Kaimu Afisa Maendeleo Vijana Mkoa wa Singida, Frederick Ndahani (katikati mwenye fulana ya blue) akikabidhi zawadi ya mbuzi kwa wachezaji wa Timu ya Muhanga FC baada ya kuwa washindi wa  michezo mbalimbali iliyofanyika mjini jana  mkoani haa yenye lengo la kupinga ukatili wa kijinsia kwa wanawake na watoto.
Mkurugenzi wa Shirika ya YUNA,  Ally Mwamzola (kushoto) akizungumzia umuhimu wa michezo. Kulia ni Afisa Michezo wa Manispaa ya Singida, Samweli Mwaikenda na Kaimu Afisa Maendeleo Vijana Mkoa wa Singida, Frederick Ndahani.
Zawadi zikitolewa kwa washindi wa michezo hiyo.
Zawadi zikitolewa
 


Na Dotto Mwaibale, Singida


KAIMU Afisa Maendeleo Vijana Mkoa wa Singida, Frederick Ndahani amevitaka vyama vya mechezo katika Mkoa wa Singida kuhakisha wanawasaidia vijana wa kike kutimiza ndoto za vipaji vyao kupitia agizo la Rais Samia Suluhu Hasssn alipolitoa kwa Waziri wa Utamaduni Sanaa na Michezo wakati akiapisha Baraza jipya la Mawaziri. 

Rais Samia aligiza kuona michezo kwa upande wa wanawake inathaminiwa kama ilivyo  kwa wanaume ,hivyo vyama vya michezo vinawajibu kuweka mikakatika ya kukuza vipaji vya vijana wanawake kuanzia ngazi ya chini,

Ndahani aliyasema hayo wakati akitoa zawadi kwa washindi wa michezo mbalimbali iliyofanyika mjini Singida iliyokuwa na lengo la kupinga ukatili wa kijinsia kwa wanawake na watoto.

Michezo hiyo ilidhaminiwa na mashirika yasiyo ya kiserikali ya Men engage,Youth of United Nation Association Tanzania (YUNA),Youth Movement for Change (YMC), Ofisi ya Mkurugenzi Manispaa na Chama cha Mpira wa Miguu Manispaa ya Singida.

Akimkaribisha mgeni Rasmi Mkurugenzi wa Shirika ya YUNA,  Ally Mwamzola amewataka wanaume kuhakikisha kuwa ukatili kwa wanawake na watoto unatoweka nchini kwani wanaume bado wanashiriki katika ukatili wa kijinsia.

Naye Afisa michezo wa Manispaa hiyo Samweli Mwaikenda ameyashukuru mashirika hayo Kwa kuamua kutumia michezo katika kutoa elimu ya kupinga ukatili wa kijinsia,ameyataka mashirika mengine kuiga mfano kwani kuna faida kubwa kutumia michezo katika kutoa elimu.

Mkurugenzi wa Shirika la YMC Fudelis Lyunde  amemshukuru Kaimu Afisa Maendeleo ya Vijana Mkoa wa Singida, Ndahani kwa kukubali kuja kushiriki na vijana katika michezo na kuomba aendelee na moyo huo wa kuwa karibu na vijana ili wafikie ndoto  zao katika nyanja za michezo na uchumi.

Share To:

Post A Comment: