Kaimu Mkurugenzi Mkuu toka Tume ya Taifa ya Umwagiliaji Bw. Daudi Kaali akiwasilisha mada katika kikao kazi nawataalam wa Kilimo na Ushirika Mkoani Singida
Godwin Mutahangarwa Mwanasheria kutoka Tume ya Taifa ya Umwagiliaji akiwasilisha mada i nayohusu Sheria ya Kilimo cha Umwagiaji ya mwaka 2013 na kanuni zake katika kikao kazi na wataalam wa kilimo Mkoani Singida.


Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji Miundo mbinu tokaTume ya Taifa ya Umwagiliaji Mhandisi Senzia Maeda, akigawa makablasha kwa wataalam wakilimo wakati wa kikao kazi kilichofanyika Mkoani Singida.
Warishiriki wakifuatilia kikao kazi kilichohusisha wataalam wa Kilimo na Ushirika Mkoani Singida
 

Na Mwandishiwetu - Singida


Maafisa Kilimo Ushirika na Umwagiliaji Mkoani Singida, wametakiwa kuzingatia nakutumia kikamilifu Sheria ya Taifa ya Umwagiiaji ya mwaka 2013 na kanuni zake pamoja na Sheria ya usimamizi na uhifadhi wa Mazingira ya mwaka 2004,ilikuweza kunusuru na kulinda vyanzo vya maji,nakutunza Miundombinu ya kilimo cha Umwagiliaji.

Hayo yamesemwa leo na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji Bw. Daudi Kaali, alipoikuwa akizungumza katika kikao kazi na maafisa kilimo ushirika na wahadisi wa Umwagilijiaji Mkoani Singida.

Bw. Kaali amewataka wataalam hao wazielewe sheria hizo na kuhakikisha zinafanyakazi na kueleweka kwa umma na bila kupepesa macho kuwe na utii washeria bila shuruti na kuwachulia hatua wale wote wanaofanya uharibifu wa mazingira kwa kufanya shughuli za kibinadamu kwenye vyanzo vya maji,ilikulinda miundombinu ya kilimo cha umwagiliaji.

“Ni lazima kuzingatia utunzaji wa mazingira kwa kutokukata miti ovyo,nauchafuzi wa miundombinu ya umwagiliaji, mshirikiane na mamlaka husika ili kuweza kunusuru mazingira na kutunza miundombinu hiyo na mazingira,iko wazi kabisa kuwa, miundombinu mingi iliyoharibika inaonekana kuwa chanzo kikubwa ni uharibifu wa mazingira.” Alibainisha.

Akiongelea suala la Uhabirifu wamazingira litokanalo na mabadiliko ya Tabianchi, Bw. Kaali amesema ili kuhimili na kukabiliana na changamoto hiyo, wamekuwa wakihamasiha matumizi sahihi ya teknolojia nyingine sambamba na kupanga mikakati ya pamoja ya kuelendeleza sekta ya kilimo cha umwagiliaji kwa kushirikiana na sektabinafsi.

Akiongea katika kikao kazi hicho, Bw. Suleiman Musunga Afisa Kilimo,Ushirika na Umwagiliaji toka Wilaya ya Mkalama ameushukuru Mradi wa kurejesha Ardhi iliyoharibika nakuongeza usalama wa chakula katika maeneo kame nchini, (Reversing land Degradation trends and increasing food security in degraded ecosystem in semi-arid areas of Tanzania) Unaoratibiwa na Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira ,Kwa kukamilisha hatua ya awali ya kazi ya upembuzi yakinifu na nakuelekea kwenye hatua nyingine ya ujenzi wa mabwawa.


Mradi ambao utawawezesha wakulima katika eneo hilo kuweza kupata maji salama kwa ajili ya kilimo,na wafugaji kwa ajili ya mifugo na matumizi ya jamii iinayoishi maeneo kame.

Kikao kazi hicho cha siku tatu, kilihusisha wataalam wa sekta ya kilimo na umwagiliaji kutoka katika Manispaa ya Singida na wilayaza Manyoni,Ikungi,Itigi,Iramba na Mkalama.

Share To:

TANGA RAHA BLOG

Post A Comment: