Mgombea Ubunge wa Jimbo la Manyoni Mashariki mkoani Singida kupitia  tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dkt. Pius Chaya, akihutubia wananchi na wana CCM katika mkutano wa hadhara wa uzinduzi wa kampeni ulioandaliwa na CCM wilayani hapa jana.
Katibu wa Umoja wa Vijana CCM Wilaya ya Manyoni, Wambura Igembya akizungumza kwenye mkutano huo. 
Mgombea Udiwani wa Viti Maalumu wa Tarafa ya Kintinku, Joyce Kalikawe, akizungumza kwenye mkutano huo.

Mgombea Udiwani wa Viti Maalumu wa Tarafa ya Kintinku, Sara Diria, akizungumza kwenye mkutano huo.


Dotto Mwaibale na  Alinikisya Humbo, Manyoni


MGOMBEA Ubunge wa Jimbo la Manyoni Mashariki mkoani Singida kupitia  tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dkt. Pius Chaya amesema iwapo wananchi watampa ridhaa ya kumchagua kazi kubwa atakayoanza nayo ni kuwavuta wawekezaji.

Chaya aliyasema hayo jana wakati akihutubia wananchi na wana CCM katika mkutano wa hadhara wa uzinduzi wa kampeni uliofanyika stendi ya shimoni ulioandaliwa na CCM wilayani hapa.

" Mkinichagua kuongoza jimbo ili ahadi yangu kubwa kwenu nitahakikisha nawavutia wawekezaji waje kuwekeza kwa kuanzisha viwanda na kutafuta masoko ili kukuza wa wana Manyoni na Taifa kwa ujumla. 

Alisema Serikali yetu imejikita zaidi katika uchumi wa viwanda hivyo kwa kushirikiana kwa pamoja na wana CCM wenzake atahakikisha wanaitekeleza ilani ya chama hicho ya 2020-2025 kwa vitendo kwa kuwavuta wawekezaji" alisema Chaya huku akishangiliwa.  

Akizungumzia suala la kilimo na ufugaji, Dkt, Chaya alisema kuna haja ya kujenga mabwawa yatakayo tumika kuvuna maji kwa ajili ya kunywesha mifugo na kulima kilimo cha umwagiliaji jambo ambalo litapunguza changamoto ya ajira kwa vijana na kuongeza pato kwa Taifa.

Aidha kuhusu changamoto ya mawasiliano ya barabara inayounganisha wilaya ya Chemba na Manyoni kupitia Kata ya Makanda kwenda kata ya Kintinku ambayo imekuwa ikikata mawasiliano nyakati za mvua,  Chaya ameahidi kutafuta utatuzi wake mara moja baada ya kuchaguliwa.

Dkt. Chaya alitaja vipaumbele vyake vingine kuwa ni pamoja na maboresho ya huduma ya afya, huduma ya maji, elimu na sekta ya kilimo ambayo ndio uti wa mgongo kwa watanzania.

Aliongeza kuwa endapo watampa ridhaa atahakikisha anasimamia kikamilifu nyanja mbalimbali za kijamii na kiuchumi kwa mustakabali wa maendeleo ya jimbo hilo na taifa kwa ujumla.

Alisema atahakikisha anasimamia vyema fedha katika ukamilishaji wa miradi ya maji iliyopo kuondoa kero hiyo, sanjari na kupigania kuwa na hospitali mpya ya kisasa ya wilaya, huku katika kukuza sekta ya kilimo na mifugo bila kusahau suala la elimu na michezo, ameahidi kuipa kipaumbele.

Mgombea Udiwani wa  CCM kata ya Manyoni, Simon Mapunda ametaja vipaumbele vyake kwa kata hiyo mara atakakapochaguliwa  kuwa ni kuongoza kata hiyo  kuwa ni pamoja  Afya, elimu na maji. 

Alisema kwa ushirikiano wa wananchi na halmashauri atahakikisha wanaboresha miundo mbinu mbali mbali ambayo ni pamoja na  suala la ujenzi wa soko jipya la kisasa, afya pamoja na elimu ili kuleta heshima na hadhi ya mji wa Manyoni ikizingatiwa upo karibu na makao makuu ya nchi.

Juu ya ushirikiano katika kipindi cha kampeni kwa wagombea walioshindwa kwenye kinyang'anyiro cha kura za maoni, John Madindilo na Moses Ntandu wameahidi ushirikiano.

Kwa upande wake aliyekuwa diwani wa kata hiyo Magembe Machibula mbali ya kueleza aliyofanya kipindi chake kwa ushirikiano mwema na wananchi na serikali katika sekta mbalimbali ambayo ni pamoja na uboreshaji elimu, afya, maji na ardhi, alisema pamoja na juhudi hizo lakini bado kuna changamoto ambazo zinahitaji kutatuliwa.

Ameongeza kuwa juu ya suala la kuongeza maeneo ya utawala kwenye Kata ya Manyoni yenye kadirio la wakazi 60,000 na kuunda kata nyingine, Machibula akimnadi mgombea huyo amemuomba kubeba jambo hilo, huku akiahidi ushirikiano.

Kwa niaba ya madiwani wote wa jimbo la Manyoni mashariki, Joyce Kalikawe ambaye ni mteule wa udiwani viti maalumu kutoka CCM, akiomba kura kwa Rais, Wabunge na Madiwani wa chama hicho, amewasihi wanawake wenzake kukiamini Chama Cha Mapinduzi.

Kwa upande wake Munde Tambwe Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Tabora na Mlezi wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Singida alimkabidhi Dkt, Pius Chaya ilani ya chama hicho ya 2020-2025 itakayotekelezwa kwa miaka mitano ijayo nakuwaomba wananchi kumpa kura nyingi Mgombea urais kupitia CCM, Dkt. John Magufuli na Wabunge na Madiwani.

Share To:

Post A Comment: