Nteghenjw Hosseah, OR-TAMISEMI


Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Prof. Riziki Shemdoe amesema uhamisho wa watumishi wa Tawala za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa utafanyika mara nne kwa mwaka yaani kila robo ya mwaka husika. 


Akizungumza na waandishi wa habari mapema leo Prof. Shemdoe amesema  kila tarehe 10 ya mwezi unaofuata baada ya robo mwaka kwisha uhamisho utafanyika na majina yatawekwa kwenye tovuti ya Ofisi ya Rais-TAMISEMI.


“Robo kwanza ya  mwaka yaan Julai - Septemba majina ya uhamisho yatakua yanatoka tarehe 10 October , na robo ya Pili Oktoba - Desemba majina ya uhamisho yatatoka Januari 10."


Aliongeza kuwa: " katika robo ya tatu ya  Januari- Machi majina ya uhamisho yatatoka April 10 na robo ya mwisho ya Aprili-Juni majina ya uhamisho yatatoka Julai 10."


Aidha Prof.Shemdoe  alibainisha kuwa majina ya watumishi wote watakaohamishwa yatawekwa kwenye Tovuti ya Ofisi ya Rais TAMISEMI ambayo ni www.tamisemi.go.tz.


Pia amewataka Makatibu Tawala wa Mikoa yote nchini kuwasilisha orodha ya watumishi wa kuhama  ofisi ya Rais-TAMISEMI kila tarehe 05 ya mwezi unaofuata baada ya robo mwaka.


Aidha, aliwataka Makatibu Tawala wote kutokupitisha maombi ya watumishi wanaotaka kuhamia kwenye majiji, manispaa na miji kwa kuwa maeneo hayo yana idadi kubwa ya watumishi.


Aidha, Profesa Shemdoe aliwataka Makatibu Tawala kuwapa kipaumbele watumishi wenye changamoto  mbalimbali zilizothibitishwa.


Pia aliwataka watumishi wote kubaki kwenye vituo vyao na barua  za uhamisho zitatumwa kwa waajiri wao na wataona majina yao kwenye Tovuti ya Ofisi ya Rais TAMISEMI.


Pia aliwataka watumishi kujihadhari na matapeli wanaotaka fedha kwa ajili ya kufanikisha uhamisho wao kwa kuwa Uhamisho ni bure na ni haki ya kila mtumishi.


Alisema kuwa Barua za Uhamisho za kipindi cha nyuma ambazo zilishafika Ofisi ya Rasi TAMISEMI zinashughulikiwa  na majina yatatolewa kila mwezi mpaka Juni 30 kabla utaratibu mpya haujaanza kutumika

Share To:

msumbanews

Post A Comment: