Mkuu wa Mkoa wa Simiyu David kafulila amewataka wakuu wa wilaya katika mkoa huo kufungua milango ya ushirikiano na jamii ya wafanyabiashara ili kuchochea maendeleo katika Mkoa huo.
Amesema
 kwa pamoja wanajukumu la kuchangamana katika kuleta maendeleo kwa 
sababu jamii ya wafanyabiashara inamajibu mengi ya changamoto ambazo 
zinaweza kukwamisha maendeleo.
Kafulila
 ameyasema hayo alipokuwa katika hafla ya kumuaga aliyekuwa katibu 
tawala wa Mkoa wa Simiyu Miriam Mbaga iliyofanyika Julai 5, na 
kuhudhuliwa na wakuu wa wilaya zote za mkoa wa Simiyu.
"ushirikiano huo utatumika kujenga mawazo mapya katika jamii,Isiwe
 kwamba mkuu wa wilaya mtu aone kumfikia ni shida, hapana tengenezeni 
milango ya kufikika ili mkutane mkae na kuzungumza maendeleo", alisema.
Aidha
 amewataka wafanyabiashara kuendelea kushiriki katika kuinua ubora wa 
elimu mkoani humo kwa kuichangia sekta ya elimu ili kuendelea kuwapa 
nafasi zaidi wanafunzi waliopo katika madarasa ya mitihani kufanya 
vizuri.
Katika hatua 
nyingine kafulila amewataka wafanyabiashara wa zao la Pamba 
kushirikikiana na wakulima wa zao hili katika kukifanya kilimo cha pamba
 kuwa kilimo chenye tija ili kufikia malengo ya mkoa ya kuzalisha pamba 
tani 500,000.
"Tuzidi kuchanga mawazo, tushirikiane, tumsaidie huyu mkulima tangu hatua za awali ilitija katika shughuli zao iongezeka".

Post A Comment: