Katibu Mkuu wa  Umoja  wa Wanamuziki Tanzania  (TAMUFO) , Stella Joel

 


Na Dotto Mwaibale 


UMOJA wa Wanamuziki Tanzania  (TAMUFO) wametoa salamu za rambi rambi kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Samia Suluhu Hassan kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais wa Tanzania Hayati Dkt.John Magufuli kilichotokea Machi 17, 2021katika Hospitali ya Mzela jijini Dar es Salaam. 

Salamu hizo za rambi rambi pia wamezitoa kwa Waziri Mkuu, viongozi mbalimbali, mjane wa marehemu Janeth Magufuli ,Rais wa Zanzibar na wananchi kwa ujumla.

Akizungumza na waandishi wa habari Katibu Mkuu wa TAMUFO, Stella Joel alisema kifo cha Rais Magufuli wamekipokea kwa mshituko  mkubwa na kuwa watamkumbuka  milele daima.

"Tunamshukuruaa Mungu kwa ajili ya maisha ya Rais Magufuli ambaye katika uongozi wake aliinua  Tasinia ya Muziki kwa kuwasaidia wasanii kwa kutatua  changamoto zao mbalimbali" alisema Joel.

Alisema Rais Magufuli alifanikiwa kuzipatia ufumbuzi changamoto hizo kwa kuwa jali wanamuziki hao  upande wa kiafya kwa Kuwapatia Bima ya Afya ya NHIF kwa gharama nafuu kwa ajili ya vipimo na matibabu katika Hospitali za Serikali na za Binafsi.

Joel alisema alikuwa katika maandalizi ya  kufanya maboresho mengi  ili wanamuziki waweze Kufaidika na kazi zao.

" Hakika tutamkumbuka Magufuli  kwa mema mengi aliyoyafanya enzi za uhai wake kama  Rais wa Tanzania"alisema Joel.

Stella alisema kwa niaba ya TAMUFO ana mpongeza Mama Samia Suluhu Hassan kwa kuapishwa kuwa Rais  Wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  na kuwa wana amini atayaendeleza yale  yote ambayo Hayati Rais Magufuli aliyokuwa ameyaanzisha  ambapo wanatambua kwamba kazi hiyo walishirikiana Pamoja.

" Tunakuombea Rais Mama Samia Mungu awe pamoja naye katika kutekeleza yale yote na sisi wanamuziki tumepokea kwa furaha kwa kuapishwa na kuwa Rais wa kwanza Mwanamke katika nchi yetu." alisema Joel.

Share To:

Post A Comment: