MKuu wa Mkoa wa Iringa,  Queen Sendiga amesema hadi kufikia Oktoba 14, 2021 Mkoa huo ulikuwa na jumla ya watu 19,898 waliochanjwa chanjo ya Uviko-19 aina ya Johnson.
 
Idadi hiyo ni sawa na 81.2 ya dozi 24,485 ya chanjo hiyo.
 
Sendiga ameyasema hayo leo Jumamosi Oktoba 16, 2021 ofisini kwake wakati akizungumza na wanahabari kuhusiana na kupokea chanjo mpya ya Sinopharm.

Amesema kuwa 0ktoba 15, 2020 Mkoa wa Iringa umepokea jumla ya dozi 21,734 za chanjo ya Sinopharm kutoka Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais (Tamisemi).

"Asilimia zaidi ya 99 ya wagonjwa ambao sasa hivi wapo katika hospitali yetu ya mkoa ni wale ambao hawajapokea chanjo na ndio wale wanaopata maambukizi , kwa takwimu hizo tunaona ni uthibitisho ulio wazi kwamba unapopata chanjo unajiweka katika nafasi nzuri,” amesema Sendiga.

Sendiga amewashauri wananchi wenye umri wa kuanzia miaka 18 na kuendelea kuchoma chanjo ya Sinopham ambayo itatolewa kwa dozi mbili.

Kwa upande wake mratibu wa chanjo Mkoa wa Iringa, Hans Mapunda amesema wamepokea chanjo ya Sinopharm ambayo inatolewa dozi mbili ukilinganisha na ile ya Johnson.


Share To:

Teddy Kilanga

Post A Comment: