Khadija Kalili , Kibaha
Katibu Tawala Mkoa wa Pwani Injinia Mwanasha Tumbo  amesema kuwa serikali inajipanga kujenga mabweni kwenye shule mbalimbali nchini Ii kuweza  kuwasaidia watoto wenye changamoto  waweze kubaki shuleni.

RAS Mwanasha alisema hayo leo alipokuwa  mgeni rasmi katika Kongamano la watu wasioona lililofanyika Mjini Kibaha.

"Niwahakikishie  kuwa serikali iko bega kwa bega na nanyi  ukiwemo fursa za kupata ajira serikalini hivyo nawahimiza wazazi kuto waficha watoto wenye changamoto kwa sababu serikali yetu ya awamu ya sita chini ya Rasi Samia Suluhu Hassan inawajali' alisema RAS Mwanasha.

Aidha alitoa wito  na kuwataka  jamii hiyo ya watu wenye changamoto ya kuona  kuendelea kuchukua tahadhari juu ya ugonjwa wa Uviko 19 na kusisi na kusisitiza  kwamba ugonjwa huo upo na kuwaambia wahamasishane Ili Kila mmoja aweze kupata chanjo.
Wakati huohuo Mkurugenzi wa Kibaha Mjini Injinia Mshamu Munde amewapongeza  watu wenye changamoto ya kuona kuwa wanaongoza kwa uaminifu pindi wanapokopeshwa huku akiwamasisha waendelee kuitumia fursa ya mikopo inayotolewa katika Halmashauri zote nchini kwa makundi matatu ambayo ni  wanawake,vijana na walemavu.

Mkurugenzi Munde alisema kuwa Halmashauri ya Mji Kibaha  wamepanga  mipango jumuishi  kwa kutulia maanani  walemavu  wa viungo  na kuzingatia watu wasioona tutawawekea  vipaumbele  kwani tunatambua  nyie msioona  mna umuhimu mkubwa katika jamii  na mko katika rekodi  ya kundi  la kurejesha  mikopo kwa uaminifu mkubwa.

"Halmashauri zote zinatoa mikopo hii hivyo changamkieni hii fursa Ili muweze kukua kiuchumi"alisema Injinia Munde.

Mwenyekiti wa Chama Cha Wasioona nchini Omar Sultan Mpondela  alisema wako Mkoani  kwenye maadhimisho ya Fimbo Nyeupe  ambayo ni kifaa kisaidizi kwa watu wasioona ambapo lengo kuu ni  kupaza sauti Ili jamii iweze kutambua kuwa watu wasioona ni sawa na watu wengine.

Mpondela alisema kuwa  Kongamano hili limewakutanisha viongozi wa wasioona  kutoka katika mikoa yote  nchini  pia chama hicho  kilianzishwa mwaka 1964.
Share To:

Post A Comment: