Na Mwamba wa Kaskazini
Mpaka leo tafiti mbalimbali zinampa Rais Dkt John Pombe Magufuli ushindi wa zaidi ya asilimia 85 katika uchaguzi mkuu wa Oktoba 28 mwaka huu dhidi ya wagombea wengine.


Bila shaka, hili linatokana na uchapakazi wake pamoja na uzalendo wake kwa taifa hili.

YAPO MENGI YA KUJIVUNIA  CHINI YA RAIS MAGUFULI
Kwa miaka Mitano iliyopita Tumeshuhudia  Rais John Pombe Magufuli akiendelea Kuwa Mfuasi Mzuri wa  Falsafa za Mwalimu Julius Nyerere ambaye Kupitia Dira ya Uongozi wake,  alisisitiza sana Kujenga Taifa la Kijamaa na Kujitegemea.

 Niendelee Kwa Kusema Kuwa  Rais Magufuli Mara baada ya kuingia tu Madarakani ili Kujenga Taifa la Kujitegemea Kiuchumi alifanya yafuatayo na kuendelea kuyasimamia Kikamilifu; Ameboresha Ukusanyaji  Mapato ya serikali yatokanayo na Kodi  Kutoka Bilioni 850 Mwaka 2015  hadi  Kufikia Trilioni 1.3 ( Disemba 2019 )  Fedha za Kitanzania na Kwa Mapato yasiyo ya Kodi Rais Magufuli amefanikiwa kwa Kiasi Kikubwa Kuboresha Ukusanyaji wake  na Kuongezeka Kutoka Chini ya Bilioni 688 mwaka 2014/2015 hadi Kufikia Trilioni 2.4  Fedha za Kitanzania Mwaka 2018/2019

 Aidha Rais Magufuli pia amefanikiwa sana Katika  kudhibiti Matumizi yake na  Kwa Kiasi kikubwa   ameelekeza fedha  hizo kuwahudumia Watanzania Kwa kuwaletea Maendeleo Katika Sekta zote. Rais Magufuli amefanikiwa Kwa Kiasi Kikubwa Kuimarisha Utendaji Kazi Serikalini, Maadili na Nidhamu Kwa Watumishi wote wa Serikali ( UMMA ) na Katika hili hakusita Kuchukua hatua za kinidhamu hadharani  Kwa Watumishi Walioshindwa Kufanya Kazi kwa Weledi, Nidhamu, Maarifa na Uadilifu.

Rais Magufuli toka ameingia madarakani mwaka 2015 alituahidi Kulinda Raslimali za Taifa letu ili kuhakikisha Urithi wa Raslimali tulizojaaliwa na Mwenyezi Mungu zinabaki Kuwanufaisha Watanzania wote na hapa ningependa kuwakumbusha Watanzania Kwa kurejea  katika lile Sakata la makinikia na Madini yetu kama mfano mmoja wapo.

Mosi kabisa, Mageuzi Makubwa sana yamefanyika  Ikiwa ni pamoja na Kuanzisha Wizara Mahsusi ya Madini, Kudhibiti Utoroshaji  na Usafirishaji wa Madini ghafi nje ya Nchi, Rais Magufuli ameanzisha Masoko ya Madini Kila Mkoa ambapo Kupitia hili Mapato  yatokanayo na Madini sasa yamekuwa na yanaonekana wazi. Serikali ya Rais Magufuli kupitia Bunge la JMT ilitunga na kupitisha Sheria ya Kulinda Rasilimali za Taifa ya Mwaka 2017 (  The Natural Wealth and Resources Permanent Sovereignty Act, 2017 ) Ikiwemo Madini.

 Kupitia Sheria hii, tumeshuhudiwa Kwa mara ya Kwanza  Watanzania wanamiliki Rasilimali zao kwa Nguvu za Kisheria Kama akina Saniniu Laizer😅 Mzee wa Tanzanite.

Ni kupitia Sheria hiyo pamoja na Jitihada za Rais  Magufuli na Serikali yake, wale Waliokuwa wanatunyonya “Mabeberu"  Walisalimu Amri na Kukubali Kutulipa Watanzania Malipo ya Fidia ya *Dola za Kimarekani Milioni Mia Tatu ( us-dollars 300 Millions ) ambazo Kampuni ya Barrick  ilikubali Kutulipa Kufuatia Majadiliano na Makubaliano na Tayari Dola za Kimarekani Milioni Mia Moja ( us –dollars 100 Millions ) tumekwisha lipwa.

 Mafanikio mengine Kupitia Makubaliano ya Serikali ya Rais Magufuli na Kampuni ya Barrick*  ni pamoja na Kuanzishwa  kwa Kampuni ya Twiga Minerals Company  ambayo Serikali yetu inamiliki 16%  na Kampuni ya Barick 84% .

Watanzania tunayo mengi sana  ya Kujivunia Kama Taifa linalohitaji Kusonga Mbele  Kimaendeleo, Kiuchumi na Kidemokrasia pia.

Kwa Uchache tu, nakukumbushia Machache Miongoni Mwa Mengi aliyoyafanya:
• Arusha amepeleka Miradi Mkubwa wa Maji: Bilioni 520 Arusha Jiji, Mradi wa Maji Chanzo toka Mto Simba Kilimanjaro Bilioni 16, Ujenzi na Upanuzi wa Barabara  Kuwa njia nne Kutoa  Ngaramtoni hadi USA River  ikiwemo zile za Mchepuko / Mzunguko ( By-Pass ) ambazo zimekamilika zaidi ya Bilioni 164, Tumejengewa Hospitali  Mpya  za Wilaya  ya Longido ( Bilioni 2 ), H/Wilaya Karatu Bilioni 1.5, H/ Wilaya Ngorongoro ( Bilioni 1.8 )  na H/Wilaya Arusha ( Bilioni 1.5 ) Pamoja na Kuboresha Hospitali za zamani.

• Ununuzi wa Ndege Mpya 11 Kwa fedha zetu za ndani sio mkopo, yaani CASH PAYMENTS ( Boeing 787-8 Dreamliners ziko 2, Airbus 220-300 ziko 2, Bombadier Dash 8  Q-400 ziko 4 na  nyingine Tatu kuja Miezi michache ijayo. Hapa Serikali ya Dkt. Magufuli imeboresha huduma ya Usafili wa Anga kupitia  Shirika  la  Huduma  ya  Usafirishaji Kwa  njia ya  Anga Tanzania      ( ATCL )ambapo Mapato yameongezeka na Utalii umeongezeka zaidi na Kuongeza Pato la Taifa.

• Ujenzi Mradi Mkubwa wa Uzalishaji  Umeme wa Mwl. Nyerere - Megawati 2115 ( Stieglers Gorge ) utakaogharimu  Pesa zetu za ndani Trilioni 6.5 ( Dola za Kimarekani Bilioni 2.9 ) hadi kukamilika Kwake na Kazi inaendelea vizuri sana.

• Mradi Mkubwa wa Ujenzi wa Reli ya Kisasa  ya Treni ya Umeme ( SGR ) Kutoka  Dar es salaam hadi Mwanza. Maendeleo ya Mradi wa Kipande cha Kutoka  DSM-Morogoro na Kutoka Morogoro hadi Makutupora  Dodoma utagharimu Trilioni 7.062  fedha zetu wenyewe kwa kodi zetu.  Kipande cha Mwanza –Isaka-Dodoma Maandalizi yanaendelea vizuri. .
• Rais Magufuli hakuwasahau wana Dar es salama. Kawapelekea Miradi ya Kutosha;

 Miradi Mikubwa ya Ujenzi wa Madaraja na  Barabara za Juu  kama: Mradi wa Ujenzi wa Barabara za Juu Ubungo ( Ubungo Interchange Flyover (  zaidi ya Bilioni 200 zimetumika ), Mradi wa Ujenzi wa Barabara za Juu - Mfugale flyover  ( zaidi ya Bilioni 247  ), Mradi wa Salender Brigde  na Daraja la Majini Ziwa Viktoria  Busisi – Kigongo urefu wa Km 3.2 litakalo gharimu Bilioni 699 pesa za Kitanzania hadi kukamilika kwake, ujenzi unaendelea vizuri sana.

• Mpango wa Elimu Bila Malipo Kuanzia Shule Msingi hadi Sekondari ambapo Serikali ya JPM inatenga zaidi ya Bilioni 23 Kila mwezi ili kugharamia Elimu Msingi hadi Sekondari.

• Rais Magufuli ametimiza ndoto  ya  Baba wa Taifa Hayati  Mwl. JK Nyerere ya Mpango wa Kuhamishia  Serikali Dodoma. Dodoma sasa inapendeza, vijana wamepata ajira na Maendeleo Mkoa wa Dodoma sio suala la kuuliza Mwenye Majicho atizame mwenyewe.

• Mpango wa Kujenga Vituo vya Afya Kila Kata Nchini Kote Kwa Maeneo yasiyokuwa na Vituo vya Afya.

• Rais Magufuli pia ameweza Kujenga Hospitali  Mpya za Wilaya  Katika Halmashauri 67 Nchini Kote.

• Uboreshaji wa Viwanja vya Ndege ikiwemo Jengo Jipya la Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere ( JNI ), Mradi uliogharimu Bilioni 722 Fedha zetu za ndani. Sambamba na hili tunakumbuka pia Ununuzi na Ujenzi wa Mifumo ya Kuongozea Ndege Katika Viwanja vya Ndege vya JNIA Dar es salaam, Mwanza, Kilimanjaro na  Songwe Kwa gharama ya Bilioni 67.3 Fedha zilizotolewa na Serikali ya Rais Magufuli.

Ndugu zangu ni Mengi ya Kujivunia Kutokana na Uongozi wa Rais Magufuli. Nimeshindwa Kuyaandika yote maana ni Mengi sana.  

Lakini hawa wengine , tujiulize wamefanya nini  kwa taifa hili walipokuwa watumishi, au wabunge  kumzidi   JPM??

1. Wengine walipokuwa  wabunge hawawezi kukuonesha hata mtaro wa maji waliosaidia kuujenga jimboni;

2. Wakiwa wabunge walisifika kwa kuzuia wananchi kushiriki maendeleo;

3. Wakiwa wabunge hawakuwahi kupitisha bajeti yoyote kwa maendeleo ya wananchi zaidi ya kuzikataa zote;

5. Kiongozi sahihi ni lazima Asisitize amani, Lakini wapo wagombea  wengine hakuna mahali popote wamesisitiza amani zaidi ya vurugu.

6. Kiongozi Bora ni lazima awe mzalendo wa taifa lake...Lakini wapo wengine Wanaonekana kuamini katika mataifa ya nje kuja kuwasaidia kwa kufikiri na kutekeleza.

7. Wapo waonaponda kila kitu cha nchi wakiwemo Waasisi wa Taifa

8. Wapo waonaponda kila maendeleo yaliyopo nchini ikiwemo barabara wanazopita, maji wanayokunywa, umeme wanaoutumia kila siku n.k
Share To:

msumbanews

Post A Comment: