia maeneo.


Aidha Waziri Mkuu ameiagiza TAMISEMI  kuandaa utekelezaji wa mikakati madhubuti wa kusimamia utendaji kazi wa maafisa ugani ili kuongeza uzalishaji wa tija katika maeneo ya kilimo.


‘Naafisa ugani wasimamiwe kimalifu na wawezeshee vitendea kazi kama usafiri nk kwa ajili ya kutekeleza majukumu yao.


Amewataka wakurugenzi wa Halmashauri kuhakikisha wanawapangia kazi maafisa ugani kulingana na fani walizosomea ili kuleta tija na weledi katika utekelezaji wa majukumu yao kulingana na Jiografia ya maeneo yao.


Mhe. Majaliwa ameziagiza Halmashauri zote nchini kuhakikisha wanatenga fedha kutoka katika mapato ya ndani  ili kutekeleza mpango wa maendeleo ya kilimo , mifugo na  uvuvi wa Wilaya  na fedha hizo zitoke kwenye tozo za maeneo hayo ili kutumika kuendeleza mpango huo.


Aidha amewaagiza Wakuu wa Mikoa na Makatibu Tawala wa Mikoa na Wakurugenzi watendaji wa Halmashauri kuhakikisha wanaongeza usimamizi wa fedha na rasilimali zilizopo kwa kujenga uwezo wa kusimamia utekelezaji wa miradi katika ngazi zilizopo na kubuni vyanzo vingine vya kupata fedha ili kuendeleza miradi ya kilimo katika maeneo yao


Naye,Waziri wa Nchi  Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Innocent Bashungwa amemuelekeza Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-TAMISEMI kuziagiza  Halmashauri zote nchini  kuleta taarifa ya maeneo ambayo wametenga kwa ajili ya uwekezaji.

Share To:

Post A Comment: