Na Alex Sonna, Dodoma

MBUNGE wa Nyasa(CCM), Mhandisi Stella Manyanya, amesema sababu za Chama cha Mapinduzi(CCM), kushinda kwa kishindo kwenye uchaguzi mkuu 2020 ni kutokana na mambo yaliyofanywa na serikali chini ya Rais Dk.John Magufuli.

Akichangia Mpango wa tatu wa Maendeleo wa Miaka mitano bungeni leo, Manyanya amesema wananchi wameelewa namna ambavyo CCM imetekeleza yale yaliyoahidiwa na masikio yao kwasasa wasikiliza mpango huo utawasaidiaje.

“Mpango huu utakuwa na maana zaidi pale tutakapohakikisha unakuwa na manufaa kwa watanzania,”amesema.

Aidha, ameishauri serikali kuhakikisha inakamilisha ujenzi wa bwawa la uzalishaji umeme la Mwalimu Nyerere na ujenzi wa reli ya kisasa katika Mpango huo kwa kuwa miradi hiyo ni mkombozi kwa watanzania.

“Inahitaji mtu ambaye hakuwepo kwenye mgao wa umeme ashangae Bwawa la Nyerere, ni mtu atakayeshindwa kujua tunapoteza mapato kutokana na usafirishaji mizigo kutoa bandarini kupeleka nchi jirani, wana CCM tuna wajibu wa kuelimisha wananchi ili kujua umuhimu wa miradi hii mikubwa,tuendelee kuisemea hadi itakapokamilika,”amesema.

Ameomba serikali kukamilisha miradi hiyo ili isaide upatikanaji wa fedha nyingi za kuhudumia maeneo mbalimbali katika nchi.

“Tuwe na fedha kidogo au zaidi lazima miradi hii ya kimkakati ikamilike, pia tuimalishe ulinzi wa mipaka yetu,”amesema.

Aidha, amesema maendeleo yanakwenda kwa kasi Nyasa na Mbinga kutokana ujenzi wa barabara uliofanywa.

“Niombe yale yaliyoainishwa kwenye Ilani ya uchaguzi ya CCM barabara ya Chiwindi-Mbambay hadi Litui-Amani makoro na daraja la mitomoni kipande kile kinadai katika mpango huu mambo yatekelezwe kama yalivyoahidiwa,”amesema.

Share To:

TANGA RAHA BLOG

Post A Comment: