Mkuu wa Kitengo cha Wateja Maalum Benki ya NMB, Getrude Mallya akimakabidhi mfano wa hundi yenye thamani ya Sh.milioni 25.5 Mwenyekiti wa Klabu ya Golf ya Lugalo, Brigedia Jenerali Mstaafu, Michael Luwongo ikiwa ni udhamini wa Mashindano ya Mchezo wa Golf ya Mkuu wa Majeshi 'NMB CDF Trophy 2021'. Kulia ni Meneja wa Club ya Golf ya Lugalo, Luteni Kanali, Frank Kaluwa na Meneja Mwandamizi Wateja Maalum wa NMB, Emmanuel Mahodanga wakishuhudia. Benki ya NMB imetoa takribani milioni 60 kwa ajili ya udhamini wa mashindano hayo kiujumla kwa mwaka huu.


Mkuu wa Kitengo cha Wateja Maalum Benki ya NMB, Getrude Mallya (katikati) akizungumza na wanahabari (hawapo pichani) kwenye hafla ya kupokea mfano wa hundi yenye thamani ya shilingi milioni 25.5 kwa ajili ya udhamini wa Mashindano ya Mchezo wa Golf ya Mkuu wa Majeshi 'NMB CDF Trophy 2021'. Kulia ni Mwenyekiti wa Klabu ya Golf ya Lugalo, Brigedia Jenerali Mstaafu Michael Luwongo pamoja na Meneja Mwandamizi Wateja Maalum wa NMB, Emmanuel Mahodanga (kulia) wakishuhudia.

 Benki ya NMB imetoa Sh. 60 Milioni kwa ajili ya kudhamini Mashindano Maalumu ya mchezo wa Gofu ya Mkuu wa Majeshi (CDF ) ambayo yanatarajia kuanza Septemba 17 hadi 19 kwenye viwanja vya Klabu ya Gofu vya Lugalo Jijini Dar es Salaam.


Mashindano hayo hufanyika kila mwaka lengo kuu ni kuuinua mchezo huo pamoja na kukuza vipaji vya wachezaji chipukizi ili kuja kuwa tegemezi siku zijazo.

Akizungumza kwenye hafla ya kukabidhi hundi Mkuu wa kitengo cha wateja maalumu wa NMB, Getrude Mallya, alisema wanajisikia furaha kuwa sehemu ya kufanikisha kufanyika kwa shindano hilo ambalo anaamini mwaka huu litafana kutokana na zawadi nono ambazo zimeandaliwa kwa washindi.

Mallya alisema kiasi hicho cha fedha kimetumika katika kununua vifaa mbalimbali vitakavyo tumiwa na washiriki wa shindano hilo ikiwemo fulana, kofia, bendera na zawadi za washindi ambazo zitatolewa siku ya mwisho.

“Sisi kama NMB tunajisikia furaha kuona shindano la mwaka huu linakwenda kufanyika kwa ubora na mafanikio ya juu kabisa nahii inathibitisha kwamba sisi ndio Benki ambayo inaijali jamii kwa ukaribu kutokana na kudhamini masuala mbalimbali ikiwo ya kimichezo,” alisema Mallya

Meneja huyo pia aliupongeza uongozi wa klabu ya Lugalo, kwa imani yao kwao na kuendeleza mchezo wa Gofu nchini kwa juhudi kubwa wanazozifanya za kuanzisha mashindano mbalimbali na kuwachagua wao kushirikiana nao kuyadhamini.

Kwaupande wake Mwenyekiti wa klabu ya Gofu ya Lugalo Michael Luwango, alisema zaidi ya wachezaji 170, wanatarajia kushiriki mashindano ya mwaka huu ikiwemo vijana wadogo wa shule (Junior) ambao wao ndio watakao fungua mashindano hayo siku ya kwanza Septemba 17.

Alisema tofauti na miaka mingine mwaka huu wametoa nafasi ya watu mbalimbali kushiriki michuano hiyo wakiwemo watu binfsi na wachezaji wakulipwa pamoja na wageni endapo watajisikia kushiriki.

Kiongozi huyo alisema mpaka sasa mwitikio kwa watu wanaoomba kushiriki ni mkubwa ambapo zaidi ya watu 100 wameshathibitisha ushiriki wao na maandalizi yanakwenda vizuri ikiwemo ubora wa viwanja ambavyo vitatumika kwenye shindano hilo.

Naye Katibu wa Chama cha Gofu Tanzania Boniface Nyiti, alisema shindano hilo la Mkuu wa Majeshi lipo kwenye kalenda ya TGU na limekuwa na mchango mkubwa kwa taifa kutokana na kutoa wacheaji wengi ambao wanajenga timu ya taifa.

Nyiti aliwataka viongozi wa klabu za mchezo huo wanaoanzisha mashindano mengine kipindi ambacho shindano la Mkuu wa Majeshi linafanyika watawachukulia hatua ikiwemo kuwafungia kutoshiriki mchezo huo kwa kufuata sheria kwani kufanya hivyo nikuwanyima fursa wachezaji kuto onesha uwezo wao.

Mpaka sasa zaidi ya klabu 10 kutoka mikoa tofauti imethibitisha kushiriki michuano hiyo baadhi yao ni Morogoro, Zanzibar, Arusha, Moshi, Dar es Salaam Gymkhana Klubu na Lugalo .
Share To:

Post A Comment: