Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani mkoani hapa Mrakibu wa Polisi (SP) Nestory Didi akikagua matairi ya Basi la Kampuni ya Ally' Star wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya Safiri Salama Usalama Wetu Kwanza walioianzisha yenye lengo la kupunguza au kumaliza kabisa changamoto za ajali mkoani hapa.

Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani Wilaya ya Singida, Mrakibu Msaidizi wa Polisi (ASP) Robert Sewando, akiwaelekeza jambo SP Didi wakati wa uzinduzi wa kampeni hiyo. 

Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani mkoani hapa, Mrakibu wa Pilisi (SP) Nestory  Didi akizungumza na baadhi ya wajumbe wa kamati ya usalama barabarani mkoani hapa kabla ya uzinduzi wa kampeni hiyo.

Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani mkoani hapa, SP Didi akiwaelekeza jambo askari wa usalama barabarani wakati wa kampeni hiyo.
Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani mkoani hapa, SP Didi akisalimiana na dereva wa Basi la Nyahunge Simon Mtakune wakati wa Kampeni hiyo.

Ukaguzi wa mabasi ukiendelea.

Baadhi ya Wajumbe wa Kamati ya Usalama Barabarani mkoani hapa wakiingia ndani ya moja ya mabasi yaliyokuwepo kituoni kutoa elimu kwa abiri ya usalama barabarani. Kulia ni Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani mkoani hapa, SP Didi.

Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani mkoani hapa, SP Didi, akizungumza na waandishi wa habari na wadau wa usafirishaji.

Mjumbe wa Kamati ya Usalama Barabarani mkoani hapa Fatuma Malenga akizungumza kwenye uzinduzi huo kuhusu matumizi ya barabara kwa watu wenye ulemavu..

Dereva Musa Shikobe akizungumzia  na waandishi wa habari kwenye  uzinduzi huo.

Wakala wa Mabasi ya NBS Daffi Nyandekwa akizungumzia umuhimu wa madereva kufuata sheria na kanuni zilizowekwa za usalama barabarani.


Na Dotto Mwaibale. Singida


JESHI la Polisi mkoani hapa kupitia kikosi cha Usalama Barabarani  (TRAFFIC) limeanzisha kampeni kambande ya utoaji wa elimu ili kumaliza kabisa changammoto za ajali mkoani hapa.

Akizungumza wakati akizindua kampeni hiyo Kituo Kikuu cha Mabasi  Misuna,  Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani mkoani hapa Mrakibu wa Polisi (SP) Nestory Didi alisema wameianzisha kampeni hiyo yenye lengo la kupunguza ajali au kuzimaliza kabisa.

Alisema kampeni hiyo ambayo itakuwa endelevu wameipa jina la Safiri Salama Usalama Wetu Kwanza ambapo watakuwa wakiyakagua mabasi na magari yote na kutoa elimu kwa watumiaji wa wakiwamo abiria.

" Kama mnavyoshuhudia ninyi wenyewe haya matukio ya ajali yanayoendelea kutokea sisi kama jeshi la polisi jukumu letu ni kulinda maisha ya raia na mali zao hivyo tumeamua kutoa elimu na kuhamasisha abiria na makundi mengine yanayotumia barabara wakiwepo watembea kwa miguu, waendeshaji wa bajaj, wanafunzi, bodaboda na walemavu," alisema Didi.

Didi alisema makundi hayo yote yanatumia vyombo vya moto hivyo wanachotaka ni kuona wanakuwa salama pale wanapotumia barabara za umma.

Leo tumeongea na abiria vile vile na madereva kuhusu wajibu wao wanapokuwa wanaendesha magari na tumewaeleza wanatakiwa kuzingatia sheria na kanuni zilizowekwa za usalama barabarani lengo likiwa wanahakikisha wanawafikisha abiria wao salama wanakokwenda.

Aidha Didi alisema abiria nao wanajukumu la kuwasaidia jeshi la polisi kukemea yale maovu yanayofanyika pindi wanapokuwa kwenye safari akitolea dereva anayelipita gari jingine kwenye kona au anayeyapita magari sita kwa wakati mmoja huyo asipokemewa ni lazima ajali zitaendelea kutokea.

Alisema baada ya kuongea na madereva hao wamesema kuanzia leo hii ajali zitabaki kuwa ni historia kwa kuwa watazingatia sheria na kuwa abiria nao watakuwa mabalozi wao wa kutoa taarifa pindi watakapo kuwa wanaona mambo yanaenda tofauti.

Didi alisema wametoa namba za simu popote watakapo kuwa wanaweza kupiga simu au kutuma ujumbe na wao watachukua hatua ya kumkamata dereva husika.

Dereva Musa Shikobe na wakala wa mabasi ya Kampuni ya NBS, Daffi Nyandekwa walisema madereva wanatakiwa wajenge tabia ya kujisimamia wenyewe kwani abiria wanao wabeba ni ndugu zao hivyo wanaposabaisha ajali wanapoteza nguvu za taifa na familia.

Share To:

Post A Comment: