Mkuu wa Mkoa Manyara Makongoro Nyerere (kulia) akimpongeza Mkuu wa Wilaya ya Hanang Janeth Mayanja kwa kazi nzuri ya kuhamasisha maendeleo kwenye wilaya hiyo.
Viongozi wakiwa meza kuu wakati wa maadhimisho hayo ya wiki ya maendeleo Hanang yaliyofanyika ofisi ya mkuu wa wilaya hiyo. Kutoka kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Hanang, Janeth Mayanja, Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Makongoro Nyerere na Waziri Mkuu Mstaafu wa Awamu ya Tatu, Fredirick Sumaye.
Vifaa vikipokelewa.
Mkuu wa Mkoa Manyara Makongoro Nyerere (kulia) ambaye alikuwa mgeni rasmi katika kilele hicho na mgeni wa Heshima Waziri Mkuu Mstaafu wa Awamu ya Tatu Fredrick Tluway Sumaye wakisaini baada ya kupokea vifaa hivyo.
Ndoo za rangi zilizopokelewa.
Saruji na ndoo za rangi zilizopokelewa.
Sehemu ya saruji iliyopokelewa.
Waendesha boda boda wakiwa wamebeba saruji katika maadhimisho hayo.
Viongozi mbalimbali walioshiriki maadhimisho hayo. kutoka kushoto ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Hanang, Rose Kamili, Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo, Jennifer Omolo. Mkuu wa Wilaya ya Hanang, Janeth Mayanja, Waziri Mkuu Mstaafu wa Awamu ya Tatu Fredrick Tluway Sumaye, Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Hanang, Mathew Dallema na Mbunge wa Jimbo la Hanang, Samuel Hayyuma.


Na Dotto Mwaibale, Hanang


VIFAA vya ujenzi vyenye  thamani zaidi ya  Sh.100,000,000.00 (Milioni mia) vimechangishwa na makundi mbalimbali  wilayani Hanang mkoani Manyara katika kilele cha wiki ya maendeleo.

Mkuu wa Mkoa wa Manyara Makongoro Nyerere  ambaye alikuwa mgeni rasmi katika kilele hicho kilichofanyika katika viwanja vya  ofisi ya wilaya hiyo akizungumza na wananchi wakati akipokea vifaa hivyo alimpongeza mkuu wa wilaya hiyo Janeth Mayanja kwa kazi nzuri aliyoifanya ya kuhamasisha maendeleo wilayani humo.

Vifaa vilivyopokelewa katika kilele hicho ni mbao, mchanga, saruji, Gypsum board, Gypsum Powder,vigae, mbao, misumari  rangi za aina mbalimbali ambavyo vinakwenda kutumika kukarabati miundombinu ya Hospitali ya Tumaini  wilayani Hanang.

Katika maadhimisho hayo mgeni wa Heshima alikuwa ni Waziri Mkuu Mstaafu wa Awamu ya Tatu Fredrick Tluway Sumaye.

Wiki hiyo ya maendeleo wilayani humo iliandaliwa na mkuu wa wilaya hiyo Janeth Mayanja lengo likiwa kutatua kero  mbalimbali  wilayani humo  hasa katika Hospital ya Wilaya ya Hanang.

Katika kuitikia mpango huo mzuri wa maendeleo uliobuniwa na mkuu wa wilaya hiyo wadau mbalimbali walijitokeza kuchangia ikiwemo wafugaji,wakulima,Taasisi za Dini,wafanyabiasha,wajasiriamali, makampuni,Taasisi mbalimbali klabu za mpira mkuu wa wilaya amewashukuru wananchi na wadau wote wa maendeleo kwa kuchangia kwa hiari vifaa hivyo ili kuunga jitihada za Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu.

Share To:

dotto mwaibale

Post A Comment: