Balozi wa Tanzania nchini Kenya, Dkt. John Simbachawene akiiwakilisha Tanzania katika Mkutano Maalumu wa Nane wa Mawaziri wa Mazingira wa Afrika (AMCEN) uliofanyika jana Desemba 4, 2020 kwa njia ya mtandao katika ukumbi wa Ofisi ya Makamu wa Rais jijini Dodoma. 
 
Katika Mkutano huo uliohudhuriwa pia na wataalamu kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais, viongozi hao kutoka barani Afrika wamejadili masuala muhimu na agenda za Mkutano wa Baraza la Umoja wa Mataifa la Mazingira (UNEA-5) utakaofanyika Februari, 2021 na kukubaliana msimamo wa pamoja wa Afrika katika kushiriki Mkutano huo.
Share To:

Post A Comment: