Waziri wa Nishati January Makamba, (kulia) akizungumza na Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia kwa upande wa Tanzania, Mara Warwick, (hawapo pichani) wakati wa kikao cha kujadili maendeleo ya miradi ya sekta ya Nishati, kilichofanyika mkoani Dar Es Salaam, Machi 28, 2022.

Waziri wa Nishati January Makamba, (katikati), Kaimu Katibu Mkuu, Wizara ya Nishati Kheri Mahimbali (wa tatu kulia) na Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia kwa upande wa Tanzania, Mara Warwick ,(wa pili kushoto) wakati wakizungumza wakati wa kikao cha kujadili maendeleo ya miradi ya sekta ya Nishati, kilichofanyika mkoani Dar Es Salaam, Machi 28, 2022.

Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Seif Said,( kulia) na Mkurugenzi wa Huduma za Ufundi wa Wakala wa Nishati Vijijini( REA), Mhandisi Jones Olotu, wakiwa katika kikao cha kujadili maendeleo ya miradi ya sekta ya Nishati, kilichofanyika mkoani Dar Es Salaam, Machi 28, 2022.

Kaimu Katibu Mkuu, Wizara ya Nishati Kheri Mahimbali (wa pili kushoto) na Kamishna Msaidizi Maendeleo ya Umeme Wizara ya Nishati, Mhandisi Styden Rwebangira (kushoto) wakiwa katika kikao cha kujadili maendeleo ya miradi ya sekta ya Nishati, kilichofanyika mkoani Dar Es Salaam, Machi 28, 2022.
Waziri wa Nishati January Makamba, (katikati) akizungumza na ujumbe kutoka Benki ya Dunia, Viongozi waandamizi kutoka Wizara ya Nishati, Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) wakati wa kikao cha kujadili maendeleo ya miradi ya sekta ya Nishati nchini, kilichofanyika mkoani Dar Es Salaam, Machi 28, 2022.

Na Zuena Msuya DSM,

Waziri wa Nishati January Makamba amekuta na ujumbe wa benki ya dunia ukiongozwa na Mkurugenzi Mkazi wa benki hiyo kwa upande wa Tanzania, Mara Warwick, na kuzungumzia mambo mbalimbali kubwa likiwa ni uendelezaji wa Sekta Nishati ikiwemo masuala ya umeme na gesi.

Katika mazungumzo hayo, Makamba ameishukuru benki hiyo kwa ushirikiano wake na Serikali ya Tanzania pia kuwezesha utekelezaji wa miradi ya Maendeleo nchini ukiwemo ule wa kuinganisha Tanzania na Zambia (TAZA).

Mazungumzo hayo yamefanyika katika ofisi za wizara hiyo zilizopo mkoani Dar Es Salaam, Machi 28, 2022, pamoja na mambo mengine mazungumzo hayo yamelenga zaidi kuimarisha ushirikiano kati ya benki hiyo na Serikali ya Tanzania katika kuendeleza miradi mbalimbali ya maendeleo.

“Serikali ya Tanzania inaishukuru Benki ya Dunia kwa kuwezesha miradi ya nishati hapa nchini, tunawaahidi tutaendelea kushirikiana na katika nyanja mbalimbali kwa kuwa tumeona matokeo chanja katika miradi ambapo benki hiyo imeiunga mkono hasa katika Sekta ya Nishati,” alisema Makamba.

Mkutano huo pia umehudhuriwa na Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Nishati, Kheri Mahimbali, Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Seif Said na Mwakilishi wa Mkurugenzi Mtendaji Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Anitha Ishengoma pamoja na Viongozi wengine waandamizi kutoka Wizarani, REA na TANESCO.

Katika kikao hicho wamejadili mradi wa Usambazaji wa umeme vijiji, njia kuu za kusafirisha umeme pamoja masuala ya gesi.

Kwa upande wake Mkurugenzi Warwick amemueleza Waziri wa Nishati kuwa wataendelea kushirikiana na serikali ya Tanzania kwa kuinguka mkono sekta ya Nishati, ili kutanua wigo wa ukuaji wa maendeleo ya sekta hiyo.

Pia watawajengea uwezo wataalam wa kada hiyo ili kuweza kuongeza tija na ufanisi katika sekta hiyo.
Share To:

Post A Comment: