.Afisa tawala Mkuu wa Chuo kikuu cha Sokoine cha Kilimo SUA Bwana Peter Mwakiluma akitambulisha wageni mbalimbali waliofika kwenye ufungaji wa michezo hiyo ya Chibunda Cup 2020 kwa niaba ya naibu makamu mkuu wa chuo utawala na fedha. 

Meneja wa benki ya CRDB tawi la SUA bi. Isabela Kitila akitoa salamu za CRDB ambao ndio wadhamini wakuu wa mashindano hayo.

Meneja wa Benki ya NMB tawi la Wami bwana Harold Lambikile akizungumza neno kwa wanamichezo na wadau waliofika kwenye ufungaji rasmi wa michuano hiyo ya Chibubda Cup.

Naibu makamu mkuu wa Chuo Utawala na fedha Prof. Amandusi Muhairwa akitoa salamu za Chuo kwa niaba ya Makamu mkuu wa Chuo Prof. Raphael Chibunda kuhusu michezo hiyo na umuhimuwake kwa wanajumuiya wa SUA.

Mgeni rasmi kwenye kufunga mashindano hayo ya Wafanyakazi wa SUA Bi. Asteria Mwang"ombe ambaye ni Afisa Michezo wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro akitoa neno kabla ya washiriki na wadau wa michezo hiyo iliyofanyika kwenye viwanja vya michezo vya SUA kwenye kampasi ya Edward Moringe.

Mgeni rasmi kwenye kufunga mashindano hayo ya Wafanyakazi wa SUA Bi. Asteria Mwang"ombe ambaye ni Afisa Michezo wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro akipata maelekezo kwa waamuzi wa mchezo huo wa mpira wa miguu. Mgeni rasmi kwenye kufunga mashindano hayo ya Wafanyakazi wa SUA Bi. Asteria Mwang"ombe ambaye ni Afisa Michezo wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro akikagua timu za mpira wa miguu zilizoshiriki kwenye kucheza mechi ya ufungaji katika ya SUA na Don Bosco. Wachezaji wa mpira wa wavu kati ya timu ya wafanyakazi wa SUA na DON BOSCO wakichuana vikali kwenye mchezo wa kufunga michuano hiyo.

**************************************

Na; Calvin Edward Gwabara.

Watanzania wametakiwa kuhakikisha wanatenga muda kwaajili ya kushiriki kwenye michezo na mazoezi mbalimbali ya mwili ili kuaidia kujenga mwili na taifa la watu wenye afya watakaoleta maendeleo.

Wito huo umetolewa na afisa michezo Manispaa ya Morogoro Bi.Asteria Mwang’ombe kwa niaba ya mkurugenzi wa manispaa hiyo wakati akizungumza na wanamichezo na wanajumuiya wa SUA, Benki ya CRDB na NMB wakati akifunga rasmi michezo kwa ya wafanyakazi wa SUA ya Chibunda CUP.

Bi. Asteria ameupongeza uongozi wa SUA kwa kuamua kuanzisha michezo hiyo ambayo inawakutanisha wafanyakazi wote wa SUA kwenye michezo 20 mbalimbali na kuipongeza benk ya NMB kwa kuamua kufadhili mashinano hayo kila mwaka toka kuanza kwake.

‘’ Naupongeza sana uongozi wa SUA kwa kulipatia kipaumbele swala la michezo kwa wafanyakazi na wanafunzi hasa kwa kuamua kuanzisha idara maalumu kwaajili ya michezo Chuoni hii ni hatua nzuri kwani itaongeza ufanisi na ari ya wanajumuiya wa SUA kushiriki kwenye michezo” Alisistiza Bi. Asteria.

Afisa michezo huyo ameahidi kutoa ushirikiano wowote utakaohitajika katika kufanikisha michezo chuoni hapo ikiwemo swala la walimu wamichezo pale watakapohitajika na kwamba changamoto mbalimbali zilizobainishwa atazifikisha kwa uongozi wa manispaa ili kuona namna ya kuzitatua.

Akizungumza kabla ya kumkaribisha Mgeni rasmi kufunga maichezo hiyo Naibu makamu mkuu wa chou upande wa taaluma Prof. Amandus Muhairwa kwa niaba ya makamu mkuu wa chou Prof. Rapgael Chibubda amesema michezo hiyo ni sehemu ya Chuo kupata wanamichezo ambao watakiwakilisha chou kwenye michezo mbalimbali ndani nan je ya nchi.

Prof. Muhairwa amesema Uongozi wa chou unathamini sana umuhimu wa michezo ndio maana imeweka mikakati mbalimbali ya kuboresha viwanja na kununua vifaa mbalimbali vya michezo kwenye kampasi zake zote ili wafanyakazi na wanafunzi washiriki vyema michezo.

‘’ Kutokana na idadi kuwa ya wanafunzi na wafanyakazi Chuo kinaendelea na jitihada za kuongeza viwanja vipya na vya kisasa ili kukidhi mahitaji na tayari kiwanja kipya cha mchezo wa kikapu cha kisasa Mkoani Morogoro tumemaliza kukijenga na sasa kinatumika hat ana watu wan je ya Chuo” Alifafanua Prof. Mhairwa.

Hata hivyo ametumia nafasi hiyo kuupongeza uongozi wa benki ya NMB kwa kufadhili mashindano hayo ya wafanyakazi kwa miaka minne mfululizo lakini akaomba wadau kuwaunga mkono kwa kujitokeza kufadhili mashindano ya wanafunzi ili ambayo ni mikubwa na yenye mvuto sana.

Kwa upande wake Muwakilishi wa banki ya CRDB bi. Isabela Kitila ambaye ni meneja wa tawi la CRDB SUA ameshukuru uongozi wa SUA kwa kuendelea kuwashirikisha katika michezo hii kwa miaka minne mfululizo kama wadhamini wakuu na kuahidi kuendelea kudhamini kila mwaka.

Isabela amesema kuwa michezo hiyo imewafanya wana CRDB na wanajumuiya wa SUA kuishi kama ndugu na familia kwakuwa michezo imekuwa ikiwaunganisha kwa njia mbalimbali na kufahamiana ikizingatiwa idadi kubwa ya wafanyakazi wa SUA waliopo bila michezo isingekuwa rahisi.

“Niwahakikishie kuwa sisi kama CRDB mlipo tupo na tutaendelea kuwepo katikati yenu kwenye kushiriki michezo hii na mambo mengine hivyo karibuni sana kwenye benki yetu muweze kupata huduma pia za kibenki mbalimbali kulingana na mahitaji yenu maana sisi na nyinyi ni familia moja” Alisistiza Isabela.

Nae Menejea wa benki ya NMB tawi la wami bwana Harold Lambileki amesema leo wao ndio mara ya kwanza kushiriki kwenye michezo hiyo hivyo wamekuja kujifunza kuona kinachofanyika ili na wao waweze kushiriki kikamilifu kama wadau muhimu wa michezo nchini.

Amesema Wanamichezo ndio wateja wa huduma za benki ya NMB hivyo watahakikisha kwenye michezo ijayo nao wanakuwa sehemu ya wadhamini wa michezo hiyo muhimu ya wafanyakazi lakini pia kwenye michezo mingine ili kusaidia kuboresha afya na kuimarisha undug una ushirkiano.

Michezo hiyo ya wafanyakazi wa SUA ilianza miaka minne iliyopita na imekuwa ikishidanisha wafanyakazi wote kwenye michezo mbalimbali 20 na mwisho wa michezo hiyuo zawadi mbalimbali zinatolewa ikiwemo vikombe,medali na fedha taslimu wa washindi

Share To:

TANGA RAHA BLOG

Post A Comment: