Mganga Mkuu wa Jiji la Tanga (CMO) Dkt Charles Mkombe akizungumza wakati wa semina hiyo |
MGANGA Mkuu wa Jiji la Tanga (CMO) Dkt Charles Mkombe amesema kwa mujibu wa takwimu zao mpaka Septemba 27 mwaka huu walikuwa wamechanga chanjo ya Uviko watu 6000.
Mkombe
aliyasema hayo wakati wa semina elekezi
kwa watumishi wa Afya Jijini Tanga na
waandishi wa Habari kuhusu Ugonjwa wa Covid 19 iliyofanyika Jijini Tanga
Alisema kampeni ya Kitaifa ya kuharakisha utoaji wa
chanjo ya uviko 19 itasaidia kutokana na kama dunia imekumbwa na janga kubwa na
lina madhara makubwa na watu wengi wameungua korona na wengine wamefariki.
Aidha alisema
ugonjwa huo umeleta changamoto ya matumizi ya dawa na vifaa tiba na ya kiuchumi
maana kabla ya Korona watu walikuwa wanafanya biashara vizuri lakini sasa
zimefungwa.
“Madhara ya
Korona ni zaidi ya kiafya imegusa ishu za kijamii na kiuchumi na kumekuwa na
ongezeo la gharama za vitu mbalimbali ikiwemo vifaa vya hospitali gharama
zimepanda mara dufu”Alisema
Alisema
ugonjwa huo umeleta mtikisiko mkubwa kwenye jamii na watu wamekata tamaa wamekuwa ni waoga
kuishi
Awali
akizungumza Afisa Afya wa Mkoa wa Tanga Magoma alisema mkoa huo chanjo ya Uviko
19 ilikuwa inasua walipokea dozi 35000
na walianza rasmi Agosti 3 mwaka huu na ilizinduliwa na Mkuu wa Mkoa huo Adam
Malima ilikuwa ya kusuasua kidogo
kutokana na vituo vilivyofunguliwa kuwa vichache .
Alisema wana
vituo zaidi ya 300 na vituo ambavyo vilikuwa vinatoa huduma ni 33 huku vituo
vitatu kila Halmashauri na baadhi ya maeneo mengine kutoka kituo hadi wananchi
walipo inabidi watembee umbali mrefu au wakalale huko karibu na vituo vya
jiriani.
“Lakini pia
kuchelewa kufikia lengo la uchanjaji na tuna lengo la kutazama mabadiliko
walizopewa kumaliza kwenye muda uliowekwa”Alisema
Hata hivyo
alisema sababu kubwa ni vituo kuwa mbalimbali na wananchi Lakini suala hilo
limefanyiwa kazi na halmashauri hivi sasa zimefungua kliniki za mkoba lakini
vituo vinavyotoa bila kujali vya serikali,vya umma au madhehebu ya dini
vitakuwa vinatoa chanjo na elimu inaendelea kwa jamii ili kuona umuhimu wa
chanjo kuweza kudhibiti ugoinjwa wa Uviko.
Hata hivyo
kwa upande wake Mwakilishi wa Wizara ya
Ofisi ya Rais Tamisemi kutoka Dodoma Mwita Waibe amesema hivi sasa Taifa litaendelea
kutoa chanjo ya Uviko 19 kwa wananchi wake ili wasiendelee kupata madhara
yatokanayo na ugonjwa huo.
Waibe Mwita
ambaye pia ni Mkuu wa Msafara uliopo Tanga kuhamasisha suala la chanjo ya UVIKO
19 kwa mkoa wa Tanga Mwita Waibe ambapo alisema madhara hayo ni yaliyojitokeza
huko nyuma wakati chanjo haikuwepo.
Alisema Taifa
limejiridhisha kwamba chanjo hizo ni salama na hazina madhara ya aina yoyote
hivyo wananchi wahakikisha wanajitokeza kupata chanjo hizo.
Aidha alisema
wanaendelea kuangalia hali upokeaji umekuwaje na changamoto kubwa kutokana na
kwamba mikoa inatofautiana kwa hiyo katika ngazi ya Taifa ikaona ni vizuri
kuwafikia wananchi kuanzisha zoezi la kushawisha kuharakisha uhamamsisha kwa
wananchi ili waweze kupata uelewa
Alisema wataendelea
kufanya utafiti kama serikali kuona uchukuaji wa chanjo na upokeaji baada muda wanakaona kuna changamoto kubwa ni
suala pamoja wapo ni upatikanaji wa chanjo karibu na wananchi na elimu ni
changamoto hayo ndio maana wameamua kutengeneza kampeni harakishi kuhakikisha
wananchi wanapewa elimu.
“Lakini
kuhakikisha chanzo zote zilizokuwa zikitolewa kwenye vituo vichache zinatolewa
kwenye vituo vyote vya kutoa huduma ya afya”Alisema
Awali
akizungumza Afisa Afya wa Mkoa wa Tanga Magoma alisema mkoa huo chanjo ya Uviko
19 ilikuwa inasua walipokea dozi 35000
na walianza rasmi Agosti 3 mwaka huu na ilizinduliwa na Mkuu wa Mkoa huo Adam
Malima ilikuwa ya kusuasua kidogo kutokana
na vituo vilivyofunguliwa kuwa vichache .
Alisema wana
vituo zaidi ya 300 na vituo ambavyo vilikuwa vinatoa huduma ni 33 huku vituo vitatu
kila Halmashauri na baadhi ya maeneo mengine kutoka kituo hadi wananchi walipo
inabidi watembee umbali mrefu au wakalale huko karibu na vituo vya jiriani.
“Lakini pia
kuchelewa kufikia lengo la uchanjaji na tuna lengo la kutazama mabadiliko walizopewa
kumaliza kwenye muda uliowekwa”Alisema
Hata hivyo
alisema sababu kubwa ni vituo kuwa mbalimbali na wananchi Lakini suala hilo
limefanyiwa kazi na halmashauri hivi sasa zimefungua kliniki za mkoba lakini
vituo vinavyotoa bila kujali vya serikali,vya umma au madhehebu ya dini
vitakuwa vinatoa chanjo na elimu inaendelea kwa jamii ili kuona umuhimu wa
chanjo kuweza kudhibiti ugonjwa wa Uviko.
Post A Comment: